Shaffih Dauda: Mukoko Tonombe kauzwa kwasababu ya red card ya Fainali ya F.A

Shaffih Dauda: Mukoko Tonombe kauzwa kwasababu ya red card ya Fainali ya F.A

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Akiwa katika kipindi cha michezo cha Sports Extra ya Clouds Fm, mchambuzi Shaffih Dauda amesema sababu kuu ya Mukoko kuuzwa na Yanga kwenda TP Mazembe ni kadi nyekundu aliyoipata katika mchezo wa Fainali ya FA dhdi ya Simba.

Katika mchezo huo, Mukoko Tonombe alimpiga kiwiko John Bocco na kupewa red card na kusababisha Yanga kupoteza mchezo huo.

Shaffih aliongeza "Ndani ya Yanga kuna wahafidhina walimuona Mukoko kama aliuza mechi, hivyo wakapanga kumuondoa kikosini taratibu"

Haiingii akilini, mchezaji bora wa msimu uliopita eti kushindwa kupata nafasi katika kikosi hiko, Mukoko kaondolewa kimchongo, aliongeza Shaffih.

Je, unamuunga mkono Shaffih au unampinga?
 
Hili lijamaa nalo linazeeka vibaya anyway kumuacha mukoko ni kosa kubwa na tutakuja kujutia hapo mwakani tukienda kimataifa
Bangala ataumia na benchi yupo zawadi. Tutatundikwa magoli vibaya mno.

Leo nimeumia Sana hii tabia ya kuacha wachezaji walioizoea Team pasipo mantiki itatukost Sana.

Wameleta winga na kuacha kiungo mawinga yanga wapo kama utitiri..!
 
Akiwa katika kipindi cha michezo cha Sports Extra ya Clouds Fm, mchambuzi Shaffih Dauda amesema sababu kuu ya Mukoko kuuzwa na Yanga kwenda TP Mazembe ni kadi nyekundu aliyoipata katika mchezo wa Fainali ya FA dhdi ya Simba...?
Tukianza na mechi yenyewe ya fainali ya FA pale tabora nani alikua bora kuliko mwingine kati ya simba na Yanga? Jibu ni rahisi sana kwa wakati ule simba alikua bora sana.

Swali lingine je,mukoko asingetoka yanga wangeshinda ile game? Jibu ni ni rahisi tu "labda" ila kwa mtazamo wangu ni "hapana". Kwanini nasema hapana! Ni kwa sababu Simba alikua bora sana kuliko yanga, wengine moyoni wataguna mbona Yanga alimfunga simba kwenye ligi.. Yap ni kweli alimfunga tunajua.. Ila tujikumbushe nyuma kidogo msimu mmoja nyuma zaidi simba hakuwahi kumfunga yanga kwenye ligi ila nusu fainali ya FA alimfunga goli nne moja.. Kwahiyo kwa kigezo cha ubora bado simba wangeshinda tu.

Sasa nije kwenye hoja ya Shaffih dauda kua Wanazi wa yanga wamemuuza mukoko kwenda TP mazembe kisa " aliuuza mechi". Kwanza sijui kama in kweli kauzwa au ni "maneno" tu japo nilimsikia Mbumbuli akisema wamemuuza Mukoko pia kwa kumchukua Ushindi sasa sijajua kwanini bado mukoko yupo jangwani maybe dirisha la usajili Congo bado halijafunguliwa au anamalizia msimu!? Sijui.

Lakini hoja hii japo inaweza kua na ukweli mwingi ndani yake lakini mi naamini Kuna inshu haipo sawa kati ya Yanga na mukoko na nahisi tatizo lilianzia kwenye dirisha kubwa lililopolita coz kipindi Tuisila Kisinda anaondoka yanga na mukoko pia alitakiwa kusepa sema yanga ni kama walikwamisha hilo dili sasa nazani hapo Kuna inshu ilitokea ambayo imepelekea Mukoko kutolewa kafara maana ukirejera lile tukio la red card mashabiki wa yanga walikua upande wa mukoko hakuna aliyemlaumu...

Nipo kwenye group la WhatsApp la yanga makao makuu.. Wadau wote walimtetea mukoko sasa hao wahafidhina ni kina nani kama mashabiki walikua upande wa mukoko?? Anyway huenda hoja yake INA mashiko.. Ngoja tuendelee kunywa mchuzi nyama tutazikuta chini.

#mwananchi mwema [emoji172][emoji169]
 
Hili lijamaa nalo linazeeka vibaya
Anyway kumuacha mukoko ni kosa kubwa na tutakuja kujutia hapo mwakani tukienda kimataifa
Bangala ataumia na benchi yupo zawadi
Tutatundikwa magoli vibaya mno.

Leo nimeumia Sana hii tabia ya kuacha wachezaji walioizoea Team pasipo mantiki itatukost Sana..
Wameleta winga na kuacha kiungo mawinga yanga wapo kama utitiri..!
Nami nimeumia ile mbaya lakini kwa sasa sitasema sana, nasubiri kuona kiwango kitakachooneshwa na Ushindi!!

Kwa mujibu wa MwanaSpoti la siku kadhaa zilizopita, sharti la Mazembe kumwachia Ushindi ilikuwa ni wao kupatiwa Mukoko!!

Ushindi alikuwa Mazembe kimwili tu lakini akili yote ilikuwa Yanga kutokana na yale aliyokuwa anayasikia kwa wana!!

Hata hivyo, tusiwe na hofu sana... vijana wanakula life la maana sana pale AVIC Town jambo litakalofana kuvuta Wa-Congo wengi zaidi kuja Bongo! Kuna kila dalili, it's a matter of time kabla Wachezaji wanaocheza ndani DRC chaguo lao la kwanza kwa kanda hii kuwa TP Mazembe na baada ya hapo ikawa Yanga na Koro!

Sema linapokuja suala la kupigana jihad, I'll always remember him!
 
Nami nimeumia ile mbaya lakini kwa sasa sitasema sana, nasubiri kuona kiwango kitakachooneshwa na Ushindi!!

Kwa mujibu wa MwanaSpoti la siku kadhaa zilizopita, sharti la Mazembe kumwachia Ushindi ilikuwa ni wao kupatiwa Mukoko...
Mimi pia nahisi hivyo lakini ni vyema aende huko ili acheze kuliko huku nabi alikuwa anamuweka benchi
 
Akiwa katika kipindi cha michezo cha Sports Extra ya Clouds Fm, mchambuzi Shaffih Dauda amesema sababu kuu ya Mukoko kuuzwa na Yanga kwenda TP Mazembe ni kadi nyekundu aliyoipata katika mchezo wa Fainali ya FA dhdi ya Simba...
Huyo naye kanjanja tu,kwani wachezaji hawauzwagi,?Atwambie basi na TK master aliuzwa kwa sababu gani?
 
Inawezekana Mukoko alikuwa analazimisha kupangwa , yaan alikuwa anaona Kama anaonewa kukaa benchi.

Sasa ikawa Yanga Waamue Kati ya Nabi na Mukoko mmoja aondoke. Maana katika jicho la Soka mchango wa Mukoko bado ulihitajika Jangwan.
 
Akiwa katika kipindi cha michezo cha Sports Extra ya Clouds Fm, mchambuzi Shaffih Dauda amesema sababu kuu ya Mukoko kuuzwa na Yanga kwenda TP Mazembe ni kadi nyekundu aliyoipata katika mchezo wa Fainali ya FA dhdi ya Simba...
Tatizo la huyu shaffi ni kutaka kutoa maoni kwenye kila suala

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
huyu jamaa atuachie yanga yetu, ajikite kumchambua pablo franco aka kocha wao wa mchongo, nyambafu
 
Akiwa katika kipindi cha michezo cha Sports Extra ya Clouds Fm, mchambuzi Shaffih Dauda amesema sababu kuu ya Mukoko kuuzwa na Yanga kwenda TP Mazembe ni kadi nyekundu aliyoipata katika mchezo wa Fainali ya FA dhdi ya Simba...
Fallacy of argumentation.........mjinga pekee ndiyo anaweza kumuelewa
 
Back
Top Bottom