Shahidi: Mwalimu Mkuu anayedaiwa kumlawiti Mwanangu alimwambia 'ukisema nitakupiga nikuvunjevunje'

Shahidi: Mwalimu Mkuu anayedaiwa kumlawiti Mwanangu alimwambia 'ukisema nitakupiga nikuvunjevunje'

Kesi Namba Cc 32444/24 inayomkabili Mwalimu Saleh Ayoub (39) mkazi wa Salasala Jijini Dar es Salaam kutoka Shule ya Msingi Green Acres iliyopo Mbezi Africana, anayedaiwa kumlawiti Mwanafunzi wake (11) imeendelea Februari 17, 2025, ambapo shahidi mmoja kati ya sita upande wa Jamhuri amekamilisha kutoa ushahidi.

Shahidi huyo (jina linahifadhiwa) ambaye ni Mama Mzazi wa Mtoto anayedaiwa kufanyiwa tukio hilo, ameiambia Mahakama kwamba alifahamu kwa mara ya kwanza baada ya mtoto wake kumueleza kuwa anapata maumivu wakati wa haja kubwa huku akidai maumivu hayo alianza kuyapata tangu alipoanza kuingiziwa uume kwenye sehemu yake ya haja kubwa.

Shahidi huyo ameendelea kueleza kwamba alipoanza kumdadisi mtoto kutaka kujua nani alikuwa anamfanyia kitendo hicho, amedai mtoto alipata 'kigugumizi' kabla ya kueleza alikuwa akifanyiwa hivyo na Mwalimu Mkuu aliyefahamika kwa jina Saleh Ayoub.

Anaeleza kwamba Mtoto huyo wa kiume (jina linahifadhiwa) alimueleza kwamba Mwalimu Saleh Ayoub akiwa shuleni alikuwa anamtoa darasani na kumpeleka kwenye chumba kisicho na matumizi pamoja na kwenye choo kisha kuanza kumuingizia uume kwa nguvu kwenye sehemu ya haja kubwa na kisha kuutoa kwa nguvu na baada ya hapo kumtaka ajisafishe.

Akiongozwa na Wakili wa Jamhuri, shahidi amedai kwa maelezo ya mtoto wake, alimwambia kwamba amekuwa akimfanyia kitendo hicho mara nyingi na Mwalimu huyo huku akimtisha kwa kumwambia akisema popote atampiga amvunjevunje.

Katika hatua nyingine shahidi adai kwamba majibu ya Daktari kutoka Hospitali ambayo mtoto alipelekwa kwa ajili ya kufanyiwa vipimo mara baada ya kupewa mwongozo na Jeshi la Polisi, yalieza kwamba mtoto alikuwa ameharibika sana sehemu ya haja kubwa.

Akifanyiwa Cross-Examination na Wakili wa utetezi, Faraji Mangula, shahidi ameulizwa kama anafahamu au anahusika na taarifa ambazo zimekuwa zikiripotiwa Mtandaoni kuhusu shauri hilo, pia kama ameona taarifa hizo zinazodaiwa kuripotiwa, akijibu suala hilo shahidi amekana na kusema hafahamu juu ya uwepo wa taarifa hizo kwenye chombo cha habari ambacho hakikutajwa jina lake.

Baada ya shahidi huyo kukamilisha kutoa ushahidi wake, Hakimu Mkazi Mkuu, Hawa Magesa ameahirisha shauri hilo linalosikilizwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni mpaka Februari 26, 2025 huku akisisitiza kuwa mpaka Februari 2025 anataka mashahidi wawili wawe wamemaliza kutoa ushahidi wao ili kuepuka shauri hilo kucheleweshwa.

Itakumbukwa, mshtakiwa huyo alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza siku chache baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuhoji sababu za kutofikishwa Mahakamani kwa Watuhumiwa aliodai wanahusika na vitendo vya ukatili katika Shule ya Green Acres iliyopo Mbezi Africana, Jijini Dar es Salaam.

Kusoma taarifa za nyuma za kesi hii, bofya:
~ Walimu wa Shule ya Green Acres (Dar) wanaotuhumiwa kulawiti na kuwadhalilisha Wanafunzi, wanalindwa na nani?

~ Dar: Mwalimu wa Shule ya Green Acres anayedaiwa kumlawiti Mwanafunzi wake afikishwa Mahakamani

~ Watu 6 kutoa ushahidi Kesi ya Mwalimu wa Shule ya Green Acres anayetuhumiwa kumlawiti Mwanafunzi wake

~ Ushahidi wa Kesi ya Mwalimu wa Green Acres, Saleh Ayoub anayetuhumiwa kumlawiti Mwanafunzi wake kuanza kutolewa Februari 6, 2025

~ Kesi ya Mwalimu wa Shule ya Msingi Green Acres anayetuhumiwa kulawiti Mwanafunzi yaahirishwa Mwezi mzima, Hakimu apata hudhuru

~ Dar: Kesi ya Mwalimu Saleh Ayoub anayedaiwa kumlawiti Mwanafunzi yaahirishwa hadi Februari 17, 2025
Inaumiza sana hii.
 
Siyo kubaka, kalawiti na Ripoti ya Daktari inaonesha mtoto kalawitiwa hadi kuharibika, then unakuja kusema hudhani kama mtoto kaumizwa, like seriously?
Back in days i examined a 6 yrs old F whom her mother claimed she was defiled by his biological father
Technically it was a police case
Kid was raped and defiled yes but not by his father
It happens dunia uwanja wa vita
 
Shida ya haya mambo unaweza kuwaza hivi Hawa watu wana akili kweli , yaani unamnajisi mtoto kweli! .

Lakini katika tafiti zangu ni kuwa kuna issues za ushirikina . Mfano unaweza kuambiwa na mganga ,tafuta mtoto wa kiume ufanye hicho kitendo Mara kadhaa ..kama ni Wa kike unaambiwa mtafute ambaye hajakutana na mwanaume na awe ndugu wa karibu ufanye Naye Hilo tendo . Kwangu Mimi nikionaga waganga wa kienyeji najisikia hata kuwaua kabisa . MUNGU anisamehe Sana kwa mawazo haya mabaya .

Kuna mpangaji wangu aliletaga UPUUZI huu na nilimswaga mapema tu.
 
Mweee! Mie nashindwa kuelewa why watu kama hawa wanafikishwa mahakamani
Maza angemalizana na mtuhumiwa kimafia tu.

Mtoto wa wa miaka 11 tena wa kiume anakuvutia kitu gani, humhurumii.

Watu wa namna hii ni kumalizana nao kimtaa mtaa.
 
Back in days i examined a 6 yrs old F whom her mother claimed she was defiled by his biological father
Technically it was a police case
Kid was raped and defiled yes but not by his father
It happens dunia uwanja wa vita
Yes ni ngumu kuamini mpaka ushuhudie.

Nilipataga msala, nikabahatika kupata dhamana, ila siku ya kesi ikifika nilikuwa nikienda mahakamani nawekwa selo kama washtakiwa wengine.
Nikakutana na jamaa anatuhumiwa kumbaka binti yake, kumbe mkewe kapata mwanaume mwingine lengo lake ni jamaa afungwe achukue nyumba. Jamaa alikuja kuokolewa na ushahidi wa daktari ndo alikanusha (japokuwa hela ya yule mama dokta alikula) jamaa aliachiwa ila akabaki analia tuu.
 
Yes ni ngumu kuamini mpaka ushuhudie.

Nilipataga msala, nikabahatika kupata dhamana, ila siku ya kesi ikifika nilikuwa nikienda mahakamani nawekwa selo kama washtakiwa wengine.
Nikakutana na jamaa anatuhumiwa kumbaka binti yake, kumbe mkewe kapata mwanaume mwingine lengo lake ni jamaa afungwe achukue nyumba. Jamaa alikuja kuokolewa na ushahidi wa daktari ndo alikanusha (japokuwa hela ya yule mama dokta alikula) jamaa aliachiwa ila akabaki analia tuu.
Mambo ni mengi duniani hapa ukiskia kesi yoyote kwenye media usihukumu
 
Haya mambo muda mwingine ni kuyaacha km yalivyo, kuna mengi nyuma ya Pazia.
Kuyaacha kama yalivyo kiaje mkuu? Na mengi nyuma ya pazia kama yapi? Visasi au mtoto ni Biological homo?
 
Kuyaacha kama yalivyo kiaje mkuu? Na mengi nyuma ya pazia kama yapi? Visasi au mtoto ni Biological homo?
Mbna yako zaidi ya hayo. muhimu kila mtu apate haki stahiki kulingana na case husika.
 
Ukiwa mwalimu usipende ukaribu wala mazoea na wanafunzi kabisa.

Pia usipende ukaribu wala mazoea na watoto wa majirani zako.

Anaweza akawa anafokolewa na watoto wenzake halafu akaja kukuangushia jumba bovu wewe
 
Mtoto wa miaka 11 kufanyiwa ukatili wa kiasi hicho na isigundulike mapema kuna tatizo kati yake na wazazi/ walezi.
 
Back
Top Bottom