Shaibu ametoa Wito kwa Waziri wa TAMISEMI kumuwajibisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya

Shaibu ametoa Wito kwa Waziri wa TAMISEMI kumuwajibisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
ACT WAZALENDO YACHARUKA HUJUMA UJENZI WA KITUO CHA AFYA KYANG'OMBE, RORYA
IMG-20240727-WA0006.jpg

Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ndugu Ado Shaibu ametoa Wito kwa Waziri wa TAMISEMI kumuwajibisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa kuruhusu Mradi wa Kituo cha Afya Kata ya Kyang'ombe kujengwa chini ya kiwango.

Ado alitoa kauli hiyo alipokagua ujenzi wa Kituo hicho cha afya kinachojengwa kwa nguvu za wananchi na michango ya wahisani.

"Ndugu Mchengerwa tupia jicho lako hapa Kata ya Kyang'ombe Wilaya ya Rorya. Diwani amenijulisha kuwa wananchi wamechangishana fedha na shirika la NMB limechangia fedha Mil. 15 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya. Nimesikitishwa kuelezwa kuwa Wataalamu wa Halmashauri wameutelekeza mradi huu na Mkandarasi anajenga chini ya kiwango bila mwongozo wa Injinia wa Halmashauri ambaye amekataa kuja kwenye mradi. Nimekuta mbao za kuezekea kituo hicho cha afya zikiwa duni na mkandarasi anafanya anavyotaka mwenyewe. Hii ni dalili ya rushwa na Wizara inapaswa kuchukua hatua"-alisema Ndugu Ado
 
Figisu na visasi vya makusudi na ushamba wa CCM hivyo..Hawako tayari kuleta maendeleo kwa Wana Rorya kisa ni wanazi wa mabaliko kupitia CHADEMA baada ya kuvurugwa na AIRO LAMECK wa CCM kwa miaka mingi:Walimpa kura nyingi mno za Ubunge- Ezekiel Wenje wa CHADEMA-2020 na aliwasumbua sana kwenye kampeni licha ya Magufuli kuwatisha hataleta maendeleo watakapo chagua upinzani nayo haikusaidia.....Magufuli akatoa amri sasa asitangazwe mshindi na apelekwe kusikojulikana haraka sana.Wenje naye akakimbilia CANADA haraka sana kuokoa usalama wake.
 
Figisu na visasi vya makusudi na ushamba wa CCM hivyo..Hawako tayari kuleta maendeleo kwa Wana Rorya kisa ni wanazi wa mabaliko kupitia CHADEMA baada ya kuvurugwa na AIRO LAMECK wa CCM kwa miaka mingi:Walimpa kura nyingi mno za Ubunge- Ezekiel Wenje wa CHADEMA-2020 na aliwasumbua sana kwenye kampeni licha ya Magufuli kuwatisha hataleta maendeleo watakapo chagua upinzani nayo haikusaidia.....Magufuli akatoa amri sasa asitangazwe mshindi na apelekwe kusikojulikana haraka sana.Wenje naye akakimbilia CANADA haraka sana kuokoa usalama wake.
Tatizo la Rorya naliona zaidi kwa jicho la ujuaji wa kijinga. Kuna wahuni wachache kisa wana fedha haramu wanataka wanaRorya waache akili ndogo zitawale akili kubwa!
Na ccm ilivyo ya ajabu kwa makusudi kabisa inawakumbatia hao hao wajinga wachache!
Mwisho wa siku ni kukoleza mgogoro kati ya Utegi na Shirati!
WanaRorya wasipokuwa makini wilaya yao itazidiwa kasi ya maendeleo na Wilaya changa za hivi karibuni.
 
Back
Top Bottom