Shairi: Damu ya Albino

Shairi: Damu ya Albino

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,497
Reaction score
4,775
Kwa pamoja tuungane na kuwatetea ndugu zetu hawa wenye ulemavu wa ngozi.
1>damu yake yamwagika,bila hata ya hatia.
Na vilio vya sikika.,maumivu wasikia.
Yamewajaa mashaka,kipi walichokosea ?
Damu ya maalibino,nani ataja ilipa ?
2>damu itatulaani,kosa tukiendeleza.
Wauaji ni motoni,wao waamini giza.
Watajutia rohoni,na aliewapoteza.
Damu ya maalibino,nani ataja ilipa ?
3>damu yao itasema,kwanini tuliuliwa.
Siku ile ya kiyama,hukumu kuhukumiwa.
Hakuna ataesema,motoni kuchuliwa.
Damu ya maalibino,nani ataja ilipa ?
4>damu yao siyo maji,ipotee hivi hivi.
Damu yao si mtaji, ichezewe kama hivi.
Hakika kila muwaji,si mtu nyakati hizi.
Damu ya maalibino,nani ataja ilipa ?
5>maswali tujiuze,hadi jibu tulipate.
Tuache kupiga zeze,makubwa yasitupate.
Na tena tuwakimbize,wauaji tuwapate.
Damu ya maalibino,nani ataja ilipa ?
Shairi:damu ya albino.
Mtunzi:Idd Ninga

Maoni=iddyallyninga@Gmail.com

"DAIMA TUTAWAKUMBUKA MILELE,KAMA WATANZANIA HAWATOWATAZAMA,BASI MUNGU ATAWASHIKA MKONO,MSIOGOPE HAKUNA HAKI ITAKAYOPOTEA,ISIPOLIPWA DUNIA,ITAJALIPWA MBINGUNI"
 
Back
Top Bottom