Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 893
- 1,021
Kula ilonona
Niliyowaza ni mengi, hadi kuandika hili
Ni usia wa mvungi, aliompa Sadali
Wa kilemba au shungi, kila mtu yake hali
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Usifanye kwa kuiga, kuona ndio ufanye
Zitumie zako kuga, mwenyewe na ujikanye
Uoga si wa kufuga, kaa chini jikusanye
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Hatufanani hakika, kwa sura au fikira
Pambana na heka heka, ukomeshe ufukara
Jiondolee mashaka, nenda pasi na papara
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Amua kwa mara moja, pigana na utashinda
Hii vita si ya mmoja, kataa kupindapinda
Usiwe mtu viroja, pambano litakushinda
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Usisikize ya watu, wengi wamejawa husda
Funga kamba za viatu, tembeza hata visoda
Shida zako si za watu, acha wakupake poda
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Abuuabdillah [emoji3578]
0744883353
Jumaomari5@gmail.com jumaomari@ymail.com
Niliyowaza ni mengi, hadi kuandika hili
Ni usia wa mvungi, aliompa Sadali
Wa kilemba au shungi, kila mtu yake hali
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Usifanye kwa kuiga, kuona ndio ufanye
Zitumie zako kuga, mwenyewe na ujikanye
Uoga si wa kufuga, kaa chini jikusanye
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Hatufanani hakika, kwa sura au fikira
Pambana na heka heka, ukomeshe ufukara
Jiondolee mashaka, nenda pasi na papara
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Amua kwa mara moja, pigana na utashinda
Hii vita si ya mmoja, kataa kupindapinda
Usiwe mtu viroja, pambano litakushinda
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Usisikize ya watu, wengi wamejawa husda
Funga kamba za viatu, tembeza hata visoda
Shida zako si za watu, acha wakupake poda
Kama wataka haramu, basi kula ilonona
Abuuabdillah [emoji3578]
0744883353
Jumaomari5@gmail.com jumaomari@ymail.com