Shairi: Nyege ni kunyegezana by Andanenga

Yes Poetic licence BASATA ndio wanatoa!
hapana!
BASATA hawatoi poetic licence!
hata kwanza nawashangaa wanavodhalilisha taaluma yao!
Poetic devices ni uhuru wa msanii kutumia lugha/ sanaa bila kufungwa na kanuni na misingi ya lugha husika!
 

Kiranga sende mrama, kaditama sio kiama ,
Kienda si mwanae kwenda, kienda rudi tuanze sema ,
Nani matusi kasema, nayasaka nitoe lana ,
Raha ya nyege nyegeni, shairi lake uhuru .

Utusi u kamusini, kwani yalowekwa na nani ?
Ninayo I kamusini , hilo katazo la nini ?
Si wanayo shubakani, hawalioni kwa nini ?
Raha ya nyege nyegeni, shairi lake uhuru .

Tulikwenda na shuleni, tukakariri vichwani ,
Mwanagenzi yu huruni, kukunja viriga tungoni ,
Haya kwetu ni mageni, sizo kunga shairini ,
Raha ya nyege nyegeni, shairi lake uhuru .

Andanenga na Mloka, sifazo kwao hakika ,
Walitunga yakatundika, na Shabani msifika ,
Wote nao na Soyinka, walijua kuandika ,
Raha ya nyege nyegeni , sheria zilianza lini ????
 
hapana!
BASATA hawatoi poetic licence!
hata kwanza nawashangaa wanavodhalilisha taaluma yao!
Poetic devices ni uhuru wa msanii kutumia lugha/ sanaa bila kufungwa na kanuni na misingi ya lugha husika!
Ha ha ha joking! Poetic licence is like I say the bus growled uphill instead of simply bus went uphill.The player who scored was completely unmarked he was free as a molecule.
 

Vitabu viliandika, vuguvugu hatakiwi
Hata peponi kufika, tiketiye hapatiwi
Vipi kufumba hakika, cheusi cheupe Kiwi
Tungo vina na mizani, vingine wenda kizani

Tungo vina na mizani, vingine wenda kizani
Utatupiga tufani, kutufunga gerezani
Tuachia tafrani, tukosekane nyumbani
Ya kivinje hutaghani, kutupaya Mikindani

Chaguzi ni kuchagua, kwa hakika kwa agua
Sifanye kujibutua, kwa tungo zenye kujua
Vipi kwenda kwa kujivua, sanaa kuiumbua?
Kwafagio kubagua, kwa majilisi vumbua

Nyege ni kunyegezana, si tungo ya lelemama
Upitie karakana, si vungo la maulana
Vipi tungo kwama kwama, kwa rula hazilalana?
Tungo za malenga wana, hazikeshi za mchana

Tungo huru nazijua, kiziona natambua
Zenda zarudi bamvua, kwa urefu ka mashua
Haiku nazo chagua, sheria zake pasua
Vipi waruka kagua, upande unapotua?

Kaditama nachutama, kata niletee maji
Shairi mithili kama, la malenga wajuaji
Silete rai za chama, za kwenda kama Bajaji
Tungo tunga za maana, wakusikize wazazi
 
Jambo baya kbs ni kwamba taasis ya kiswahili Tanzania inajisahau sana, yaan inaacha maneno mengi sana ya kiswahili yatumike kiutusi utusi tu, kuliko yanavyopaswa kutumia kwenye jamii.

Mfano neno kutia..
Kutembea
Mtarimbo
Uroda
 
Mkuu Nyani Ngabu mgambo wako wa BASATA wameshafanya kazi yao kwa diamond na wasafi festival yake.
 
Uhuru kenyata nae kaamua kusisitiza ya kuwa nyege ni kunyegezana.
 
Naliweka hapa hilo Shairi:

Peni yangu Andanenga, uwino unapotona,
Mantiki huzilenga, na balagha na bayana
,Hufaidika malenga, huvurugika akina
,Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili

.Msemo wa Kiswahili, nyege ni kunyegezana
,Maana yaki kamili, wema ni kutendeana,
Wasiojua fasili, hunamba nimetukana
,Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.


Ni msemo maarufu, ambao shaka hauna
,Kwenye kamusi sanifu, funueni mtaona
,Niwezeje kukashifu, nami mwana muungwana!
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.


Ninataja ukurasa, wazi hapa naunena,
Soma mbili moja tisa, soma bila ya fitina,
Msemo siyo wa sasa, si juzi licha wa jana,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.


Ushairi kubwa fani, mithili yake haina,
Kujua zake bayani, yataka kikubwa kina
Muoneni mwafulani, hata kuku wamguna,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili

.Ulipotamkwa mlo, kaja akitunatuna,
Akakabwa koromelo, akabaki kugunaguna,
Kabakia lolololo, uzamani umechina
,Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili

.Alhaji Jitukali, pokea pongezi tena
,Kikubwa chako kilili, hapandi yule mtwana,
Atuache tule wali, yeye ugali wa dona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili.

Kaditama wa Busara, na Mbwezi heko kijana
,Pongezi ndugu Kagera, Yobu has ante sana,
Ndimi Mshairi Bora, kipofu ninaeona,
Nyege ni kunyegezana, msemo wa Kiswahili

.(Mshairi Bora)Amiri A. S. Andanenga (Sauti ya Kiza)SLP 4775,Kinondoni ShambaDar es salaam.

KWA MUJIBU WA KAMUSI YA KISWAHILI SANIFU.

Ukisoma Kamusi ya Kiswahili sanifu ( TUKI) ya mwaka 2012 ukurasa wa 315 Msemo Nyege ni kunyegezana maana yake Wema ni mpaka uwe wa kutendeana
 
Domo akifunguliwa tutajua ni kipenzi cha mzee km ilivyo Bashite
 
kashakuambia Andanenga yeye hatukani kamwe "NYEGE KUNYEGEZANA" maana yake "WEMA KUTENDEANA".



Mkuu, kwa yeyote aliyetunga hilo shairi na jinsi maneno hayo yalivyotumika, hapo bila shaka KATUKANA tu na hana utetezi wowote juu ya hilo, kwani hakuyaona hayo maneno mbadala "WEMA KUTENDEANA" hadi aandike ""NYEGE NYEGEZI"'??!!

Wewe unaweza kusoma shairi hilo mbele za wanao au wazazi wako??!!πŸ€”πŸ€”πŸ€”
 




Na hata, kutongoza ni kutongozana--- 😁😁😁

Je, leo Kauli hiyo inatumika "hasa" mahali gani??--- Lugha inapotumiwa ndipo inapokuwa pamoja na wakati (grow with time).

"Nyege kunyegezana" ni TUSI kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…