uzio usio onekana
JF-Expert Member
- Apr 21, 2019
- 836
- 2,658
Hezbollah imesema mmoja wa makamanda wake wakuu aliuawa katika shambulio la anga la Israel kusini mwa Lebanon, huku kundi hilo la waasi linaloungwa mkono na Iran likilipiza kisasi kwa msururu wa makombora dhidi ya Israel.
Mohammed Nimah Nasser ndiye mjumbe mkuu wa hivi punde zaidi wa Hezbollah kulengwa na Israel katika kipindi cha takriban miezi tisa ya ghasia za kuvuka mpaka ambazo zimezua hofu ya vita vya pande zote.
Hezbollah ilisema kuwa imerusha roketi na makombora 100 katika vituo vya kijeshi vya Israel "kama sehemu ya kukabiliana na mauaji". Jeshi la Israel lilisema kuwa makombora kadhaa yaliyoanguka katika maeneo ya wazi yalizua moto, lakini hakuna majeruhi yoyote yaliyoripotiwa.
Jeshi lilisema Nasser aliamuru Kitengo cha Aziz cha Hezbollah, ambacho kinahusika na kurusha roketi kutoka kusini-magharibi mwa Lebanon, na kumshutumu kwa kuongoza "idadi kubwa ya mashambulizi ya kigaidi".
Pia ilimtaja"mwenzake" Taleb Sami Abdullah, kamanda wa kitengo kingine ambaye mauaji yake yalifanyika mwezi uliopita yaliifanya Hezbollah kurusha Zaidi ya roketi 200 na makombora kaskazini mwa Israel kwa siku moja.
Tangu wakati huo, kumekuwa na msururu wa juhudi za kidiplomasia za kupunguza mvutano, huku Umoja wa Mataifa na Marekani zikionya kuhusu matokeo yanayoweza kuwa mabaya ya vita ambavyo vinaweza pia kuvuta Iran na makundi mengine washirika.
Kumekuwa na kurushiana risasi karibu kila siku katika mpaka wa Israel na Lebanon tangu siku moja baada ya kuanza kwa vita kati ya Israel na Hamas huko Gaza tarehe 7 Oktoba.
Hezbollah imesema inafanya kazi katika kuunga mkono kundi la Palestina ambalo pia linaungwa mkono na Iran. Vikundi vyote viwili vimetangazwa kuwa mashirika ya kigaidi na Israel, Uingereza na nchi zingine.
Mohammed Nimah Nasser ndiye mjumbe mkuu wa hivi punde zaidi wa Hezbollah kulengwa na Israel katika kipindi cha takriban miezi tisa ya ghasia za kuvuka mpaka ambazo zimezua hofu ya vita vya pande zote.
Hezbollah ilisema kuwa imerusha roketi na makombora 100 katika vituo vya kijeshi vya Israel "kama sehemu ya kukabiliana na mauaji". Jeshi la Israel lilisema kuwa makombora kadhaa yaliyoanguka katika maeneo ya wazi yalizua moto, lakini hakuna majeruhi yoyote yaliyoripotiwa.
Jeshi lilisema Nasser aliamuru Kitengo cha Aziz cha Hezbollah, ambacho kinahusika na kurusha roketi kutoka kusini-magharibi mwa Lebanon, na kumshutumu kwa kuongoza "idadi kubwa ya mashambulizi ya kigaidi".
Pia ilimtaja"mwenzake" Taleb Sami Abdullah, kamanda wa kitengo kingine ambaye mauaji yake yalifanyika mwezi uliopita yaliifanya Hezbollah kurusha Zaidi ya roketi 200 na makombora kaskazini mwa Israel kwa siku moja.
Tangu wakati huo, kumekuwa na msururu wa juhudi za kidiplomasia za kupunguza mvutano, huku Umoja wa Mataifa na Marekani zikionya kuhusu matokeo yanayoweza kuwa mabaya ya vita ambavyo vinaweza pia kuvuta Iran na makundi mengine washirika.
Kumekuwa na kurushiana risasi karibu kila siku katika mpaka wa Israel na Lebanon tangu siku moja baada ya kuanza kwa vita kati ya Israel na Hamas huko Gaza tarehe 7 Oktoba.
Hezbollah imesema inafanya kazi katika kuunga mkono kundi la Palestina ambalo pia linaungwa mkono na Iran. Vikundi vyote viwili vimetangazwa kuwa mashirika ya kigaidi na Israel, Uingereza na nchi zingine.