Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Haya sasa kazi ya kuwatambua wasiojulikana kupitia kwa karma inaanza taratibu, Marekani imeanza kuwasaidia!, tunaianza safari mdogo mdogo mwisho wa siku, wasiojulikana watajulikana tuu!.
P

Naona uliyaona haya 2017 na hayakufanyiwa kazi anyway kule kwenu ziwani au kwenye mto Simiyu ukitaka kuvua samaki wadogo unaenda kuchimba minyoo midogo na kuiweka kwenye ndoano na ukitaka kukamata samaki wakubwa kama Sangara basi unatumia samaki mdogo kama chambo yako
 
KARMA
2108469_IMG_20190708_112420_395.jpg
2108471_IMG_20190708_112437_219.jpg
 
Narration yako makes a big sense! BUT look: Mr, Pascal, usizidi kunipa mashaka! Mauaji, upoteaji, uteswaji, kesi za 'kipuuzi" wanazokutana nazo watu... Rais fulani hajawahi kuzikemea. Yoooooooooooooooooooooooooooooooooote yaliyotokea kwa Lisu sanasana alichojibu ni kuwa yule jamaa amelitelekeza jimbo! Wadau woooooooooooooooooooooote walisema ruhusu uchunguzi huru toka nje watampata aliyempiga risasi Lisu.. he never commented anything! Watu wamekutuhumu, kujibu tuhuma unafanyaje? Unasema Njoo mchunguze then ukweli utapatikana.
Pascal nambie yaliyotokea kwa Lisu kama angalikuwa hana mkono wake asingeruhusu kuona watu wanapoteza CCTV, wanaondoa walinzi, angelisema nataka kujua leo leo nani aliwaondoa walinzi! He never did that..... Maswali ni mengi yanayomwelemea.. irresisitible inference kuwa anahusika...
Ngoja niachie hapa......
Hili ni vizuri kuachia hapa kwasababu whoever who was behind shooting ya Tundu Lissu ni shetani kabisa, the devil in human flesh, mimi siamini tunaye shetani wa aina hii, ila kwa vile sio kila kinachofanywa na serikali lazima kiripotiwe kwenye media hivyo mimi ninaamini 100% chini ya 100% serikali imechunguza, zile CCTV ni nyumba ya Kalemani ila sio CCTV za serikali, naamini hadi Mzee atakuwa ameulizia, na uchunguzi umekwama kutokana na kukosekana mashahidi wawili wakuu ambao ni muhimu sana. Endapo kugetokea fatality kazi ingekuwa well done, by now file lingeisha fungwa, lakini kwasababu mashahidi wapo, wanasubiriwa wahojiwe ndipo uchunguzi uendelee.
P
 
Do not try to downplay UNYAMA aliofanyiwa. Kuna watu wamekufa kwa kupigwa risasi moja, sembuse 16 alizopigwa TL?
Mkuu Joka Kuu, kwanza ni kweli Tundu Lissu amefanyiwa tukio la kinyama, na hakuna binaadam yoyote mwenye utu na ubiadamu anaweza kufurahia tukio lile, tena naamini by now hata waliopanga na kutekeleza wanajuta, hivyo hakuna yoyote anaye try to Downplay, bali kwa vile mpaka sasa waliopanga na kutekeleza tukio lile ni watu wasiojulikana, zinatengenezwa postulates nyingi ili kuzitungia theory na kuzitafutia proof, sasa kwa vile moja ya theory hizo, waliofanya tukio hilo ni ma pro, hiyu jamaa yeye ni pro, anasema tukio hilo sio kazi ya ma amateurs ndio maana imelipuliwa, na wewe unasema they could be pro, you both might be right or wrong, kitu muhimu ni nawashukuru kwa hoja zenu na haswa uwezo wa ujengaji hoja na kuitetea hoja yako.

Mimi kwa upande wangu, wasiojulikana hawa niliisha wabaini siku nyingi na kuwaelezea humu
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums
Hapa kwenye bandiko hili ni just the role of dereva wa Lissu, was he part and parcel or not, jibu litapatikana soon Lissu ameomba kurejea, tumsubirie
P
 
Mayalla pole na hongera sana, umewezaje kuwa reqular contributor hapa Jamii Forum kwa kiwango hichi katika jumuia ambayo au hawana ufahamu wa kuchangia au maadili ya kuchangia yako chini sana au ufahamu wa somo na tukio uko chini mnoo.

Pole sana, unabishana na wengi wasio jua na wenye kujua wanakalia ushabiki ambao unadhalilisha Jamii Forum,Hasa kwa wenye kujua Machine guns zinafanyaje kazi kuna ulazima na sio kubeza. Mayalla una ngozi ngumu , Asante.
Mkuu Gerald Magembe, asante kwa hii. Sisi watu wa fani ya uandishi wa habari, tunaangukia katika kundi la waelimishaji umma, hivyo tunapokutana na wabishi wa humu, tunawatumia kana fursa kwa kuutumia ubishi wao kuelimishia umma.
Kwenye hili la ngozi, ni kweli nina ngozi ngumu.
Asante.
P
 
Pascal mimi natamani yafuatayo; kwakuwa sina uwezo na madaraka natamani lile jopo lililokaa na kuona suluhisho la kumdhibiti Tundu Antiphas Mughwai Lissu ni kumtwanga Risasi COVID-19 iwapitie, wale waliotafuta upenyo wa kibabe wa kukwepa kumlipia Lissu gharama za matibabu na akati anastahili hadi mimi na umasikini wangu nikakopa na kutuma Tsh1,000,000/= kama mchango wa dhati ya moyo wangu ili Lissu apatiwe matibabu ya kuokoa uhai wake nasema COVID-19 ikiwa na jina la Yesu ndani yeke pamoja na moto wa maserafi na makerubi ikawapige hao wauaji kama upepo wa kisulisuli.

Wale waliohusika kuua na kufunga miili ya watz kwenye sandarusi na kwenda kuitupa mto Ruvu na wengine kwenye fukwe za bahari nasema COVID-19 popote ulipo kawapitie hawa wasaidizi wa Lucifer watangulie kabisa kule kwenye ziwa la moto.
Haiwezekani ktk nchi hii kuwe na watu wenye mamlaka ya kutoa uhai wa watu halafu tusio na uwezo wa kuwafanya chochote tushindwe hata kumuomba Mungu au shetani kuwasulubisha.

Pamoja na kwamba kisulisuli kilishindwa kuwabeba wanaume wa kuwaoa wale mabinti wa kanisa la mlima wa moto pendine ni kwa sababu ya uzito wao lakini bado nakiamini kisulisuli hakiwezi kushindwa kuwabeba COVID-19 na kwenda kuwafanyia INOCULATION hao niliowataja hapo juu.
Haiwezekani watu watekeleze mauaji ya watz wenzetu halafu bado tuendelee kuwasifia kisa teuzi, wapitie huu uzi hapa ili wajue kuwa hatuwapendi kwa matendo yao.

Kuna hawa wadudu wengine wanaitwa wasiojulikana ikitokea COVID-19 ikawasafisha pamoja na vizazi vyao Pascal huoni kama hii itakuwa ni baraka kutoka kwa Mnyazi Mungu kwa kutupunguzia watu wenye roho mbaya za Black Mamba a.k.a Koboko (Dendroaspis polylepis) au Anaconda a.k.a Water boa or Bull killer kama wataalam wanavyomfaham kwa jina la Eunectes murinus.

Nikipata bahati ya kuipata AK47 ikiwa loaded halafu nikaonyeshwa kwamba huyu ndiye aliyemfyatulia risasi Lissu Pascal otea nini kitatokea? Kama niliyoyasema hapo juu ni uongo na kwamba hao hawahusiki na madhila husika basi namkaribisha ZRAIL nyumbani aje anisalimie na si vinginevyo.
Mkuu Konyola, nimekuleta huku kwasababu umewaombea Corona hawa wasiojulikana.
Kwa vile ni watu wasiojulikana, hata wakisombwa na Corona, hakuna atakayejua, ila tusiwaombee watu wafe kwa Corona kwa kuwahisi tuu bila ushahidi, karma inaweza kukugeuzia kibao.

Mfano ni kweli Tundu Lissu ameshambuliwa na watu wasiojulikana, kisha Mkuu Konyola akaombea shetani Corona awakusanye na kuwapeleka moja moja kwa mkuu wao Lucifer kule kwenye makao yao ya milele ya jahanum ya ziwa la moto wa milele, hii ni sawa ni ombi halali kwasababu Tundu Lissu ameshambuliwa kweli na waliopanga na waliotekeleza ushetani ule ni mashetani kabisa hivyo kuwaombea vifo ni halali kabisa na hili na mimi naliunga mkono.

Lakini ikitokea wewe Mkuu Konyola, kwavile mimi Paskali nimetofautiana na Tundu Lissu mahali, hivyo Tundu Lissu aliposhambuliwa, wewe Konyola bila ushahidi wowote ukahisi nitakuwa ni mimi kwasababu tulitofautiana na Tundu Lissu mahali, hivyo sasa unaniombea mimi Paskali ndio nife kwa Corona, ikitokea ni kweli mimi nilihusika, then naombi yako yatajibiwa na Corona itakula kichwa!, Lakini ikitokea sio mimi wala sihusiki na shambulio la Lissu, kitendo cha wewe Mkuu Konyola kuniombea nife kwa Corona, itakuwa ni ushetani, na kupitia kanuni ya karma, ombi lako hilo linaweza kujibiwa kwa kanuni ya 3 ya Newton's Laws of motion ile ya every motion there is equal and opposite reaction, hivyo ombi hilo likakugeikia.

Mungu kupitia kwa Bwana wetu Yesu Kristo alitufunza tusihukumu, tusije kuhukumiwa, hivyo wasiojulikana waliomshambulia Lissu, maadam hawajulikani na Mungu anajua kila kitu, mwachie Mungu.

P
 
View attachment 1472626
View attachment 1472650

Salaam,

Taarifa nilizozipata hivi punde toka chanzo changu kinanihabarisha kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman A. Mbowe amevamiwa na kikundi cha watu wasiojulikana akielekea nyumbani kwake usiku huu na kupigwa na wamemuumiza.

Tukio hili limetokea majira ya saa 6-7 usiku.

Mhe. Mbowe amekimbizwa Hospitali ya Ntyuka iliyopo jijini Dodoma.

Kamanda Muroto amesema wamepata taarifa kuwa kavunjwa mguu wa kulia na amelazwa Wodi namba 4 hospitalini hapo. Amesema taarifa zaidi zitafuata

MAONI YANGU:
Mhe. Mbowe kuvamiwa na kupigwa eneo la Area D, jijini Dodoma, Mtaa wa Sengia; linalotajwa kuwa na ulinzi wa kutosha, kama ilivyotokea kwa Lissu kunaacha maswali mengi, je, hili linaweza kuwa limechochewa na Lissu kutangaza nia ya kugombea Urais wa JMT October 2020? Ni hasira au kitu gani? No one knows.

Bado najiuliza; hivi kama Taifa kwa tabia hizi za kihuni tunaelekea wapi? Hawa wanaojichukulia sheria mikononi kila siku wanafanya hivyo kwa kutumwa na nani? Matendo haya yataendelea kwa viongozi wa upinzani mpaka lini?

We need to wake up, better late than never.
Duh...!.
Hii ni hatari sana!.
Hata shambulio hili la Mhe. Mbowe, limefanywa na watu wasiojulikana.
Pole sana Mhe. Mbowe,
Get well soon.
P
 
Wanabodi,
  1. Kama wahusika wa Tukio la shambulio la Mhe. Tundu Lissu, ni wale 'jamaa zetu', kwa vile wale ni ma pro, they have one million ways to do things, in a good clean job in a professional way na not leave and traces behind, and they have never missed a target!, sasa kama kweli ni wao, ndio waliomshambulia Lissu, how could they do such a bad dirty messy job?!, how could they missed a target in such close range?, hadi watumie risasi 38!, wakati kwa trained snipers, only one is enough?!.
  2. Tuambiane ukweli jamani, hawa waliofanya haya watakuwa sio wale 'jamaa zetu!' na kama ni kweli walikuwa wale, saa hizi si tungekuwa tunazungumza mengine?!.
  3. Unless kama ni kweli ni wao, ila wamejifanya to miss the target makusudically ili ku dupe the public kwa kupotezea maboya ili kupoteza lengo ionekane waliofanya tukio lile sio ma pro ili tukio lionekane limefanywa na amateurs!.
  4. Kama 'jamaa zetu' have 100 ways to do elimination in a good clean professional way by doing it right in a clean job, on natural death look aike, kama natural accidents, or any clean job that nobody would've suspected anything, why did they do such a mess, such a bad dirty job?!.
  5. Hawa "jamaa zetu" hufanya elimination kwenye some serious security threats to our national security, or threats to the status quo of the ruling elites waliopo, swali la kujiuliza ni kwa the ruling class ya sasa when was Mhe.Tundu Lissu, has ever been such a threat to warrant such elimination?!. Kama kuna defectors very high rankings wame cross na wamejizolea kura nyingi kuliko zilizomuingiza rais Kikwete madarakani ile 2010, hawa ndio the real threats!, hivyo kama issue ingekuwa ni eliminations for status quo threats, kwa nini hawa ambao ndio the real threats wasiwe targeted aje kuwa targeted Lissu?, Why Lissu?!.
Paskali
Wanabodi, hiki nilichokisema hapa, sasa kimesemwa rasmi hapa
Uchaguzi 2020 - Samia Suluhu Hassan: Askari wa serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Hivyo shambulio hili ni an inside job iliofanywa na amateurs!.
P
 
Wanabodi, hiki nilichokisema hapa, sasa kimesemwa rasmi hapa
Uchaguzi 2020 - Samia Suluhu Hassan: Askari wa serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Hivyo shambulio hili ni an inside job iliofanywa na amateurs!.
P

Pascal,
Listen this good and clear.
Naskitika sana kwa Mama Samia Suluhu kwa kujiingiza kwene sakata hili tena wakti huu wa Kampeni za Urais na mbaya zaidi victim wa SHAMBULIO hili ni mgombea wa Urais...!!!
Briefly Mgombea mwenza wa CCM upande wa Urais amefanya a very grave mistake. Kwamba ameanza kujibu mapigo ya hoja za kushambuliwa kwa Lissu wakti huu wa Kampeni! Kiukweli Lissu ataiumbua CCM, Magufuli na Samia mapema mno.
Tayari Lissu anahoji kwa Samia kuwa kumbe ni kweli WASIOJULIKANA (ASKARI)wanatumia RISASI 3 TU KUUA basi ndio WAHUSIKA...!!!

Hawa unaowaita mapro they're human beings, they can miss the target as well! Ndiyo kilichotokea kwa SHAMBULIO la Tundu Lissu. Lakini pia lazima ujue kuwa kuna silaha Kama SMG,LMG na AK-47 ambazo hupiga risasi kwa mtindo wa "BURST" au mlipuko(kutoka risasi nyingi kwa mara moja).
Ndiyo maana risasi zilixompiga Mhe. Lissu zilikuwa takribani 38!

Mwisho nataka mjue wewe,Samia, Magufuli na CCM kuwa katika JARIBIO la KUUA Kuna Mungu pia anayeweza KURUHUSU au KUZUIA.
Leo Lissu Yuko hai kwa UWEZO WA MWENYE ENZI MUNGU. Nakumbuka kauli ya Madaktari wa Nairobi walomtibu Lissu wakti wakimhudumia walisema WALIKUWA WAKITIBU MUUJIZA WA LISSU. Kwa kawaida mtu akishapoteza DAMU kiasi Cha 80% ni KIFO! Leo Mhe. Tundu Antipas LISSU yuko "LIVE" a.k.a MUBASHARA akikabiliana uso kwa na maadui zake!
Huu ni MUUJIZA kwa Lissu, Tanzania na Dunia nzima.
Yawezekana muujiza huu was kuokoka Lissu ni mpango mahsusi kwa Watanzania.
Stay tuned come 28 October, 2020.
 
Wanabodi,

Kumbe sometimes sii kweli kuwa wahusika wa kila tukio ni watu wasiojulikana, sometimes wahusika wa matukio hayo sio watu wasiojulikana bali ni watu 'wasiojulikana'!.

Hivyo hili ni bandiko fikirishi tuu la dhana dhanifu ya kuwahusu watu wasiojulikana vs 'wasiojulikana' ambao mwisho wa siku baada ya uchunguzi wa kipolisi, wasiojulikana watakuja kujulikana, na 'wasiojulikana' kamwe hawatakuja kujulikana kwa njia za kawaida ila kitu kinacho itwa karma kitakuja kuwajulikanisha mmoja baada ya mwingine, tatizo ni wakati karma ikiwajulikanisha, hakuna watu wa ku connect the dots kuwa hiyo ni karma ya tukio gani.

Hivyo kuna mashambulio yanayofanywa na watu 'wasiojulikana', ambao hawa, kamwe hawakuja kujulikana!, haswa pale ambapo 'wasiojulikana' hawa ni wale 'jamaa zetu'!, ila karma itawashughulikia.

Paskali
HAPANA, sijahukumu mtu miye. Nimesema kwa kadiri ya maandiko matakatifu (Neno la Mungu - Biblia) isemavyo..

Hebu soma hapa;

WARUMI 12:19
"...wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imendikwa 'kisasi ni juu yangu Mimi; mimi nitalipa', anena BWANA..."

Unaweza pia kusoma Kumbukumbu la Sheria 32:35; Walawi 19:18; Mathayo5:39 nk nk

Kwa hiyo ndugu yangu Paschal Mayalla, tusifikiri kuwa tunapowatendea watu wengine mabaya kwa sababu na kisingizio chochote hata kama mtu huyo ni mnyonge au dhaifu kisasi gani tukadhani sisi tunaotenda unyama huo tutakuwa salama...

å Waliokosea sana waliompiga marisasi yote yale Tundu Lussu kwa sababu iwayo yoyote...

å Wanakosea sana watawala wanaotumia nguvu na madaraka yao vibaya kunyanyasa wapinzani wao, wanaowakosoa kwa haki hata isivyo haki, wanaokataa kukubaliana na mawazo au Sera zao...

Watambue kuwa, anayewatetea hawa wote ni Bwana Mungu Muumba wa mbingu na nchi. Mungu anasema hivi: YEYE MWENYEWE NDIYE ALIPAYE KISASI...

Lipo lango la kukimbilia na kuepuka kisasi cha Mungu. Ni TOBA. Ni kukimbilia Golgotha msalabani pa mwokozi Yesu Kristo tukiwa na mafurushi yote ya dhambi zetu na kuzitupa hapo...


Kaka, mimi sijahukumu mtu. Nimesema kwa kuzingatia muktadha wa maandiko matakatifu - Biblia inavyosema...
Waliomshambulia Lissu ni watu wasiojulikana.
P
 
Back
Top Bottom