Shambulizi la jeshi la Nigeria lawaua watoto 7 Niger

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Watoto saba wamekufa na wengine watano kujeruhiwa katika shambulizi la angani nchini Niger hii ikiwa ni kulingana na gavana wa jimbo moja nchini humo

Shambulizi hilo lililofanywa na vikosi vya Nigeria katika eneo la mpakani lilikuwa likiwalenga majambazi lakini badala yake liliwaua na kuwajeruhi watoto hao siku ya Ijumaa

Kulingana na Gavana Chaibou Aboubacar wa mkoa wa Maradi jeshi la Nigeria lilikuwa likiwalenga majambazi hao, lakini kwa bahati mbaya liliwakuta watoto hao waliokuwa katika kijiji la Nachade.

DW Swahili
 
Kuna nchi zinapata shida hasa watoto kutokana na ugaidi.

Nakumbuka wanafunzi waliotekwa miaka ile ya Obama shule yote they took all girls, nililia.

Hii kitu bado inaendelea.

Natamani amani yetu isivurugwe wamama na watoto tutateseka.
 
Yaaani majambazi yanalipuliwa na ndege Vita!? Sasa hayo majambazi au magaidi !?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…