Share Nasi Hapa Cheat Code Ya Mazoezi Yoyote

Share Nasi Hapa Cheat Code Ya Mazoezi Yoyote

Bei inategemea na aina mfano whey protein hua naona zinaanzia 60k, 80k, 120k, na kuendelea.

Na kwa k/koo kuna duka lilikua pale Shimoni
Asante mkuu. Nitalitembelea kucheki

Sent from my Iphone 7 using JamiiForums mobile app
 
Ukimaliza mazoezi yako bila kuoga, kunywa maji, juisi au uji wenye maziwa au peanut butter kisha lala kwa saa moja.

Ukiamka oga na endelea na ishu zako.
 
Kama unataka kua na mwili mkakamavu usio mkubwa sana ila wenye mikato.
Flexibility na speed katika ishu zako fanya plyometrics.

Online tutorial na mazingira ya kibongo hayaendani lakini nilimodify kwa kadri nilivyoweza.
 
Ukifanya mazoezi baada ya muda utafikia plateau/ kilele. Hapo ndiyo utakuta ukikimbia hakukupi ile spark ya mwanzo, kama unabeba uzito utajihisi hauongezi kitu tena.
Hata mazoezi utakua unayafanya kama kukamilisha ratiba.

Cha kufanya...
Badilisha routine yako yote. Kama ilikua jumatatu ndiyo unakimbia na jumanne unanyoosha viungo ifanye iwe kinyume chake. Hata wanyanyua uzito pindueni routine.
Pia kama hua unaanza mfano kukimbia kisha inakuja squats, anza squats maliza na kukimbia.
Ila kwa mnyanyua uzito usije ukabadili kwa kuanza na zoezi la mkono, hili mara zote hubaki mwisho.

Badilisha/ ongeza intake ya chakula.

Tafuta partner/ kama ulikua hauna.

Fanya zoezi lako kwa nguvu/ extreme.
 
Sina partner wa mazoezi, akitokea huwa wanakuwa wavivu na kupotea ndani ya muda mfupi, napenda mazoezi lakini baada ya muda mfupi napata uvivu na kuacha, naomba mbinu nikianza zoezi nisiache kamwe

Sent from my GT-N5100 using JamiiForums mobile app
 
Kitu poa kabisa baada ya kuanza mazoezi ni kupata matokeo ya zoezi lako, poa zaidi ni matokeo hayo yanapokuja kwa haraka.

Siyo kila mtu ana muda wa kufanya zoezi la masaa matatu, hell wengine hata saa moja kwao ni kupoteza muda.

Now uzi huu uwe special kwa ajili ya kugeana mbinu za kufikia malengo haraka, mbinu zitakazotolewa hapa ni za mazoezi yoyote.

Ni vizuri mbinu itakayotolewa iwe ambayo mtu ulishawahi kuitumia au kuiona mtu akiitumia ili likija swali unalijibu kwa uhakika.

Naanza na hizi.

1. Ukiwa unajivuta mikono usiitanue sana iwe na umbali wa usawa wa mabega yako.
Utatengeneza biceps, nguvu za mikono, mabega na 'mabawa' yatakuja kama kawaida.

2. Raundi zako ziwe 10 na seti 3 za mazoezi katika kila zoezi lako.

3. Kama unafanya zoezi la kifua anza na push ups, piga push ups za tambarare na miguu ikiwa juu ya kitu kisha nenda anza na incline bench press.

4. Ukiwa unakimbia usiteme mate na hema kwa kutumia pua, mdomo usiwe wazi. Utafikia levo ya juu kabisa ya kukimbia kwako pia utazuia kichomi.

5. Tafuta mwenza wa mazoezi.

6. Changanya juisi na peanut butter na itumie muda wote utakaokua ukifanya zoezi lako.

Zingine endeleeni wadau na mimi nitaendelea kutoa mbinu.
Nakubaliana na wewe ndugu Mwenyekiti..
 
Sina partner wa mazoezi, akitokea huwa wanakuwa wavivu na kupotea ndani ya muda mfupi, napenda mazoezi lakini baada ya muda mfupi napata uvivu na kuacha, naomba mbinu nikianza zoezi nisiache kamwe

Sent from my GT-N5100 using JamiiForums mobile app
Seti malengo ya unachotaka kukifikia kabla ya kuanza tizi.

Fuata hii routine pia

Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym
 
Seti malengo ya unachotaka kukifikia kabla ya kuanza tizi.

Fuata hii routine pia

Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym
Sasa mkuu nisaidie programme, nataka kufanya mazoezi kwa nia mbili kuu;

kwanza, nipunguze uzito na unene wa mafuta na kitambi japo si kikubwa.
Pili, nataka kujenga mwili mkakamavu mkono, wing na kifua.

Mazoezi haya yote nataka kufanyia nyumbani.
Mwanzo mgumu je programme ziweje ili niweze ku master zoezi zote utakazo nitajia, Ahsante sana.
 
Sasa mkuu nisaidie programme, nataka kufanya mazoezi kwa nia mbili kuu;

kwanza, nipunguze uzito na unene wa mafuta na kitambi japo si kikubwa.
Pili, nataka kujenga mwili mkakamavu mkono, wing na kifua.

Mazoezi haya yote nataka kufanyia nyumbani.
Mwanzo mgumu je programme ziweje ili niweze ku master zoezi zote utakazo nitajia, Ahsante sana.
Kwenye kupungua napendekeza kukimbia kuwe kila siku, squats, na mazoezi ya tumbo

Unataka Tumbo Flat na Six Packs? Cheki Hapa

Kwenye wings, kama unaishi nyumba yenye geti unaweza ukatumia lile eneo linaloachwa baada ya kufungua geti kwa ajili ya kujivuta.
Na unaweza ukapiga push ups ukiwa umetanua mikono zaidi ya kawaida.

Katika kuupata mwili mkakamavu, mikono na kifua fuata ile routine ya kwanza kukutumia.
 
Kwenye kupungua napendekeza kukimbia kuwe kila siku, squats, na mazoezi ya tumbo

Unataka Tumbo Flat na Six Packs? Cheki Hapa

Kwenye wings, kama unaishi nyumba yenye geti unaweza ukatumia lile eneo linaloachwa baada ya kufungua geti kwa ajili ya kujivuta.
Na unaweza ukapiga push ups ukiwa umetanua mikono zaidi ya kawaida.

Katika kuupata mwili mkakamavu, mikono na kifua fuata ile routine ya kwanza kukutumia.
Ahsante sana, mkuu naanza rasmi, ili kupata matokeo ya haraka inaweza chukua muda gani?
 
Ahsante sana, mkuu naanza rasmi, ili kupata matokeo ya haraka inaweza chukua muda gani?
Kama unafuata kila nilichoandika hapo na unakula chakula ipasavyo, unakunywa maji na kupumzika inavyotakiwa.

Wiki sita utakua umepata unachotaka.

Hiyo routine ya kukupa kifua, mikono na ukakamavu ndani ya siku tatu utakua ushajiona jinsi ulivyobadilika

Hii ni kwa ajili ya squats

JIFUNZE: Tengeneza Mwili wa chini bila kuingia Gym
 
Kama unafuata kila nilichoandika hapo na unakula chakula ipasavyo, unakunywa maji na kupumzika inavyotakiwa.

Wiki sita utakua umepata unachotaka.

Hiyo routine ya kukupa kifua, mikono na ukakamavu ndani ya siku tatu utakua ushajiona jinsi ulivyobadilika

Hii ni kwa ajili ya squats

JIFUNZE: Tengeneza Mwili wa chini bila kuingia Gym
Aisee, mkuu ubarikiwe sana upo full detailed nitakufollow kama nitakuwa na maswali zaidi, Usichoke mkuu wangu leo jioni naanza kukimbia rasmi. Nataka jioni niwe nakimbia na kufanya zoezi la tumbo then ahsubuhi nafanya workout za kujenga mkono na kifua. Je natakiwa kupumzika siku yoyote au ni mfululizo kwa week sita. ?
 
Aisee, mkuu ubarikiwe sana upo full detailed nitakufollow kama nitakuwa na maswali zaidi, Usichoke mkuu wangu leo jioni naanza kukimbia rasmi. Nataka jioni niwe nakimbia na kufanya zoezi la tumbo then ahsubuhi nafanya workout za kujenga mkono na kifua. Je natakiwa kupumzika siku yoyote au ni mfululizo kwa week sita. ?
Usijioverload chief fanya kidogo kidogo

Mazoezi ya kufanya kila siku ni tumbo, kukimbia, wings (kujivuta) na kama utapenda squat ila utafanya aina moja tu.
Tenga kila siku na zoezi lake kama wewe ni beginner.

Leo ukifuata routine ya miguu kesho fanya ya kifua na ukakamavu.

Hiyo inaipa misuli muda wa kupumzika na kuwa vile unavyotaka.
 
Ili kuepuka kupoteza muda na kushindwa kufanya baadhi ya mazoezi. Yaunge mazoezi yako katika routine ya siku moja.

Mfano, utapiga push ups 20, ukimaliza utafanya sit ups 20, ukimaliza utapiga squats 20.
Unaanza tena mwanzo na hii iwe bila kupumzika, kwakua hayo mazoezi hayahusiani hivyo hayatagusa eneo moja mara nyingi.
Mkuu hiyo sits up ndio zoezi gani?
 
Mkuu hiyo sits up ndio zoezi gani?
Ni zoezi la tumbo

Unakua umelala chali unayainua magoti ila nyayo zinakua bado zimegusa sakafu.

Mikono unashika kichwani, kisha unakua unainuka kuanzia usawa wa kiuno kuyafuata magoti.

Sit-ups.jpg


Ukiwa unarudisha chini mwili wako kichwa kisiguse chini
 
Back
Top Bottom