Shebe Mohamed Awadh, picha zake zimebeba historia ya TANU na Uhuru wa Tanganyika

Shebe Mohamed Awadh, picha zake zimebeba historia ya TANU na Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
7SHEBE MOHAMED AWADH MZALENDO ALIYEHIFADHI HISTORIA YA TANU NA HISTORIA YA JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA JICHO LA CAMERA YAKE

Katika ukuta wa nyumba ya mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed kulikuwa na picha kadhaa za sisi watoto wake.

Katika picha zile kulikuwa na picha moja mimi nikiipenda sana. Ilikuwa picha yangu nikiwa na umri a kiasi cha mwaka mmoja hivi kwa hiyo picha hiyo ilipigwa mwaka wa 1953. Nimeshakuwa mtu mzima na nina shughuli zangu siku moja nilikwenda kumjulia hali mama.

"Mohamed hebu panda hapo juu tungua hizo picha zako."

Nikapanda kwenye kiti nikazitungua.

Mama akazifuta vumbi kisha akanambia, ''Chukua hizi picha zako kaanazo mwenyewe.''

Kwa wakati ule sikutambua kuwa alikuwa ananipa urithi wangu na kuniambia kuwa yeye hana muda mrefu tena hapa duniani kwa hiyo alitaka anipe zile picha zangu.

Haukupita muda mrefu mama akafariki.

Katika picha hizi mojawapo ilikuwa picha hiyo niliyoitaja hapo juu picha ambayo mimi nikiipenda sana na yeye akijua kuwa naipenda.

''Picha hii mama kanipiga nani?''

''Picha hiyo alikupiga Shebe,'' mama alinijibu.

''Shebe akikupenda sana siku moja alikuja akanimbia, ''Hebu nipe rafiki yangu nikampige picha.''

Mama yangu Bi. Mwanaisha alikuwa anakaa Mtaa wa Kipata na Livingstone na mkabala wa nyumba yake hii aliyokuwa akiishi ilikuwa studio ya Shebe Mohamed Awadh.

Mtoto wa Mzee Shebe, Mbaraka Shebe tulikuwa tukifanyakazi pamoja bandarini na nikimfahamu pia na dada yake Masad lakini sikujua kwa wakati ule kuwa baba yao alikuwa rafiki yangu toka nazaliwa.

Nilipomuuliza Mbaraka kama yeye ni mtoto wa Mzee Shebe aliyekuwa na studio Mtaa wa Livingstone na Kipata akaniambia ndiyo na huyo ndiye baba yake.

Nimepata kumzungumza Mzee Shebe hapa jamvini mara kadhaa lakini kama kupita njia.

Mzee Shebe Mohamed Awadh hajatajwa popote katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika lakini picha nyingi ninazoziweka hapa zinatoka katika jicho la camera yake katika miaka ya 1950 na naamini Mzee Shebe ni mtu wa mwanzo kuweka kumbukumbu za Nyerere na harakati za kupigania uhuru katika picha.

Baada ya uhuru Mzee Shebe aliajiriwa na magazeti ya TANU, ''Uhuru,'' na ''The Nationalist '' kisha akahamishiwa Maelezo na mwisho SHIHATA alikomalizia utumishi wake na kustaafu.

Mtoto wa Mzee Shebe Mbaraka ametunfanyia hisani kubwa kwa kutufungulia kasha la picha alizoacha baba yake nasi tuziangalie na hizi anasema ni chache tu lakini zinatosha kuturudisha nyuma nusu karne kuona wapi tulipotoka.

Mbaraka ameahidi In Shaa Allah kutochotea picha katika kasha la baba yake kadri siku siku zinavyosogea mbele.

Picha kushoto ni Shebe Mohamed Awadh, John Rupia na Julius Nyerere.
Screenshot_20200820-230749.jpg
Screenshot_20200820-234533.jpg
IMG-20200819-WA0132.jpg
IMG-20200819-WA0083.jpg
 

Attachments

  • IMG-20200819-WA0069.jpg
    IMG-20200819-WA0069.jpg
    41.4 KB · Views: 5
  • Screenshot_20200820-235328.jpg
    Screenshot_20200820-235328.jpg
    43.4 KB · Views: 6
Naona kuna na nembo ya TBC hapo chini; hakika sijaelewa. Jina TBC limeanza enzi za Tido Muhando, yaani hata miaka 15 haijapita. Anyway, twendage hivyo hivyo
 
7SHEBE MOHAMED AWADH MZALENDO ALIYEHIFADHI HISTORIA YA TANU NA HISTORIA YA JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA JICHO LA CAMERA YAKE

Katika ukuta wa nyumba ya mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed kulikuwa na picha kadhaa za sisi watoto wake.

Katika picha zile kulikuwa na picha moja mimi nikiipenda sana. Ilikuwa picha yangu nikiwa na umri a kiasi cha mwaka mmoja hivi kwa hiyo picha hiyo ilipigwa mwaka wa 1953. Nimeshakuwa mtu mzima na nina shughuli zangu siku moja nilikwenda kumjulia hali mama.

"Mohamed hebu panda hapo juu tungua hizo picha zako."

Nikapanda kwenye kiti nikazitungua.

Mama akazifuta vumbi kisha akanambia, ''Chukua hizi picha zako kaanazo mwenyewe.''

Kwa wakati ule sikutambua kuwa alikuwa ananipa urithi wangu na kuniambia kuwa yeye hana muda mrefu tena hapa duniani kwa hiyo alitaka anipe zile picha zangu.

Haukupita muda mrefu mama akafariki.

Katika picha hizi mojawapo ilikuwa picha hiyo niliyoitaja hapo juu picha ambayo mimi nikiipenda sana na yeye akijua kuwa naipenda.

''Picha hii mama kanipiga nani?''

''Picha hiyo alikupiga Shebe,'' mama alinijibu.

''Shebe akikupenda sana siku moja alikuja akanimbia, ''Hebu nipe rafiki yangu nikampige picha.''

Mama yangu Bi. Mwanaisha alikuwa anakaa Mtaa wa Kipata na Livingstone na mkabala wa nyumba yake hii aliyokuwa akiishi ilikuwa studio ya Shebe Mohamed Awadh.

Mtoto wa Mzee Shebe, Mbaraka Shebe tulikuwa tukifanyakazi pamoja bandarini na nikimfahamu pia na dada yake Masad lakini sikujua kwa wakati ule kuwa baba yao alikuwa rafiki yangu toka nazaliwa.

Nilipomuuliza Mbaraka kama yeye ni mtoto wa Mzee Shebe aliyekuwa na studio Mtaa wa Livingstone na Kipata akaniambia ndiyo na huyo ndiye baba yake.

Nimepata kumzungumza Mzee Shebe hapa jamvini mara kadhaa lakini kama kupita njia.

Mzee Shebe Mohamed Awadh hajatajwa popote katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika lakini picha nyingi ninazoziweka hapa zinatoka katika jicho la camera yake katika miaka ya 1950 na naamini Mzee Shebe ni mtu wa mwanzo kuweka kumbukumbu za Nyerere na harakati za kupigania uhuru katika picha.

Baada ya uhuru Mzee Shebe aliajiriwa na magazeti ya TANU, ''Uhuru,'' na ''The Nationalist '' kisha akahamishiwa Maelezo na mwisho SHIHATA alikomalizia utumishi wake na kustaafu.

Mtoto wa Mzee Shebe Mbaraka ametunfanyia hisani kubwa kwa kutufungulia kasha la picha alizoacha baba yake nasi tuziangalie na hizi anasema ni chache tu lakini zinatosha kuturudisha nyuma nusu karne kuona wapi tulipotoka.

Mbaraka ameahidi In Shaa Allah kutochotea picha katika kasha la baba yake kadri siku siku zinavyosogea mbele.

Picha kushoto ni Shebe Mohamed Awadh, John Rupia na Julius Nyerere.View attachment 1543552View attachment 1543554View attachment 1543556View attachment 1543559
Wee mtu ww , m/mungu akupe maisha marefu maana tunaenda kuchukua nchi mwaka huu..ktk kuiandika upya historia ya nchi hii ww utakuwa ni moja ya watu muhimu Sana ..tuombee tu hii 2020 tuchukue nchi na naamini historia itakukumbuka huko mbeleni kuwa ulihifadhi mambo muhimu ya nchi yako kwa moyo wa kipekee ..ubarikiwe Sana kamanda
 
Naona kuna na nembo ya TBC hapo chini; hakika sijaelewa. Jina TBC limeanza enzi za Tido Muhando, yaani hata miaka 15 haijapita. Anyway, twendage hivyo hivyo
Ilianza TBC baadae ikaja kuwa RTD, TIDO akarudisha TBC.
 
Usiwasahau pia Watu kama kina Adrian Roden, Mzalendo aliyetunza kumbukumbu za TANU na harakati za uhuru kwa njia ya picha jongefu.

 
Cherry picking as usual on people who share own religious and/or tribal affiliations, however mediocre or insignificant their contributions to the welfare of ALL the people of this country, regardless of their religious, creed, ethnic or whatever background. Kama hoja ni historia ya mababu zako, kwanini uhangaikea sana kuutangazia umma wa Watanzania na dunia nzima kila kukicha, badala ya kuishia kuwasimulia wajukuu na vitukuu vyako wakati wa kwenda kulala kama ulivyosimuliwa wewe na babu na wajomba zako barazani Kariakoo?
 
Tanganyika Broadcasting Corporation,hii ilikuwa kabla ya kuundwa SHIHATA na redio kuitwa RTD.
Bali...
Radio ilianza Tanganyika 1952 ikiitwa Sauti ya Dar es Salaam.

Kisha ikawa Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) na baabae Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) kisha ikarudi TBC.
 
Bali...
Radio ilianza Tanganyika 1952 ikiitwa Sauti ya Dar es Salaam.

Kisha ikawa Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) na baabae Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) kisha ikarudi TBC.
Yaa ,nimekupata sheikh,Mimi nilianzia ilupokuwa Tanganyika Broadcasting Corporation.Asante Sana.
 
Mungu akupe umri mrefu ili tuendelee kupata elim hii adhim... Lkn Mungu atuwafikishe tuweze yazngatia yote Yale yanayowahusu wazee wetu
 
Asante Sana mzee wangu kwa kumbukizi. Mashujaa wa TANU na nchi hii kumbe wamejaa pomoni
 
Kama picha zinatosha kichapishwe kitabu chenye picha zaidi na maelezo yake.

Kama hiki hapa ni kitabu cha picha za rais Obama. Kina picha nyingi za urais wake na maelezo kuhusu hizo picha.
JPEG_20200823_090053_332955992171410323.jpg
 
Back
Top Bottom