Zamiluni Zamiluni
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 13,997
- 15,112
Karibu sana... safari study ni Moja ila kila mmoja wetu anafika ktk kituo chake maalum ...Asante mkuu.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Karibu sana... safari study ni Moja ila kila mmoja wetu anafika ktk kituo chake maalum ...Asante mkuu.
Poleni sana.Shaikh Ahmad Haidar Mwinyimvua
Katika miaka ya 50 kuendea 60 alikua mwanafunzi wa Muslim Academy Znz. Akasafiri kwenda Aden kabla ya kwenda Misri . Huko Misri alisoma miaka 13 .
Alikua mwalimu hodari wa Sharia na Lugha ya Kiarabu.
Aliwahi kwenda Mzumbe Morogoro kuwasomesha Mahakimu Ndoa na Mirathi ya Kiislamu. Baadae alikua ni Imamu wa Msikiti wa Mwinyi Kheri Akida. Hapo alidumu mpaka kufariki kwake.
Aliugua ugonjwa wa Kisukari. Alikua ni mkweli na mwenye uchungu wa Dini yake. Mara nyingi akituhimiza kusoma sana. Aliwahi kisomesha Lugha ya kiarabu Elimu ya watu wazima katika shule ya Gerezani. Mie nilikua ni mmoja katika wanafunzi wake aliowasomesha Lugha ya Kiarabu. Allah amrehemu na ajaalie kaburi lake linawirike kwa nuru ya elimu