Sheikh Hamisi Mataka: Nilivyokoseshwa elimu ya Sekondari

Sheikh Hamisi Mataka: Nilivyokoseshwa elimu ya Sekondari

SASA NDO ZAMA ZA UISLAM KUWA NA KUWA NA NGUVU ZINAVOANZA SASA.


ONA NAMNA ULAYA TARATIBU INAVYOSILIMU!!!


ONA NAMNA "NJAMA ZA AKINA NYERERE NA KANISA KATOLIKI" ZUNAVYOGUNDULIKA.

HAKIKA ZAMA ZA SASA UISLAM WAKUA SANA DUNIANI.
Kha!
 
Tatizo mnalalamika sana ,mngekuwa kama Gugume mngekuwa poa.Ebu sasa Kazeni buti kielimu.Tunaokaa wilaya ya Temeke tunaona udhaifu mkubwa toka level ya familia hadi kaya.Badilikeni ulalamishi hauleti ufumbuzi.Mshike elimu asiende zake.
Nyiokunda,
Sisi hatulalamiki sisi tunaandika na kuhifadhi historia yetu kwa kizazi hiki na kijacho.

Hilo la ''kukaza buti,'' chembelecho mbona nimeshalieleza hapa kuwa baada ya sisi
kuwashinda Waingereza na kupata uhuru wetu mwaka wa 1962 uliitishwa Muslim
Congress ya Kwanza na 1963 ikaitishwa Muslim Congress ya Pili na ilikuja azimio
la kujenga shule za msingi na sekondari pamoja na Chuo Kikuu chini ya EAMWS.

EAMWS ikaweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na liliwekwa na
Mwalimu Nyerere.

Haukupita hata miezi mingi huyu huyu Mwalimu Nyerere akaipiga marufuku EAMWS
kuwa ni taasisi haramu.

Kuanzia mwaka wa 1968 kila juhudi iliyofanywa na Waislam katika elimu serikali ilipiga
vita.

Wewe hujui historia ya Waislam lakini unataka kujadili mambo ya Waislam,
Hii haiwezi kuwa.

Soma kwanza uelimika ndiyo ujadili.
 
Madrid...
Hiyo ni ajabu kubwa sana kwa kuwa huwa kwa kawaida haiwi hivyo labda
ningeomba kujua kuwa huyo aliyopewa alikuwa Muislam?

Juu ya hayo nimefurahi kuwa na wewe umehakikisha kuwa Wizara ya Elimu
huwa wanakata majina.
Huo ni mtazamo wangu kwakua Baba yangu alikua anafaulu sana Darasani hatoki 5 bora lakini hakuchaguliwa secondary ndiyo maana yangu unalizungmziaje??[/QUOTE]
Madrid,
Hili unaloeleza si jambo la kawaida.
Kawaida ni kama nilivyoeleza na kuweka hapa mifano halisi.

Nimgependa kujua alipokatwa baba yako hiyo nafasi yake alipewa nani?
 
Nyiokunda,
Sisi hatulalamiki sisi tunaandika na kuhifadhi historia yetu kwa kizazi hiki na kijacho.

Hilo la ''kukaza buti,'' chembelecho mbona nimeshalieleza hapa kuwa baada ya sisi
kuwashinda Waingereza na kupata uhuru wetu mwaka wa 1962 uliitishwa Muslim
Congress ya Kwanza na 1963 ikaitishwa Muslim Congress ya Pili na ilikuja azimio
la kujenga shule za msingi na sekondari pamoja na Chuo Kikuu chini ya EAMWS.

EAMWS ikaweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu mwaka wa 1968 na liliwekwa na
Mwalimu Nyerere.

Haukupita hata miezi mingi huyu huyu Mwalimu Nyerere akaipiga marufuku EAMWS
kuwa ni taasisi haramu.

Kuanzia mwaka wa 1968 kila juhudi iliyofanywa na Waislam katika elimu serikali ilipiga
vita.

Wewe hujui historia ya Waislam lakini unataka kujadili mambo ya Waislam,
Hii haiwezi kuwa.

Soma kwanza uelimika ndiyo ujadili.
Link zako nimezisoma zote na nyingi Nukualiana na wewe .Tatizo baada ya hapo kama mlionewa kwa sasa ni hatua gani mnapiga hasa kwenye elimu?
 
Huo ni mtazamo wangu kwakua Baba yangu alikua anafaulu sana Darasani hatoki 5 bora lakini hakuchaguliwa secondary ndiyo maana yangu unalizungmziaje??
Madrid,
Hili unaloeleza si jambo la kawaida.
Kawaida ni kama nilivyoeleza na kuweka hapa mifano halisi.

Nimgependa kujua alipokatwa baba yako hiyo nafasi yake alipewa nani?[/QUOTE]
Unajua Mo swala siyo kapewa nani mzee wangu.Unajua ukija na mantiki ya kusema waislam wameonewa unakosea Kwa sababu hata wakristo nao walipitia majanga Mimi mwalimu secondary aliniambia yeye alikua yuko vizuri darasan akafeli mtihani wa mwisho akarudia darasa mara mbili hakuchomoka kabisa.

Ikabidi akapambana akaenda shule ya wakatoliki wakaona mbona kijana yupo Vizuri tu.Anakwambia enzi zao unaweza ukarudia hata mara 4 na usipate nafasi.

Mzee wangu shule aliyosoma alifaulu mwanafunzi 1 tu wilaya nzima hawa Fiki 10.Mi naamin ukweli unajua sema unajaribu kuupindisha.
 
Madrid,
Hili unaloeleza si jambo la kawaida.
Kawaida ni kama nilivyoeleza na kuweka hapa mifano halisi.

Nimgependa kujua alipokatwa baba yako hiyo nafasi yake alipewa nani?
Unajua Mo swala siyo kapewa nani mzee wangu.Unajua ukija na mantiki ya kusema waislam wameonewa unakosea Kwa sababu hata wakristo nao walipitia majanga Mimi mwalimu secondary aliniambia yeye alikua yuko vizuri darasan akafeli mtihani wa mwisho akarudia darasa mara mbili hakuchomoka kabisa.

Ikabidi akapambana akaenda shule ya wakatoliki wakaona mbona kijana yupo Vizuri tu.Anakwambia enzi zao unaweza ukarudia hata mara 4 na usipate nafasi.

Mzee wangu shule aliyosoma alifaulu mwanafunzi 1 tu wilaya nzima hawa Fiki 10.Mi naamin ukweli unajua sema unajaribu kuupindisha.[/QUOTE]
Madrid,
Nakuwa na subira kwa kuwa najua wewe huijui historia ya Waislam baada ya uhuru.
Mimi nina wajibu wa kukusomesha hadi ujue hata kama hukubaliani na mimi.

Umesoma kitabu cha Abdul Sykes?
Kila aliyekisoma kitabu hicho alitoka kabadilika.

Hebu tuanze hapo kwanza.
Usije na kesi moja ikawa umejenga hoja.

Nadhani umesoma mikasa ya wanafunzi wa Kiislam na Wizara ya Elimu nilizoweka
hapa.

Nakuongezea mkasa mwingine:
Mwalimu Bori Lilla alikuwa mwalimu Mkuu wa shule mbalimbali kwa miaka mingi.

Mzee Lilla alikuwa katika Kamati ya Kusahihisha Mitihani.

Baada ya kumaliza kusahihisha wakawa sasa wanaweka majina halisi badala ya no.
ili wanafunzi wafahamike.

Katika orodha yao kulikuwa na idadi kubwa tu ya wanafunzi Wakrsito na Waislam.

Mmoja wanakamati akaona orodha ya Mzee Lilla ina Waislam wengi akauliza kwa
sauti kali: ''Mbona orodha yako imejaa Waislamu?

''Wewe mgeni humu ndani?
Mzee Lilla akamjibu kwa sauti kali vilevile, ''Mimi siyo mgeni mimi Muislam.''

Ukimya ulitokea pale ulikuwa mkubwa.
Mzee Lilla haya kanihadithia kwa ulimi wake mwenyewe.

Ninaandika haya ili nyie msiojua kuwa lipo tatizo mfahamu na viongozi wetu
nao pia wajue ili watumie madaraka yao kuondoa dhulma katika nchi yetu
kwani dhulma ikiachiwa ishamiri huangamiza.
 
Link zako nimezisoma zote na nyingi Nukualiana na wewe .Tatizo baada ya hapo kama mlionewa kwa sasa ni hatua gani mnapiga hasa kwenye elimu?
Nyiokunda,
Swali lako linahitaji kutengenezwa ili hata wewe ulielewe.

Waislam hawana tatizo na mipango kama si hujuma Waislam wangekuwa na Chuo Kikuu
toka miaka ya ya mwishoni 1960 na shule za msingi na sekondari zingeendelea kujengwa.

Tatizo lipo katika taasisi za elimu kuanzia Wizara ya Elimu hadi Baraza la Mitihani (NECTA).

Miaka yote watoto wanapelekwa shule kusoma lakini tatizo lipo hapo juu na serikali imeelezwa
matatizo yaliyopo.

Waislam tumefika hadi kufanya maandamano ili hatua zichukuliwe kurekebisha mambo:

DSC04006%252520%2525282%252529.JPG

Maandamano haya yalianza Msikiti wa Kichangani yakiongozwa na
Sheikh Ponda hadi Wizara ya Mambo ya Ndani Waislam walipokabidhi
barua kwa serikali.

Mohamed Said: HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM - TAARIFA YA MUFTI WA BAKWATA SHEIKH SHAABAN BIN SIMBA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
Unachotala kutuambia hapa ni nini?
UDINI (kuonewa uislamu) kwenye kuchaguliwa kuingia sekondari toka la saba? Maana huko kwingine pamoja na kuwa mwalimu wa DINI na kuwa muislamu bado uliendelea..!!!

Huo ndio uhalisia, lengo ni kukatisha tamaa lakini kwakua hakuweza kukata tamaa, alipambana mpaka damu ya mwisho kuona aalichokitarget kinafanikiwa....
 
Unajua haya mambo ukweli ni kwamba islam mliwekeza sana kwenye madrassa na hii elimu ya kawaida mliichukulia kama ya wakristo, nimeishi sana lindi na mtwara naelewa kitu nachozungumza kilwa kisiwani nilikuta shule kubwa ya madrassa wanafunz wanaenda asubuhi wanarud jioni huo mda wa kwenda kusoma physics wanaupata wapi? Kwa hiyo wazee wenu aliinyapapaa elimu dunia na wamisionary waliwekeza kwenye elimu dunia, na hii dhana hadi leo ipo ndio mikoa waliokaa sana waarabu kiwango chao cha elimu ni kidogo

Hakuna kitu kama hiko, kusoma sana elimu ya dini kwa muislamu si kigezo cha kusema aipuuze elimu ya dunia.. .. Isipokua kinachofanywa ni hila na chuki za watawala ambao asilimia kubwa ni wakristo. Na ndio maana hata miaka ya juzi juzi waliamua kutuafuata mpaka ktk somo la dini, kuwakosesha wanafunzi wa kiislamu maksi zao za mtihani wa dini ili wadrop ktk kiwango cha ufaulu, aliyestahik kupata division one, akapata div two...

Serikali inaulizwa inakiri kwa kusema computer zimekosea, sasa swali linakuja computer zikosee ktk somo la dini ya kiislam tu?
 
Hakuna kitu kama hiko, kusoma sana elimu ya dini kwa muislamu si kigezo cha kusema aipuuze elimu ya dunia.. .. Isipokua kinachofanywa ni hila na chuki za watawala ambao asilimia kubwa ni wakristo. Na ndio maana hata miaka ya juzi juzi waliamua kutuafuata mpaka ktk somo la dini, kuwakosesha wanafunzi wa kiislamu maksi zao za mtihani wa dini ili wadrop ktk kiwango cha ufaulu, aliyestahik kupata division one, akapata div two...

Serikali inaulizwa inakiri kwa kusema computer zimekosea, sasa swali linakuja computer zikosee ktk somo la dini ya kiislam tu?
Mkuu umegusia mpaka mitihani ya dini ambayo haina tija kwa necta, mm nakuambia uhalisia elimu islam ni kipindi hiki tu wameijua ndio mana ufauru wa zanzibar ambako viongozi wake kuanzia ngazi ya juu hadi mjumbe ni islam ufauru wao duni shule
Msisingizie baraza mkuu
 
Mkuu umegusia mpaka mitihani ya dini ambayo haina tija kwa necta, mm nakuambia uhalisia elimu islam ni kipindi hiki tu wameijua ndio mana ufauru wa zanzibar ambako viongozi wake kuanzia ngazi ya juu hadi mjumbe ni islam ufauru wao duni shule
Msisingizie baraza mkuu
Ndugu zanguni,
Bahati mbaya wanaostahili kutoa majibu wako kimya wanajibu hao ambao hawahuusiki lolote katika shutuma hizi.
 
Ralph...
Rais Benjamin Mkapa alipoelezwa matatizo haya katika risala rasmi aliyosomewa
na viongozi wa Waislam alitoa majibu kama hayo yako na akaomba ushahidi wa
kisayansi.

Ushahidi wa kisayansi ukatayarishwa katika njia ya kitabu ili uwafikie watu wengu
zaidi.

Kitabu kilizuiwa uwanja wa ndege na baada ya kama siku mbili tatu hivi serikali ikatoa
tamko kuwa kitabu hicho kimepigwa marufuku hakiruhusiwi kuingia nchini.

Huo ndiyo ukawa mwisho wa ushahidi wa hiyo dhulma ambayo iliombwa upatikane
ushahidi wa kisayansi.

Toafauti yangu mimi na wewe ni kuwa sisi ni watendewa na tumekivaa kiatu kwa hiyo
tunajua upande gani kinabana.
Sheikh wangu ushahidi wa kisayansi una utaratibu wake wa kuupata. Hata rais Bush alikuwa na ushahidi kuwa rais Saddam alikuwa amelimbikiza silaha za maangamizi, lakini ulimwengu wote sasa unajua ushahidi ule ulikuwa batili.
Vipo vitabu vimeandikwa kwa data zilizopikwa, za uongo tu. Kama ni hadithi tu za utani wa wakurya na wahaya hazina matatizo. Lakini kama zinaweza kuleta maumivu ya hisia za watu wengi na bado ni za uongo, hizo ni za kupiga marufuku kabisa. Ni kwa msingi huohuo serikali ilikipiga marufuku kitabu cha mwandishi Salmin Rushdie kiitwacho "Satanic Verses", japo mwenyewe siku zote amedai yaliyomo ni ya kweli.
 
HUU NI UONGO MWEUPE... KWA VYOVYOTE VILE WAZEE WALITAKA WATOTO WAO WASOME ILA WASIALIBIWE IMANI ZAO.

UKRISTO NAO ULITUMIA MASHULE/ELIMU KAMA NJIA YA KUSAMBAZA UKRISTO.


HATA MKUTANO WA BERLIN ULISISITIZA HIVYO.

MIMI NI SHAHIDI NNA MIAKA 35,MAMANGU KAZALIWA 1959 ILA ASEMA AUJUA VIZURI UKRISTO KULIKO UISLAM.. MAANA HATA BAADA YA UHURU IMECHUKUA MIAKA SI PUNGUFU YA 7 KUTAIFISHA SHULE NA HATA WALIPOTAIFISHA MABAKI/KWA MAANA YA MASOMO YA UKRISTO YALIENDELEA KUWEPO.


MJOMBA ANGU MWINGINE ALISOMA HUKO, NA HAKUWA MAKINI NA DINI, NA WAISLAM WENGI WALIPATA SHIDA.


UKWELI NI KUWA HATA PALE WALIPOTAKA KUANZISHA SHULE WALIPATA VIKWAZO VINGI SAANA.

NA NANI ASIYE JUA NAMNA GANI UISLAM UNAHIMIZA SAANA ELIMU.

WAZUNGU WENYEWE ELIMU WALIITOA KWA WAISLAM.


HAYA MAMBO NI KWELI.. MSIKATAE..

AFU SOMENI KWANZA VITABU KABLA YA KUCOMMENT.
Rudia kusoma post yangu mstari kwa mstari halafu uoneshe uongo ulipo.
 
HIZI NI PROPAGANDA ZA WAMISHONARI KUWA WALIKOMBOA WATUMWA ZANZIBAR..

UONGO MTUPU.


KASUMBA HIZI TUMEFUNDISHWA MASHULENI.
Eti ni Propaganda? Tembelea makumbusho pale Zanzibar, Soko la Watumwa, nenda Bagamoyo hata Mombasa utakuta simulizi za freedom villages walikokuwa wakiishi watumwa waliokombolewa.
 
KWANI ULIAMBIWA FISADI HUIBA HELA YOTE KWA MKUPUO???


HUIBA KIDOGO KIDOGO ILI ASIJULIKANE, NA UFIKIRIE LABDA HUJUI MAESABU, AU UMEPATA HASARA.


HAYA MAMBO YAPO. PERIOD.

NO RESEARCH NO RIGHT TO SAY.


UNAKURUPUKA NDOTONI UNASEMA.

WENZAKO WAMERESEARCH KWANZA KABLA YA KUONGEA.

HIVI MNADHANI WATU WANAONGEAONGEA HOVYO???
Research gani inayozidi personal experience? Mtu amedai kuwa Kighoma Malima akiwa waziri wa elimu ndiye aliyeasisi utaratibu wa kutumia namba za mitihani katika mitihani badala ya majina. Nami nikashuhudia kuwa nilisoma shule ya msingi na sekondari kabla Malima hajawa waziri wa elimu na utaratibu tuliotumia kwenye mitihani ya mwisho ni wa namba na siyo majina. Wengine waliosoma miaka hiyo niliyotaja wamo humu na wanaweza kushuhudia kuwa nisemayo ni ya kweli.
 
Sheikh wangu ushahidi wa kisayansi una utaratibu wake wa kuupata. Hata rais Bush alikuwa na ushahidi kuwa rais Saddam alikuwa amelimbikiza silaha za maangamizi, lakini ulimwengu wote sasa unajua ushahidi ule ulikuwa batili.
Vipo vitabu vimeandikwa kwa data zilizopikwa, za uongo tu. Kama ni hadithi tu za utani wa wakurya na wahaya hazina matatizo. Lakini kama zinaweza kuleta maumivu ya hisia za watu wengi na bado ni za uongo, hizo ni za kupiga marufuku kabisa. Ni kwa msingi huohuo serikali ilikipiga marufuku kitabu cha mwandishi Salmin Rushdie kiitwacho "Satanic Verses", japo mwenyewe siku zote amedai yaliyomo ni ya kweli.
Ralph...
Mimi sina tatizo na hoja kama hizi zako kwani za kawaida kote penye dhulma.

Wale wanaofaidika hutupa lawama kwa muhanga.
Hili linafahamika.

Mimi niko hapa kustua akili za wananchi wenzangu na kuwagutusha viongozi wetu.

Wahusika wanajua na pembeni wanajadili linalowashinda ni kuukubali ukweli kwani uzito wake ni mkubwa sana.

Ndiyo maana wako kimya mnaojibu ni nyie.
 
Ralph...
Mimi sina tatizo na hoja kama hizi zako kwani za kawaida kote penye dhulma.

Wale wanaofaidika hutupa lawama kwa muhanga.
Hili linafahamika.

Mimi niko hapa kustua akili za wananchi wenzangu na kuwagutusha viongozi wetu.

Wahusika wanajua na pembeni wanajadili linalowashinda ni kuukubali ukweli kwani uzito wake ni mkubwa sana.

Ndiyo maana wako kimya mnaojibu ni nyie.
Sheikh wangu sisi hapa tunajadiliana tu, majibu hatuna. Nina sababu binafsi ya kutaka objectivity katika mjadala huu, zije hoja zenye ushahidi halisi (siyo wa hisia) kutoka pande zote za wanaojadiliana, na sote tuweze kuafiki yanayoafikika na kuyakataa yale ambayo bado yanaonekana kama ya kutunga tu. Sababu yangu ni hii: huu mfumo ambao baadhi ya waislamu wameulalamikia miaka yote na kuuita 'mfumokristo' haujawahi kunifaidisha kwa lolote wala sijawahi kuuona, japo miye mkristo. Ni fiction, mfumo wa kufikirika tu, haupo. Chochote nilichonacho nimekihangaikia kweli, sana. Kwahiyo sikubaliani na mtu anayesambaza uvumi kuwa kuna mfumo unaonipendelea, na hivyo kunijengea uhasama na wale wanaodaiwa kuonewa, ilhali sijapendelewa chochote. Na hata hao waislamu mnaosema wanaonewa, jamani, nimesoma nao shule za sekondari na chuo kikuu, na wengine walifaulu vizuri sana na sasa wengine ni maprofesa huko. Of course wapo waliofeli pia, kama wengine wa dini nyigine walivyofeli. Sijawahi kuona dini ikitumiwa dhidi ya mtu yeyote katika hatua zote za kitaaluma na kikazi nilizopitia, na nina makamo ya kutosha.
Napinga hili jambo kwa sababu linatufarakanisha kwa sababu za kutunga tu!
 
Hajui Ndalichako ALIKUBALI watoto wa kiislam kushushwa maksi ktk somo la Islamic knowledge...

Islamic Knowledge hata mtu angepata A, ilikuwa haisaidii lolote katika hesabu za kuchaguliwa kuendelea na masomo, kwa hiyo hoja hii haina mantiki. Mlishaambiwa ni tatizo la kiufundi kwa mtu aliyetengeneza formula ya Excel pale NECTA, lakini kwa kuwa wengi hamuelewi hata Excel inavyotumika, basi mmekazana tu Ndalichako, Ndalichako, Ndalichako!
 
Sheikh wangu sisi hapa tunajadiliana tu, majibu hatuna. Nina sababu binafsi ya kutaka objectivity katika mjadala huu, zije hoja zenye ushahidi halisi (siyo wa hisia) kutoka pande zote za wanaojadiliana, na sote tuweze kuafiki yanayoafikika na kuyakataa yale ambayo bado yanaonekana kama ya kutunga tu. Sababu yangu ni hii: huu mfumo ambao baadhi ya waislamu wameulalamikia miaka yote na kuuita 'mfumokristo' haujawahi kunifaidisha kwa lolote wala sijawahi kuuona, japo miye mkristo. Ni fiction, mfumo wa kufikirika tu, haupo. Chochote nilichonacho nimekihangaikia kweli, sana. Kwahiyo sikubaliani na mtu anayesambaza uvumi kuwa kuna mfumo unaonipendelea, na hivyo kunijengea uhasama na wale wanaodaiwa kuonewa, ilhali sijapendelewa chochote. Na hata hao waislamu mnaosema wanaonewa, jamani, nimesoma nao shule za sekondari na chuo kikuu, na wengine walifaulu vizuri sana na sasa wengine ni maprofesa huko. Of course wapo waliofeli pia, kama wengine wa dini nyigine walivyofeli. Sijawahi kuona dini ikitumiwa dhidi ya mtu yeyote katika hatua zote za kitaaluma na kikazi nilizopitia, na nina makamo ya kutosha.
Napinga hili jambo kwa sababu linatufarakanisha kwa sababu za kutunga tu!
Ralph...
Kama nilovyokueleza hapo mwanzo ikiwa huamini kuwa EAMWS ilivunjwa kwa kuwa ilikuwa na mipango imara ya kuwanyanyua Waislam mimi siwezi kukulazimisha uamini.

Lakini wahusika wakuu wanajua fika ukweli huu.
Utabakia hivyo hivyo huamini kuwa wapo wanaofaidika na hali hii lakini jua kuwa hutoacha kutusikia sisi tukiwakumbusha viongozi wetu kuhusu dhulma hii na wala si nia yetu kuleta farka katika jamii.

Allah katufunza Waislam kwa onyo kali akitueleza: "Msidhulumu wala msikubali kudhulumiwa."

Historia ya wazee wetu katika kupigania uhuru wa nchi yetu na kuleta haki na kujenga umoja mimi ndiyo niliyoiandika kwa huu mkono wangu unaoandika hapa tena nikiwa kijana wa miaka 30.

Historia hii kwa hofu tu ilifutwa lakini nimeirejesha na kitabu kinakwenda toleo la tano katika miaka 20.

Hakuna yeyote aliyesimama kusema mimi nimesema uongo.

Mimi kwa mkono huu ndiye niliyeweza ku-document historia nzima ya Baba wa Taifa toka siku ya kwanza anatia mguu wake anavuka kizingiti cha nyumba ya marehemu Abdulwahid Sykes nikaeleza yote na vipi alijulishwa kwa Sheikh Hassan bin Ameir na mipango yote iliyopita kote akitembezwa nchi nzima akifikia nyumba za Waislam hadi uhuru ukapatikana mwaka 1961.

Haiyumkiniki mimi kizazi cha wazalendo hawa niwe na haja ya kufarikisha.

Mkono huu ndiyo ulioandika pia kwa masikitiko makubwa yote yaliyotokea baada ya uhuru ya kuandikwa kwa historia ya TANU mwaka 1981 na kwa hofu na khiyana historia hii ikafutwa.

Vipi nikulazimishe uamini haya yote?

Lakini mimi hawa waliounda TANU na kupigania uhuru wa nvhi yetu ni wazee wangu na wengi nimewaona kwa macho yangu na wengine wameniona nikiwa mtoto na kuwajua wazazi wangu.

Hakika mimi na wewe hatuwezi kuwa sawa katika uelewa wa historia hii.
 
Back
Top Bottom