Sheikh Hassan Bin Ameir (1880 - 1979) na Waislam wa Burundi

Sheikh Hassan Bin Ameir (1880 - 1979) na Waislam wa Burundi

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
SHEIKH HASSAN BIN AMEIR (1880 - 1979) NA WAISLAM WA BURUNDI

''Waislam walipoona juhudi zao zote hizi zinagonga ukuta wakaona waombe msaada kwa kutoka kwa ndugu zao Waislam wa Tanganyika kupitia kwa Sheikh Hassan bin Ameir.

Waislam wa Burundi wakapata msaada na wakajenga shule moja ambayo hadi leo ipo Barabara ya Nane na ya Tisa, Buyenzi na inajulikana kwa jina la Jumuiyya.

Sheikh Hassan bin Ameir alialikwa aje Burundi kuifungua shule hii na ipo hadi leo.

Katika juhudi na harakati hizi taatifa za kikachero zikafikishwa serikalini kuwa Sheikh Hassan bin Ameir kutoka Tanganyika ndiye aliyekuwa akiwachochea Waislam wa Burundi dhidi ya Wabelgiji.

Haiyumkini kabisa kuwa Sheikh Hassan bin Ameir atakuwa kaingiliana na watu wa Rwanda kwa kiasi ile ikawa yeye hawaelezi hali ya siasa ya Tanganyika na vipi Warundi kwa kiasi kile cha kuwawezesha kujenga shule asiwafunze na mbinu za siasa za mapambano.

Uhusiano huu wa Sheikh Hassan bin Ameir na Waislam wa Burundi uliwatia hofu Wabelgiji kuwa kuna uwezekano mkubwa sana kwa Waislam wa Burundi wakajiunga na Waislam wenzao wa Tanganyika na kwengineko katika kupambana na serikali.

Katika hali hii ya fitna viongozi wa ya Wabelgiji wakaitisha mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa wazi na kuwataka wananchi wahudhurie mkutano ule.

Yawezekana sana kuwa nia ya mkutano huu ulikuwa kuwaonya wananchi na hasa Waislam kuhusu njama zozote za kupinga serikali. Kufika mchana uwanja wa mkutano ukawa umejaa watu wakisuburi kufika kwa Gavana kuwahutubia.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwapo katika mkutano huu pamoja na kundi kubwa la Waislam, wake kwa waume wamekaa sehemu yao wametulia wakisubiri kuwasili kwa Gavana uwanjani pale.

Kilichotokea pale uwanjani siku ile kilikuwa hakijaonekana.

Mara msafara wa Gavana ulipoingia uwanjani kwa vishindo vyote wanawake wa Kiislam wakasimama huku wanapiga vigelele kwa sauti ya juu sana.

Uwanja mzima ulipigwa na butwaa wakiwaangalia na kuwashangaa wanawake waliojitanda vizuri waliokuwa wakipiga vigelegele kumshangilia Gavana.

Uwanja ulisisimka na waliokuwapo wakawa wamepigwa na mshagao pamoja na Gavana mwenyewe. Walikuwa hawajapata kuona kitu kama hicho kabla.

Gavana alipokaa wale wanawake wakanyamaza na wao wakakaa. Ulipita ukimya mzito watu wakitafakari kile kilichotokea pale uwanjani.

Gavana aliposimama kuzungumza kitu cha kwanza alichouliza ni kuwa wale waliokuwa wanapiga vigelegele ni nani na wametokea wapi?

Gavana akaelezwa kuwa wale ni raia wake Waislam wakiongozwa na kiongozi wao kutoka Tanganyika, Sheikh Hassan bin Ameir.

Pale pale Gavana akawashukuru kwa kumuadhimisha kwa kiasi kile na akaagiza kuwa Sheikh Hassan bin Ameir ni mtu wa Mungu yeye na watu wake wasibughudhiwe.

Vyama vya siasa vilipoanza Burundi viongozi wa vyama hivi walikuja kuwa karibu sana na TANU kutokana na msingi huu alioweka Sheikh Hassan bin Ameir na Waislam hawakusita kujiunga kwa wingi katika vyama hivi.

Viongozi wa vyama hivi wakawa wanaiangalia TANU na viongozi wake kama taa ya kuwaangazi kwenye kile kiza chao chini ya Wabelgiji na walihangaika sana kutaka na wao watiwe katika ‘’Panafricanisme,’’ kama Warundi walivyoita yaani, Pan African Freedom Movement in East and Central Africa (PAFMECA).''

Huyu ndiye Mufti Sheikh Hassan bin Ameir ambae nimemtaja sana katika taazia ya Musa Kwikima nimekuleteeni kipande hiki ili mumjue alikuwa nani na nini ulikuwa mchango wake popote pale alipoiona dhulma iwe Tanganyika au nje ya mipaka ya Tanganyika.

PICHA: Shule iliyojengwa Burundi kwa msaada wa Sheikh Hassan bin Ameir katika miaka ya 1940. Majengo ya zamani na mapya ya hivi sasa.
AL JAMIATUL MUSLIM SCHOOL BUYENZI, BURUNDI.jpg
AL JAMIATUL ISLAMIYYA ECOLE BUYENZI.jpg
AL JAMIATUL ISLAMIYYA MAJENGO MAPYA BUYENZI.jpg
 
Idadi yenyewe ya Waislamu Burundi sidhani kama inaushawishi wowote, ni wachache sana hata sasa. Mkuu, unaweza siku 1 ukaleta historia ya mzee yeyote ambaye sio wa dini yako katika wale wapigania uhuru? Kwenye maktaba yako naona unao wa dini moja tu
 
Idadi yenyewe ya Waislamu Burundi sidhani kama inaushawishi wowote, ni wachache sana hata sasa. Mkuu, unaweza siku 1 ukaleta historia ya mzee yeyote ambaye sio wa dini yako katika wale wapigania uhuru? Kwenye maktaba yako naona unao wa dini moja tu
Mazindu...
Unakereka kusoma historia ya Sheikh Hassan bin Ameir, Iddi Faiz Mafungo, Sheikh Suleiman Takadir, Bi. Tatu bint Mzee, Mshume Kiyate, Abdallah na Maulid Kivuruga, Abdillah Schneider Plantan, Thomas Saudtz Plantan, Ramadhani Mashado Plantan, Sheikh Yusuf Badi, Yusuf Chembera, Msham Awadh, Zarula bint Abdulrahman...

Mimi nilipoona kuwa hawa wazalendo hawamo kwenye historia y TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika sikuwatafuta wana historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wawaandike, nilinyanyua kalamu nikaandika historia zao.

Ikiwa wewe unao wapigania uhuru wa dini yako unaodhani mimi nimewafanyia khiyana kwa kutoandika historia zao basi nawe nyanyua kalamu.

Hapajatokea mwandishi hadi hivi sasa aliyeandika maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa usahihi na umakini kunishinda na Nyerere si Muislamu, kiasi nimeihamasisha Kigoda Cha Mwalimu Nyerere chini ya Mwenyekiti wake Prof. Issa Shivji kutafiti maisha ya Mwalimu na kuandika kitabu.

Naingia Maktaba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mazindu...
Unakereka kusoma historia ya Sheikh Hassan bin Ameir, Iddi Faiz Mafungo, Sheikh Suleiman Takadir, Bi. Tatu bint Mzee, Mshume Kiyate, Abdallah na Maulid Kivuruga, Abdillah Schneider Plantan, Thomas Saudtz Plantan, Ramadhani Mashado Plantan, Sheikh Yusuf Badi, Yusuf Chembera, Msham Awadh, Zarula bint Abdulrahman...

Mimi nilipoona kuwa hawa wazalendo hawamo kwenye historia y TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika sikuwatafuta wana historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wawaandike, nilinyanyua kalamu nikaandika historia zao.

Ikiwa wewe unao wapigania uhuru wa dini yako unaodhani mimi nimewafanyia khiyana kwa kutoandika historia zao basi nawe nyanyua kalamu.

Hapajatokea mwandishi hadi hivi sasa aliyeandika maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa usahihi na umakini kunishinda na Nyerere si Muislamu, kiasi nimeihamasisha Kigoda Cha Mwalimu Nyerere chini ya Mwenyekiti wake Prof. Issa Shivji kutafiti maisha ya Mwalimu na kuandika kitabu.

Naingia Maktaba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mazindu...
Kutoka Maktaba soma ukitaka wengine nifahamishe In Shaa Allah ingia link hiyo hapo chini:

Mohamed Said

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tatizo la Hasan Ameir alikuwa anachanganya dini na siasa, na ndio waislam wengi wanavyofanya
 
Mazindu...
Unakereka kusoma historia ya Sheikh Hassan bin Ameir, Iddi Faiz Mafungo, Sheikh Suleiman Takadir, Bi. Tatu bint Mzee, Mshume Kiyate, Abdallah na Maulid Kivuruga, Abdillah Schneider Plantan, Thomas Saudtz Plantan, Ramadhani Mashado Plantan, Sheikh Yusuf Badi, Yusuf Chembera, Msham Awadh, Zarula bint Abdulrahman...

Mimi nilipoona kuwa hawa wazalendo hawamo kwenye historia y TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika sikuwatafuta wana historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wawaandike, nilinyanyua kalamu nikaandika historia zao.

Ikiwa wewe unao wapigania uhuru wa dini yako unaodhani mimi nimewafanyia khiyana kwa kutoandika historia zao basi nawe nyanyua kalamu.

Hapajatokea mwandishi hadi hivi sasa aliyeandika maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa usahihi na umakini kunishinda na Nyerere si Muislamu, kiasi nimeihamasisha Kigoda Cha Mwalimu Nyerere chini ya Mwenyekiti wake Prof. Issa Shivji kutafiti maisha ya Mwalimu na kuandika kitabu.

Naingia Maktaba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mara nyingi (Hapo kwa Nyerere ) ukiandika kuwahusu Wakristo, unaandika on negative side, mara chache sana (binafsi sijawahi kukuona ) unaweza kuwaandika in a positive way; kwa waislamu wenzio huwezi kusema chochote kuhusu wao kusisitiziana kuhusu elimu dunia hadi baada ya ile Abuja Islamic conference ya mwaka 1992; hilo hutolisema and you will pretend you know nothing.
 
Mara nyingi (Hapo kwa Nyerere ) ukiandika kuwahusu Wakristo, unaandika on negative side, mara chache sana (binafsi sijawahi kukuona ) unaweza kuwaandika in a positive way; kwa waislamu wenzio huwezi kusema chochote kuhusu wao kusisitiziana kuhusu elimu dunia hadi baada ya ile Abuja Islamic conference ya mwaka 1992; hilo hutolisema and you will pretend you know nothing.
Mazindu...
Weka hapa sote tuyasome ambayo nimemuandika Nyerere kwa ubaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laki...
Huijui historia ya Sheikh Hassan bin Ameir.
Akichukia dhulma.

Somo la kuchanganya dini na siasa ukitaka kujadili fungua uzi wako nije nikusomeshe kwa ushahidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hasan Ameir kama alikuwa hapendi dhulma angeenda kushtaki mahakamani, badala yake akawa anamponda Nyerere msikitini ili kumchonganisha na waislamu, ndio maana nyerere akamtimua nchini kwa uchonganishi
 
Hasan Ameir kama alikuwa hapendi dhulma angeenda kushtaki mahakamani, badala yake akawa anamponda Nyerere msikitini ili kumchonganisha na waislamu, ndio maana nyerere akamtimua nchini kwa uchonganishi
Laki...
Lete ushahidi wako hapa kama Sheikh Hassan alikuwa akimsema vibaya Nyerere.

Yote uandikayo hayana ithibati.
Ukiombwa ushahidi huleti.

Sheikh Hassan bin Ameir kama mahakamani angekwenda mwaka wa 1950 alipokuwa katika TAA Political Subcommittee kamati ya ndani iliyokuwa na mipango ya kuunda TANU mwanasheria wao Earle Seaton.

Angekuwa kioja mwaka wa 1968 kumpeleka Nyerere mahakamani.

Sasa hizi ghadhabu matumizi ya maneno,"kutimua," ya nini?

Tujadili tu kiungwana na kwa heshima na adabu historia ya nchi yetu ikae vizuri na wasomaji wastarehe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laki...
Lete ushahidi wako hapa kama Sheikh Hassan alikuwa akimsema vibaya Nyerere.

Yote uandikayo hayana ithibati.
Ukiombwa ushahidi huleti.

Sheikh Hassan bin Ameir kama mahakamani angekwenda mwaka wa 1950 alipokuwa katika TAA Political Subcommittee kamati ya ndani iliyokuwa na mipango ya kuunda TANU mwanasheria wao Earle Seaton.

Angekuwa kioja mwaka wa 1968 kumpeleka Nyerere mahakamani.

Sasa hizi ghadhabu matumizi ya maneno,"kutimua," ya nini?

Tujadili tu kiungwana na kwa heshuma na adabu historia ya nchi yetu ikae vizuri na wasomaji wastarehe.

Sent using Jamii Forums mobile app

kilichomfanya Ameir kufukuzwa Tanganyika ni mihadhara yake msikitini kuiponda serikali. waislamu wa Tanganyika walikuwa sahihi kuivunja EAMS ili waunde baraza lao la BAKWATA , badala ya kuongozwa na baraza lililoasisiwa Mombasa na Aga Khan
 
kilichomfanya Ameir kufukuzwa Tanganyika ni mihadhara yake msikitini kuiponda serikali. waislamu wa Tanganyika walikuwa sahihi kuivunja EAMS ili waunde baraza lao la BAKWATA , badala ya kuongozwa na baraza lililoasisiwa Mombasa na Aga Khan
Laki...
Maisha yake yote toka alipohamia Dar es Salaam mwaka wa 1940 Sheikh Hassan bin Ameir akifanya darsa katika misikiti mbalimbali mjini na darsa lake mashuhuri lilikuwa Msikiti wa Badawy Kisutu.

Hizi darsa ndiyo wewe unaita "mihadhara."

Hizi darsa zilikuwa za wazi.

Wala BAKWATA haikuundwa na Waislam kwani tayari walikuwa na jumuiya yao ya Waislam wa Afrika ya Mashariki na ikifanya makubwa.

Lete ushahidi kuwa BAKWATA imeundwa na Waislam.

Huwezi kuupata ni maneno tu yasiyo na ithibati yeyote.

Kuna msemo wa Kizungu unaosema, '' If you have patience you will see the end of everything.'' Maana yake kwa Kiswahili ni kuwa endapo utakuwa na subra utaona hatma ya kila kitu.

Huu mwaka wa 50 mjadala wa BAKWATA haujafikia kikomo na haijakubalika.

Bado hujajiuliza?

Waislam walikuwa na mchakato wa kujenga Chuo Kikuu.

Kweli inaingia akilini kuwa Waislam waivunje EAMWS wakati inajenga Chuo Kikuu na uongozi wa Waislam apewe mwalimu wa shule ya msingi na wamfukuze alim mkubwa Sheikh Hassan bin Ameir?

Hivi unajua kuwa IGP Hamza Aziz alipopewa amri ya kumkamata Sheikh Hassan bin Ameir alikataa kufanya hivyo?

Bado hujajiuliza?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mohamed Said, unafurahisha sana. BAKWATA inaungwa mkono na waislamu wa madhehebu yote, wassuni na washia, wasioiunga mkono ni kikundi kidogo cha waislamu wenye msimamo mkali wanaoitwa " Answar Sunna" . BAKWATA iko kila mkoa, kila wilaya inashughulikia matatizo yote ya waislamu , mirathi,ndoa, n.k
 
Mohamed Said ina maana hata sheikh mkuu wa Tanzania Mufti Zuberi humtambui?
 
kilichomfanya Ameir kufukuzwa Tanganyika ni mihadhara yake msikitini kuiponda serikali. waislamu wa Tanganyika walikuwa sahihi kuivunja EAMS ili waunde baraza lao la BAKWATA , badala ya kuongozwa na baraza lililoasisiwa Mombasa na Aga Khan
Bakwata ni ya serikali sidhani kama waislamu wananufaika nayo kwenye haki za misingi ya uislamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom