Sheikh Kaluta Amri Abeid ni nani katika historia ya taifa hili?

Sheikh Kaluta Amri Abeid ni nani katika historia ya taifa hili?

Eti nasikiaga huu uwanja ni wa chama tawala nikashangaa sana, je? Kwa kuwa huyu Sheikh Amri Abeid si ali2mia pesa ya umma ktk ujenzi wake? Kwnn iwe ya chama? Na hata nasikia uwanja wa Kirumba pale Mwanza ni ya chama cha majambazi. Mwenye uwelewa a2juze jamani!
Enzi za chama kushika hatamu hakuna aliyehoji pesa za serikali kujengea uwanja wa chama
 
UWANJA huu umechukua jina kutoka kwa Rais wa kwanza wa zanzibar. Sheikh Abeid Amani Karume (1905-1972), Tanzanian political leader, became the Zanzibar first president and vice president of the republic of Tanzania. He was one of Africa's least-known leaders.
wenzio wanaita Amri Abed ww unakuja na Abed amani hizi shule zenu za kata zinashida kweli.mnsomea ujinga tu.
 
tafuta kitabu kiitwacho ALMASI YA AFRIKA,ameandika mtoto wake.
utapata historia nzima ya Kaluta Abeid.

Naweza kukipata duka lipi la vitabu kwa Arusha au Dar?
 
View attachment 70146
Picha hii ilipigwa Mwanzoni mwa Miaka ya 50 wakati Mtanashati huyu akiwa Masomoni katika Chuo Kikuu cha Rabwah Nchini Pakistan.

Uwanja Maarufu wa Sheikh Amri Abeid kule Arusha umepewa jina lake, ndiye aliyekuwa Meya wa Kwanza Mwafrika katika iliyokuwa Tanganyika (Sasa Tanzania Bara) Alikuwa Meya wa Mji Mzizima sasa Dar es Salaam.
Nakupongeza kwa bidii uliyoonyesha ya kujifunza kwa kipindi kifupi sana.
 
Shule nzuri hii kumbe alikua mtu mkubwa, kwenye hicho kifo chake kama nikweli kilitokea ktk mazingira hayo, sina shaka Nyerere alihusika
Huyu jina lake kamili ni Sheikh Kaluta Amri Abedi. Alizaliwa na ni mwenyeji wa Kigoma. Alizaliwa mwaka 1924. Alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Magharibi ukiunganisha mikoa ya Kigoma, Tabora na Shinyanga wakati wa enzi ya ukoloni. Alikuwa Meya wa kwanza mweusi wakati wa enzi za ukoloni na aliendelea na nafasi hiyo hadi siku Tanganyika ilipopata Uhuru wake hapo mwaka 1964. Baada ya Uhuru, akawa Waziri wa kwanza wa sheria katika serikali huru ya Tanganyika. Baada ya hapo akahamia kwenye wizara ya utamaduni na michezo na akawa waziri katika wizara hiyo hadi mauti yake yalipomfika mwezi wa 7 mwaka 1964.


Yeye ndiye mwandishi wa Sheria za Kutunga Mashairi na Diwani ya Sheikh K. Amri Abedi, kitabu cha kwanza kabisa kufundisha sheria za kutunga mashairi.

Alifia Ujerumani alipokwenda kutibiwa na mazishi yake yalifanyika pale Temeke ambapo viongozi wa kubwa wa bara la Afrika akiwamo Marehemu Rais Jomo Kenyatta wa Kenya walihudhuria mazishi yake. Inaaminika kifo chake kilisabibishwa na kuwekewa sumu kwenye chakula alipokwenda Misri kikazi akiwa na Nyerere pamoja na Kawawa. Hadi leo hakuna uchunguzi wowote uliofanywa na serikali ili kugundua sababu ya kifo chake.
 
Back
Top Bottom