Sheikh Kundecha: Kimbunga Hidaya kimetokana na wanadamu kufanya maasi, amsifia na kumuombea Bomboko!

Sheikh Kundecha: Kimbunga Hidaya kimetokana na wanadamu kufanya maasi, amsifia na kumuombea Bomboko!

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Sheikh machachari Kundecha Akizungumza na chombo kimoja cha habari amemsifia mkuu wa wilaya ya Ubungo kwa kutekeleza maagizo ya dini katika opeareshi yake ya kupambana na madanguro na madada poa.

Sheikh Kundecha anasema Bomboko sio anatekeleza tu maagizo ya serikali bali maagizo ya Mungu hivyo anamuombea katika kutekeleza hayo majukumu yake.

Kundecha ameitaka pia serikali kutotoa vibali vya madanguro (sina hakika kama serikali ya Tanzania inatambua au kutoa vibali vya madanguro kama anavyodai Sheikh Kundecha).

Kundecha ameenda mbali zaidi kusema hata majanga ya asili ni hukumu kutoka kwa mwenyezi mungu. Anasema "Mwenyezi Mungu anaona wenyewe mamlaka hawasimamii mambo sawasawa hivyo anatoa maangamizo".

Amesisitiza Kimbunga, maporomoko na shida mbalimbali huwa vinaathiri sehemu zenye maasi.
 
Sheikh wangu namuomba achangie Ile biliion 39 anayodaiwa na aliowakamata na kuwaweka mahabusu siku tano bila kuwafikisha mahakamani kisha kuwaachia kwa kukosa hoja.

Japo miye ni Muislamu natambua fika hii sio nchi ya Kiislamu au ya dini nyingine yeyote.
 
'God of the gap's".

Na hapa Bado ubepari haujakomaa kisawasawa Tanganyika/Tanzania.

Ubepari uliookomaa na character za social ills,Hawa watu wa Imani watachanganyikiwa na watakuwa wanatabiri na kutaja siku ya ujio wa mwana wa adamu /Mpinga kristo/Allah kuangamiza ulimwengu na mambo kibao.

America apocalypse... (Former NASA Engineer na Bible student Edga c whisenant -alitabiri Unyakuo utakuwa 1988,akaangukia pua, 88 Reasons why the rapture will be 1988.& Bila kusahau on borrowed Time.)
Na watu wa Imani kibao walioochukilia serious Imani/dini wakati ni early inventions za homo sapiens katika Dunia.

Three great inventions by homo sapiens.(early).

1.Money
2.Nations.
3.God/gods.
 
Sasa tutazame hiyo operation waiitayo-operation danguro/dada poa.

Hapa ndio unaona uwezo mdogo wa viongozi chini ya mwamvuli wa Chama tawala CCM..

Watu wanauliza sababu za Africa kutokupiga hatua za maandeleo.

Wakati sababu zipo wazi, moja kubwa ni viongozi wasio na vision, kichwani uwezo mdogo wa kutafakari na kutatua changamoto za jamii.

Unakamata madada poa/wanawake wanaotafuta riziki kwa kutoa huduma ya sex/ ngono kama mwendawazimu, pasipo kutafakari kwa kina sababu za wadada kufanya kazi hiyo?

Na kama viongozi wanamijipesa wawajia mifukoni mwao "Dada poa/wanaofanya biashara hiyo"

Na ukitafakari zaiidi utakuta mzigo wa lawama unaangukia katika Chama tawala kilichoshindwa kutengeneza Mazingira rafiki ya watu kujipatia uchumii/kipato.

Hali ngumu ya uchumii biashara kama hizi kushamiri sio swala la kushangazaa hata kidogo.

Na watu wametofautiana njinsi ya kupambana na kubaliana na Hali ngumu za uchumi..

Na watu wengine hupenda kufanya shughuli hiyo vilie vile kama burudanii,

Former Miss universe Kelly McCarthy, alikuwa akitoa hotuba katika spanking university hotuba iliyokwenda kwa jina la Faithless anadai alikuwa na ndoto ya kufanya shughuli hiyo apate Radha mpya,(Sasa huu ni ulimwengu ambao baadhi ya majiji watu hulipa kodi kupata huduma ya sex.)
 
Sasa tutazame hiyo operation waiitayo-operation danguro/dada poa.

Hapa ndio unaona uwezo mdogo wa viongozi chini ya mwamvuli wa Chama tawala CCM....
Wewe ni mgonjwa! Suala la biashara ya ngono lipo mpaka ulaya na marekani kwenye nchi tajiri uko nako ccm ndio inatawala! Kuuza mwili ni biashara ya aibu na inafanywa na wagonjwa wa akili!! Kwa akili ya kawaida mtu mwenye kujitambua na mwenye akili hawezi kununua mwanamke alie jipanga barabarani usiku anauza mwili wake kwa kila mwanaume alie mbele yake!!

Ni biashara haramu just why wanaifanya usiku! Tena wanaifanyia mbali na familia zao na makazi yao!!

Huwezi kukubali mwanao aoe au kuolewa familia ambayo mama na dada zake mke wake/mume wanaojiuza!! Changudoa hana tofauti na shoga na wengi ni watumiaji wa madawa ya kulevya!
 
Wewe ni mgonjwa! Suala la biashara ya ngono lipo mpaka ulaya na marekani kwenye nchi tajiri uko nako ccm ndio inatawala! Kuuza mwili ni biashara ya aibu na inafanywa na wagonjwa wa akili!! Kwa akili ...
Wewe hata kunisoma na kunielewa umeshindwa.

Mnaona CCM,hata kuzalisha watu wenye capacity ya kusoma kwa ufahamu na kutafakari mmeshindwa.

Taifa mnalipeleka wapii?

Poor fellow.
 
Hidaya ni janga la asili tu kama tsunami, sheikh anamsingizia Mungu kaleta janga hilo kisa dhambi za wanadamu. Mungu gani huyo aangamize ukanda wa pwani tu kwa hidaya wakati hata bara kuna watenda dhambi wa kumwaga? Sheikh analeta hadithi za abracadabra
 
Hidaya ni janga la asili tu kama tsunami, sheikh anamsingizia Mungu kaleta janga hilo kisa dhambi za wanadamu. Mungu gani huyo aangamize ukanda wa pwani tu kwa hidaya wakati hata bara kuna watenda dhambi wa kumwaga? Sheikh analeta hadithi za abracadabra
Sahihi
 
Back
Top Bottom