Sheikh Mselem: Uamsho ilikuwa ni suala la kuwaandaa watu na Katiba Mpya

Sheikh Mselem: Uamsho ilikuwa ni suala la kuwaandaa watu na Katiba Mpya

Sheikh Mselem Ali, mmoja kati ya Masheikh wa Uamsho ambao wametoka Gerezani amesema mihadhara yao ilikuwa na nia ya kuwaamsha watu kudai Katiba Mpya.

Amesema kwa kipindi kile walifanya hivyo kwa kuwa kulikuwa na fursa ya maoni kuhusu Katiba Mpya. Walifanya hayo kwa mujibu wa sheria kwa kuwa katiba in ruhusu kila mtu kutoa mawazio au maoni yake

Aidha amesema hana chama cha siasa, na wala hana mamlaka ya kudai katiba mpya. Lakini ikitokea serikali inataka maoni kuhusu katiba mpya na wakiona anaweza kuchangia mawazo basi atashiriki.

Naona disco ndio lanaanza tena.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanajisahaulisha makusudi kumwagiwa tindikali wageni, kuchomwa moto makanisa wakati wa harakati za uamsho...
Hawakumbuki yule chagga kasisi wa kanisa katoliki alifanywa nini kule Zanzibar nyakati hizo.
Nakumbuka sana kipindi kile,hadi Jakaya na Dr Shein vichwa viliwauuma sana,naona ndiyo wakaamua kuchukua maamuzi magumu, maana hali ilizidi kua tete kila kukicha kuna tukio jipya,hadi na vile vitoto vya kizungu vilivyoletwa kwa kujitolea eti navyo wakavimwagia tindikali! Watu Wana rohoo ngumu sana!!
 
Kawatoa mama au imewatoa mahakama?yeye alichokisema (huyo mama yako) kesi zote zisizojitosheleza kwa ushahidi dpp azifute,na kwa ushauri huo watu wengi walifutiwa kesi zao na hivi sasa wako huru.
Hivi wewe unaamini kwa miaka 9 bado walikuwa wanakusanya ushahidi au walikuwa hawana ushahidi.
Kimsingi hao walikuwa ni wapinzani wa muungano,hawautaki kabisa na ndicho walichokuwa wanawahamasisha wazenji waukatae,ila wenye mamlaka hawakupenda misimamo yao na badala ya kujibu hoja zao,wao wakawafungulia kesi na kwa vile wao wanajiita wanamihadhara ya kiisilamu ikaonekana wakipewa kesi ya ugaidi itaeleweka vizuri zaidi na watu kama wewe ambao kwenu serikali huwa haiongopi.
Mkuu huu ujasiri hata hao Uamsho kabla hawajakamatwa walikuwa na ujasiri gunia 3,000 kuliko huu.

Nakusihi kasikilize mihadhara yao kabla na baada ya kuachiwa.

Dola ni shetani, hizo mahakama unazosema zinaongozwa na watu wenye familia zao na wanalipwa mishahara.

Kwa taarifa yako hao masheikh wakati wako mahabusu, kila mmoja alikuwa anakaa chumba chake tulivu, anahojiwa na mijitu haijui kivyake tena akiwa uchi wa mnyama ndani ya chumba tulivu chini ya ulinzi usio wa kawaida. Wakati huo wale wafuasi wa kukushangilia hawapo, kila mmoja huko nje anaendelea na maisha yake na wala familia yako hawapeleki hata mia ya dagaa.

Usichokijua hao uamsho wameachiwa kwa vifungu vya kisheria vya kutojihusisha tena na makosa ya aina hiyo, na ikitokea wakafanya sheria inaruhusu wote kukamatwa na kuwarudisha tena mahakamani kwa makosa yale yale. Sasa ukiwasikiliza wale wazee unaona wako tayari kwa hilo ? Angalia tu ulinzi namna walivyokuwa wanapelekwa mahakamani.

Hapo ndio utajua haki iko mbinguni tu.
 
Waache uongo bana, zile clip zao za kusema watamtoa mtu roho mbichi ndio kudai katiba??? Walikua wanaeneza ujinga tu wakawahiwa....
 
Waache uongo bana, zile clip zao za kusema watamtoa mtu roho mbichi ndio kudai katiba??? Walikua wanaeneza ujinga tu wakawahiwa....
Watu wanapiga tu kelele kwasababu tuko nje ya mfumo.

Hakuna mtawala anayependa kusumbuliwa hata kidogo.

Hata kama watawala wangekuwa Chadema, wakishaona kuna kundi linasababisha nchi isitawalike, tena wanaweza kufanya mabaya kuliko CCM.
 
Back
Top Bottom