Sheikh Rajabu Ibrahim Kirama na adhabu ya viboko Machame Nkuu 1930

Sheikh Rajabu Ibrahim Kirama na adhabu ya viboko Machame Nkuu 1930

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
SHEIKH RAJAB IBRAHIM KIRAMA NA ADHABU YA VIBOKO 1930

Naweka hapa kutoka kitabu, ''Rajab Ibrahim Kirama Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam,'' yale ambayo yamo humo kuhusu adhabu ya viboko:

''Siku ile baada ya kutoka pale Barazani kwa Mangi, Rajabu Kirama akajua kuwa anao watu wanaomuunga mkono katika kutafuta haki.

Hamasa na ghera ya Uislamu ikawa sasa inaenea chini ya Mlima Kilimanjaro.

Lyamungo, Waislamu wakafanya mkutano agenda kuu ikiwa kujenga msikiti na shule ya Waislamu siku zile wakiziita, ''Muslim School.''

Mzee Rajabu sasa akawa anazungumza na watu bila uoga.

Kabla ya kujenga msikiti pale Nkuu walikuwa wanaswali kwenye kijisikiti kidogo cha udongo na kuezekwa kwa nyasi.

Nje ya msikiti huu kulikuwa na mti jina lake '‘Mruka.’'

Muadhini alikuwa anapanda juu ya mti ule ndiyo anaadhini huku chini wako watu wanamlinda asishambuliwe.

Baada ya jaribio lile la kutaka kumuua Mzee Rajabu Waislamu wa Nkuu wakaamua kumpa ulinzi.

Nkuu ikawa imegubikwa na hofu ya chini kwa chini kuwa kuna uwezekano mkubwa pakazuka vurugu kubwa.

Mangi akamshitaki Mzee Rajabu na Waingereza wakamkamata Mzee Rajabu na kumfungulia mashtaka ya kumtukana Mangi.

Kesi ya Mzee Rajabu ilivuma Uchaggani kote na mahakama ilijaa watu kutoka kila sehemu kuja kusikiliza kesi ile.

Ilikuwa haijapata kutokea Mangi kumshitaki raia wake.

Hukumu ikawa Mzee Rajabu apigwe viboko saba kwa kosa la kumtukana Mangi.

Mzee Rajabu akamwambia hakimu kuwa yeye hatokubali kulala chini kuchapwa na mwanamume mwenzake.

Hukumu hii ya viboko ilikusudiwa kumdhalilisha na kushusha hadhi yake mbele ya jamii na wale wote waliokuwa nyuma yake.

Hukumu ilibadilishwa na Mzee Rajabu Ibrahim Kirama akafungwa siku tatu kwa kosa la kumtukana Mangi.

Soma:

 
Picha ya Sheikh Rajab Ibrahim Kirama:

Screenshot_20210104-060753~2.jpg
 
Mkuu kila tukio linaloibuka naona unajaribu kulitafutia link na 'historia ya uisilamu'
 
Anajribu kuafutia link na uislamu?Au anaeleza kwamba haya sio mapya yalishatokea?
Basi awashauri kama kuna waisilamu waliochapwa siku ile, wakamshtaki DC polisi
 
Mkuu kila tukio linaloibuka naona unajaribu kulitafutia link na 'historia ya uisilamu'
Faru...
Ndiyo nilivyojaaliwa.

Jambo lolote nikisoma au kushuhudia haraka sana akili yangu inaingia katika historia kuangalia wapi limepata kutokea.

Hapa Tanzania nimetafiti na kuandika vitabu 10 vyote vimegusa historia ya Uislam na Waislam hasa katika kipindi kile cha Waafrika kujitambua 1929 - 1961.
 
Faru...
Ndiyo nilivyojaaliwa.
Jambo lolote nikisoma au kushuhudia haraka sana akili yangu inaingia katika historia kuangalia wapi limepata kutokea.
Hapa Tanzania nimetafiti na kuandika vitabu 10 vyote vimegusa historia ya Uislam na Waislam hasa katika kipindi kile cha Waafrika kujitambua 1929 - 1961.
Hivyo vitabu vinatambuliwa rasmi na mamlaka za serikali hasa katika matumizi ya formal education?
 
Anajribu kuafutia link na uislamu?Au anaeleza kwamba haya sio mapya yalishatokea?
Andoza,
Ni tatizo jinsi mtu anavyoweza kuelewa jambo.

Ndugu yetu anataabika kusoma historia ambayo hakuwa anajua ipo.
 
Uchagani pia kuna eneo linaitwa Kwa Sadala linapakana na Machame, kuna waislam wengi.

Unaweza kutupa historia fupi ya huyu Sadala au eneo hili?
 
Hivyo vitabu vinatambuliwa rasmi na mamlaka za serikali hasa katika matumizi ya formal education?
Faru...
Vitabu vyangu havipo katika mtaala wa elimu wa serikali lakini vipo viwili vinasomeshwa nje ya Tanzania.

"The Life and Times of Abdulwahid Sykes the Untold History of Muslim.Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (1998) kinasomeshwa kwenye vyuo vingi Ulaya na Marekani vinavyosomesha African History.

"The Torch on Kilimanjaro," (2007) kinasomeshwa katika shule za msingi Kenya, Uganda na nadhani na Malawi kama kitabu cha kujifunza historia na lugha ya Kiingereza kwa pamoja.

Ingawa vitabu vyangu haviko katika mtaala Tanzania kwengineko vinasomwa na kufundishwa.
 
Picha ya Sheikh Rajab Ibrahim Kirama:View attachment 1667074
Ila dini zilituvuruga sana waafrika!

Waliozileta walifanikiwa kumnyang'anya mwafrika asili yake na kumpandikiza tamaduni nyingine na kuweza kumtawala na kumfanya watakavyo.

Kirama hapo amevaa na kujiweka kama mwarabu ili aweze kutoa maelekezo ya kiarabu kwa waafrika wenzake...Unyonge wa mwafrika!!
 
Basi awashauri kama kuna waisilamu waliochapwa siku ile, wakamshtaki DC polisi
Mkuu,Kumchapa binadamu mtu mzima bakora kienyeji ni utovu wa nidhamu uliotukuka.Soon tutaanza kuwa na magaidi kama huu ushamba ukiendelea.Mark my words
 
Kutojua uwepo wa kitu kilichoandikwa ni jambo moja, ukweli wa kinachoandikwa ni jambo lingine
Faru...
Baadhi ya kazi zangu zimechapwa na Oxford University Press, East Africa na New York.

Naamini umeelewa.
 
Ila dini zilituvuruga sana waafrika!

Waliozileta walifanikiwa kumnyang'anya mwafrika asili yake na kumpandikiza tamaduni nyingine na kuweza kumtawala na kumfanya watakavyo.

Kirama hapo amevaa na kujiweka kama mwarabu ili aweze kutoa maelekezo ya kiarabu kwa waafrika wenzake...Unyonge wa mwafrika!!
Ngorunde,
Uislam upo kijijini Nkuu Machame sasa miaka 90.

Hapajatokea vita.

Ama kuhusu utamaduni wa Mwafrika Wachagga ni wale wale.

Kuhusu kutawaliwa Tanganyika iko huru na waliokuwa mstari wa mbele kabisa kupambana na ukoloni ni Waislam.

Nimeandika sana kuhusu somo hili.

Ukipenda naweza kukuwekea link nyingi tu ukasoma historia ya Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Yusuf Badi, Sheikh Suleiman Takadir kwa kuwataja wachache.
 
Faru...
Baadhi ya kazi zangu zimechapwa na Oxford University Press, East Africa na New York.
Naamini umeelewa.
Kuna vitabu vimechapwa na Mwanzo Educational Publishers (MEP) ya hapa hapa nchini, na vinatumika katika mtaala wa elimu wa Tanzania
Naamini umenielewa
 
Kuhusu kutawaliwa Tanganyika iko huru na waliokuwa mstari wa mbele kabisa kupambana na ukoloni ni Waislam.
Historia rasmi inayofundishwa Tanzania inatuambia Mwalimu Julius K. Nyerere alikuwa ni mmojawapo wa watu waliokuwa mstari wa mbele kabisa kupambana na ukoloni, na wala hata hiyo historia haitaji dini ya huyo mpambanaji
 
Kuna vitabu vimechapwa na Mwanzo Educational Publishers (MEP) ya hapa hapa nchini, na vinatumika katika mtaala wa elimu wa Tanzania
Naamini umenielewa
Faru...
Vipi nisikuelewe ilhali mimi ni mwandishi wa vitabu?
Angalia hapo chini:


Vitabu hivi na wachapaji wake ni mashuhuri.

Huu ni mfano mmoja tu lakini kwa ajili ya staha huo unatosha.
 
Back
Top Bottom