Shemeji yangu anataka kunishitaki ili achukue ardhi niliyopewa na marehemu Baba Mkwe

Shemeji yangu anataka kunishitaki ili achukue ardhi niliyopewa na marehemu Baba Mkwe

Kingsmen

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2020
Posts
279
Reaction score
213
Poleni na majukumu wataalam, naombeni msaada kidogo katika hili jambo...

Miaka ya nyuma kidogo au naweza nikasema ni late 80`s nilifanikiwa kukabidhiwa ardhi na baba angu mkwe ambae mimi nilioa binti yake wa pili kwa kuzaliwa. Kutokana na ukaribu wetu mimi na mkwe wangu akaamua kunikabidhi ardhi mimi na mume mwenzangu aliyeoa binti yake wa kwanza.

Huyu mzee alifariki mwanzoni mwa miaka ya 90 hivyo wenzetu wengine waliooa baada ya kufariki hawakuweza kupata hiyo bahati.

sasa huyu mume mwenzangu yeye aliuzaga ardhi yake muda mrefu sana ila mimi sio mtu wa tamaa na ukizingatia naishi mbali kidogo hivyo kule kijijini nimefanya kama sehemu ya kuzalisha tu.

sasa juzi mke wangu alienda kwao kidogo kuwatembelea ndipo ndugu zake wakamueka mtu kati na kumueleza kuwa wamepanga kufungua kesi ili nipokonywe ardhi niliyopewa na baba mkwe kwa hiyari yake..

Na ambaye ame initiate hiyo sikomoko ni shemeji yangu anaefuata baada ya kuzaliwa mke wangu. Maana ndie mtoto wa kiume yeye alizaliwa middle 70`s .

sasa nilikua naomba maelekezo kwa wanaofahamu vizuri sheria katika jambo kama hili mlolongo wake upoje..

Mimi sitaki ugomvi na hii familia, na sihitaji kutumia nguvu kubwa kuendesha kesi nahitaji sheria ifuate mkondo na kama ikihitajika nguvu basi naweza pia kufanya hivyo..

Nawasilisha.
 
Poleni na majukumu wataalam, naombeni msaada kidogo katika hili jambo...
Miaka ya nyuma kidogo au naweza nikasema ni late 80`s nilifanikiwa kukabidhiwa ardhi na baba angu mkwe ambae mimi nilioa binti yake wa pili kwa kuzaliwa. Kutokana na ukaribu wetu mimi na mkwe wangu akaamua kunikabidhi ardhi mimi na mume mwenzangu aliyeoa binti yake wa kwanza.....a.
Pole sana

1. Una hati ya eneo au document inayothibitisha umiliki wako?

2.Viongozi wa mtaa na majirani wanakufahamu?

Jibu kwanza Hapo ili Mahakama ya JF tukusaidie
 
Pole sana

1. Una hati ya eneo au document inayothibitisha umiliki wako?

2.Viongozi wa mtaa na majirani wanakufahamu?

Jibu kwanza Hapo ili Mahakama ya JF tukusaidie
Hapana hati sina, ila wakati ananikabidhi palikuwepo na mashahidi akiwepo mamamkwe ambaye bado yupo hai..

pia alikuwepo mume mwenzangu alieyetangulia kupewa ardhi..

Mke wangu pia alikuepo alithibitisha jambo hilo na dada yake ambaye ndiye wa kwanza kuzaliwa wote walikuwapo na bado wapo hai..

pia alikuwapo mzee ambae kwa wakati huo alikua kama mwenyekiti ila sidhani kama bado yupo hai
 
Hapana hati sina, ila wakati ananikabidhi palikuwepo na mashahidi akiwepo mamamkwe ambaye bado yupo hai..

pia alikuwepo mume mwenzangu alieyetangulia kupewa ardhi..

Mke wangu pia alikuepo alithibitisha jambo hilo na dada yake ambaye ndiye wa kwanza kuzaliwa wote walikuwapo na bado wapo hai..

pia alikuwapo mzee ambae kwa wakati huo alikua kama mwenyekiti ila sidhani kama bado yupo hai

Mbona wote ulowataja ni ndugu wa shemeji yako??? Una uhakika gani kama hawatomtetea ndugu yao?
Epuka migogoro isoya lazima, mwanaume unarithishwaje ardhi ya ukweni?!! Labda kama jamii yako ni matrilenea!!

Mjanja aliyepewa na kuuza.
 
Mbona wote ulowataja ni ndugu wa shemeji yako??? Una uhakika gani kama hawatomtetea ndugu yao?
Epuka migogoro isoya lazima, mwanaume unarithishwaje ardhi ya ukweni?!! Labda kama jamii yako ni matrilenea!!

Mjanja aliyepewa na kuuza.
Ni haki ya wanao nadhani ndio lengo kuu LA baba mkwe,hivyo basi pambana ingali hao mashaidi wapo Waite viongozi+mashaidi andikia watoto update hati miliki,tafuta mwanasheria aweza kukufungua zaidi
 
Give up and do other things! Haya mambo not worth fighting for.... wakikupeleka mahakamani, waache wachukue! Mnatoana roho kwa Mali ya wakwe Kaka? Tena ya kijijini? You are better than that!

Utalogwa wewe na mke uwaachie wengine waende leo naye!
 
Ni haki ya wanao nadhani ndio lengo kuu LA baba mkwe,hivyo basi pambana ingali hao mashaidi wapo Waite viongozi+mashaidi andikia watoto update hati miliki,tafuta mwanasheria aweza kukufungua zaidi
sijakuelewa mkuu naomba unifafanulie hapa zaidi kidogo nipate mwanga. asante
 
Give up and do other things! Haya mambo not worth fighting for.... wakikupeleka mahakamani, waache wachukue! Mnatoana roho kwa Mali ya wakwe Kaka? Tena ya kijijini? You are better than that!

Utalogwa wewe na mke uwaachie wengine waende leo naye!
Ni kweli mkuu aisee nimekuelewa sana asante
 
Ni kweli mkuu aisee nimekuelewa sana asante

Achana nayo mkuu haina haja tena msifike hata mahakamani wambie wachukue, mimi Mzee wangu alipewa nyumba Kinondoni na Marehemu babu yangu yani baba yake mama, na hati alimpatia ila alipofariki wajomba na mama wadogo wakauza vitu vyote wakaja kutaka ile nyumba, Mzee aliwapa kuepusha ugomvi nayo wakauza.

Haikuishia hapo kuna ndugu yetu mwingine alifariki, nilikuwa nikimrefer kama shangazi japo hakuwa ndugu yake baba na alikuwa mkubwa zaidi ya baba yang, akaacha kwenye wosia kaandika kwamba nyumba yake iliyoko temeke iwe mali ya mzee na mtoto mwingine wa kaka yake marehemu. Mzee aliwambia anashukuru ila yule mtoto aichukue ile nyumba nzima.

Haina haja kugombea mali hasa za ukweni kama unaweza kutafuta za kwako kwanza utakuwa unamweka mkeo kwenye wakati mgumu maana ni lazima achague kuwa upande wako ama wa familia yake, ebu jaribu kuvaa viatu vyake.
 
Achana nayo mkuu haina haja tena msifike hata mahakamani wambie wachukue, mimi Mzee wangu alipewa nyumba Kinondoni na Marehemu babu yangu yani baba yake mama, na hati alimpatia ila alipofariki wajomba na mama wadogo wakauza vitu vyote wakaja kutaka ile nyumba, Mzee aliwapa kuepusha ugomvi nayo wakauza.
Haikuishia hapo kuna ndugu yetu mwingine alifariki, nilikuwa nikimrefer kama shangazi japo hakuwa ndugu yake baba na alikuwa mkubwa zaidi ya baba yang, akaacha kwenye wosia kaandika kwamba nyumba yake iliyoko temeke iwe mali ya mzee na mtoto mwingine wa kaka yake marehemu. Mzee aliwambia anashukuru ila yule mtoto aichukue ile nyumba nzima.
Haina haja kugombea mali hasa za ukweni kama unaweza kutafuta za kwako kwanza utakuwa unamweka mkeo kwenye wakati mgumu maana ni lazima achague kuwa upande wako ama wa familia yake, ebu jaribu kuvaa viatu vyake.
Sawa kiongozi nimekuelewa
 
achana nayo waachie ata msifikishane mahakamani ardhi tena ipo kijijni WAACHIE
 
Achananao.. mali ya ukweni haina hata mzuka ku pambana nayo, mbaya zaidi ipo bush.


Mtakuja kuuana.

Itoshe kusema , achananayo.
 
Poleni na majukumu wataalam, naombeni msaada kidogo katika hili jambo...

Miaka ya nyuma kidogo au naweza nikasema ni late 80`s nilifanikiwa kukabidhiwa ardhi na baba angu mkwe ambae mimi nilioa binti yake wa pili kwa kuzaliwa. Kutokana na ukaribu wetu mimi na mkwe wangu akaamua kunikabidhi ardhi mimi na mume mwenzangu aliyeoa binti yake wa kwanza.

Huyu mzee alifariki mwanzoni mwa miaka ya 90 hivyo wenzetu wengine waliooa baada ya kufariki hawakuweza kupata hiyo bahati.

sasa huyu mume mwenzangu yeye aliuzaga ardhi yake muda mrefu sana ila mimi sio mtu wa tamaa na ukizingatia naishi mbali kidogo hivyo kule kijijini nimefanya kama sehemu ya kuzalisha tu.

sasa juzi mke wangu alienda kwao kidogo kuwatembelea ndipo ndugu zake wakamueka mtu kati na kumueleza kuwa wamepanga kufungua kesi ili nipokonywe ardhi niliyopewa na baba mkwe kwa hiyari yake..

Na ambaye ame initiate hiyo sikomoko ni shemeji yangu anaefuata baada ya kuzaliwa mke wangu. Maana ndie mtoto wa kiume yeye alizaliwa middle 70`s .

sasa nilikua naomba maelekezo kwa wanaofahamu vizuri sheria katika jambo kama hili mlolongo wake upoje..

Mimi sitaki ugomvi na hii familia, na sihitaji kutumia nguvu kubwa kuendesha kesi nahitaji sheria ifuate mkondo na kama ikihitajika nguvu basi naweza pia kufanya hivyo..

Nawasilisha.
Kwa makadirio ya haraka haraka thamani ya hiyo ardhi inaweza ikafika kama shilingi ngapi?
 
Hapana hati sina, ila wakati ananikabidhi palikuwepo na mashahidi akiwepo mamamkwe ambaye bado yupo hai..

pia alikuwepo mume mwenzangu alieyetangulia kupewa ardhi..

Mke wangu pia alikuepo alithibitisha jambo hilo na dada yake ambaye ndiye wa kwanza kuzaliwa wote walikuwapo na bado wapo hai..

pia alikuwapo mzee ambae kwa wakati huo alikua kama mwenyekiti ila sidhani kama bado yupo hai
Mapandidhi mzee baba
 
Kwa kawaida kesi ya ardhi kama hizi zinakuwa na mlolongo mrefu sana na unaweza fungua kesi ukatumia garama ambayo pengine ungenunulia mashamba mengi zaid ya hiyo,kwa maelezo yako hapo huna haki ya hilo eneo kwa sabab kuu moja huna hati miliki ya maandishi yenye ukwel wa makabidhiano na baba mkwe wako,pili mashaihid unaowategemea wanaweza kuwa msaaada lkn sio kwa asilimia 100 bali 40 Tena endapo watakuwa wacha mungu,mwisho nakushauri achana na hilo eneo katafute yako mkuuu
 
Achana na mali za ukweni. Kwanza umepewa bila maandishi ndio maana wanaona kuna possibility ya kulitwaa hilo eneo. Kwani akukuwa na vikao baada ya msiba ili kugawanya mali za marehemu (mirathi)? Na je hao shemeji zako walikuwa na taarifa kuwa ulipewa hilo eneo. Achana na mali za ukweni tafuta zako na za upande wako. Kama ufuatiliaji wa mali za ukweni afanye mkeo sio wewe. Kwanza kisheria wewe sio mrithi upande wa mkeo
 
Nakushauri waachie eneo hilo ki roho safi.
Unampa mkeo hali ngumu kisaikolojia kwamaana pande zote za mgogoro ana maslahi.
We mwanaume bwana,utatafuta mbele kwa mbele.Huyo shemeji atazinywa hizo hela na atakurudia kulia shida kwako.
 
Back
Top Bottom