Kuhusu uhuru wetu,ni jambo zuri kwamba leo tunasherehkea miaka 47 ya uhuru.
Lakini nadhani statement ya Daily News ya kusema kwamba Ndugu Rais alisema juzi alipokuwa Mvomero,kwamba ,the government does have a monopoly to violence,nadhani this statement is very provocative.Kwa sababu hii ni sawa na kusema kwamba Ndugu Rais aliyetangaza vita dhidi ya ufisadi,sasa ametoa ruhusa kwa mafisadi kuwashambulia wananchi. Haya maneno yalizungumzwa kiswahili,na ningependa sana kufahamu ni nini hasa alichosema Ndugu Rais.
Lakini,ina maana kwamba Daily News ambacho ni chombo cha Serikali,linachochea fujo. Sasa uhuru uko wapi?Hata Freeman Mbowe jana alikuwa anaongea khusu mawaziri wanaoleta vitisho.
Mafisadi ambao wameliibia Taifa wanazungumza maneno haya,adding insult to injury.
Wao wanagombana na Serikali,na ni gari za Polisi ndizo zinazopiga hodi nyumbani kwao kuwapeleka Mahakamani. Kwa hiyo hawana sababu ya kugombana na raia wa kawaida.