Sheria ambazo hazizungumzwi lakini zipo

Sheria ambazo hazizungumzwi lakini zipo

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241113_150916_Google.jpg

Unapokuwa na kampani ya watu katika mazungumzo yenu,endapo utapigiwa simu basi usiongee na simu kwa mda mrefu

Unapoenda kumtembelea mtu, baada ya kitambo kidogo ukisikia mwenyeji wako anasema anajisikia kuchoka, basi ujiongeze mda wa kuondoka umefika

Mtoto mdogo anapokuonyesha kitu basi onyesha kushangaa na kufurahishwa nacho, ina mpa furaha sana

Mtu anapo kuonyesha picha katika simu yake, basi usiswap kulia na kushoto kuangalia picha nyingine

Ukiazima gari la mtu basi kabla hujarirudisha hakikisha umelijaza full tank

Usijipige selfie mbele za watu, inawafanya watu wanao kuangalia kujisikia aibu kuona jinsi unavyohangaika sura ikae vizuri

Usimuombe mtu kitu ambacho unajua kabisa ndio hicho alichobakiwa nacho

Ni hayo tu!
 
"Mtoto mdogo anapokuonyesha kitu basi onyesha kushangaa na kufurahishwa nacho,ina mpa furaha sana"

Hii ilifanywa kazi miaka ya zamani kadogo, by now vitoto vimefunguka sana ukijifrahisha kinafiki kinagundua na kukukacha na mshangao wako wa kinafiki.
 
Back
Top Bottom