Sheria inasemaje baba anapotaka kuchukua mtoto aliyezaa na mwanamke ambae hajaoana nae?

Sheria inasemaje baba anapotaka kuchukua mtoto aliyezaa na mwanamke ambae hajaoana nae?

mtoto anayezaliwa nje ya ndoa au illegitimate child kisheria hatambuliki wala hana haki ya kurithi endapo utakufa ghafla bila kuacha usia jambo ambalo wato wengi hawajui ,lakini once you wiil legalize him or her she will be recognize legally na atakuwa na haki zote kisheria kama m,toto wako wa halali au wa ndoa so kuhalalishwa ndo kulegalize na hiyo ni baada ya mama mwenye mtoto kukubali.ukeeni manake ni upande wa mwanamke au mama
 
sheria ipo wazi mtoto kuwa chini ya mama akiwa u7,ila kama mama haeleweji baba anaweza mchukua akiweza kuwasilisha hoja vizuri mahakamani,sasa kama mtoto ni 8 old yrs jamaa akienda mahakamani ana shinda kesi chamsingi inabidi aka mhalalishe kwanza
 
Nashukuru sana kwa Mawazo yote yaliyotolewa!Kuhusu kuwaona Walimu baba yake alikwisha waona na infact aliitwa plae shuleni na kuelezwa hayo yote ambayo yameelezwa zuri zaidi hii ni mara ya pili kwa Walimu kufanya hivyo!Bwana mdogo alikwisha enda hadi USTAWI WA JAMII na kueleza matatizo ya mtoto kwa mama yake yapata miaka miwiliiliyopita na USTAWI walitoa Ushauri ya kuwa mama hana uwezo wa kumzuia mtoto kutoenda kwa baba yake ni suala la makubaliano na mwisho iliamriwa kuwa kwa vile mtoto alikuwa mdogo basi mama akae nae lakini inapofika Ijumaaa mtoto aende kwa baba yake hadi jumapili jioni kisha arudishwe kitu ambacho kilikuwa kinafanyika,ispokuwa toka mtoto aingie darasa la nne Mama amekuwa hataki mtoto aende kwa baba yake na badala yake inapofika Ijumaa huwa anatoa amri arudi kwake na ikifika jioni yeye humchukua na kumpeleka kwa rafiki zake hadi jpili usiku ambako hurudi kwa ajili ya shule jumatatu.
Tatizo tunaloliona ni maandalizi ya hovyo kimasomo kwa hali ya kawaida shule hizi za ENGLISH MEDIUM kama mtoto hasimamiwi vema zinaonekana kuwa ni ngumu kupita kiasi maana mambo mengine yanayo fundishwa mimi nilisoma nikiwa secondary school.
HATA HIVYO tunaangalia ushauri wowote tunaopewa kwa makini sana hasa hawa watu wa USTAWI ambao wametoa maagizo ya kuitwa baba na mama tarehe 16th Mwezi huu waangalie jinsi ya kuweka utaratibu sawa.Nawashukuru na tunasubiri Mawazo yenu.


Kwa nini hukuyaweka haya maelezo kwenye post yako ya kwanza? Kumbe tayari alishakwenda kwa ustawi wa jamii na wakakubaliana? Inaelekea kilichotekea sasa ni mwanamke kuvunja makubaliano. Ila fafanua hapo kwenye red. Kulikuwa na makubaliano kati yao au Ustawi wa jamii walitoa amri? Kama yalikuwa makubaliano ina maana mwanamke ameyavunja. Kama ilikuwa ni amri, then atakuwa amekaidi amri. Tofauti ni kwamba kukaidi amri inaweza kuwa na serious consequences zaidi. Badala ya kwenda kwa wanasheria, aende kwanza ustawi wa jamii hiyo tarehe 16, na aeleze exactly what is going on.
 
Vyovyote iwavyo...huyu mtoto anatakiwa kuendelezwa kielimu ili kumjengea maisha bora baadae...hivyo tafuteni ufumbuzi wa haraka ikiwa ni pamoja na hilo la kisheria ambalo lengo liwe kumsaidia mtoto na si kumkomoa mama yake! Km ulivyoeleza hukuongeza lako basi huyu dada anaweza kua na tatizo la kisaikolojia ambalo linahitaji kufanyiwa kazi!
 
Thanks tunashukuru na tunaendelea fanyia kazi hayo yote,Mawazo yenu yana mchango mkubwa kwa wote BABA,MAMA na MTOTO.
 
Jamani naomba kuuliza,mdogo wangu amezaa na Mwanamke mmoja ambaye hawakuona nae na sasa mtoto ana miaka minane!
Lakini cha ajabu huyu mtoto anavyozidi kuwa na umri mkubwa huyu dada ndo anavyozidi kuwa m_bishi kumruhusu mtoto kuja hata kumsalimia baba yake.
Mtoto anahudumiwa kila kitu ikiwa pamoja na kulipiwa over 1m school fees sasa mama hataki hata baba aangalie madaftari ya mtoto.
Nimemshauri aende kwa wana sheria je kuna ushauri wowote zaidi ya huo niliompa?

Hapo tatizo ni kwamba mtoto akichukuliwa huyo mama ataishi vp? wakati misaada inamiminika kwa ajili ya uwepo wa mtoto.
Kateni mirija ya misaada muone akiwashtaki hapo ndo pakumpatia mtoto.
 
Kuna kizungumkuti hapa.
Unasema mama ana kazi na aliwahi kwenda ulaya. Kwa nini hathamini elimu ya mtoto! kwa nini hathamini afya ya mtoto!
Fanya kila linalowezekana mkapime DNA kwanza.
Je huyo mama ameolewa? Je ana watoto wengine?
Je ni matunzo kiasi gani unatoa kila mwezi?
Majibu yatatupa uelekeo wa namna ya kukusaidia
 
Huyu Mama bado hajaolewa na hana mtoto mwingine,kwa ujumla matunzo ya kawaida kwa mwezi ni kati laki moja hadi laki ishirini achilia mbali
school fees na utilities zingine,kuhusu DNA tunaona haina haja kwa sababu mama mtoto hajawahi sema Mtoto si wa bwana mdogo,halafu bahati
nzuri au mbaya huyu mtoto huwezi uliza baba yake nani kwani ni photocopy ya Babake kabisa,tunashawishika kuwa hakuna shaka hata kidgo kuhusu huyo mtoto na baba yake.
Baba anatabia ya kula kucha-Mtoto naye hivyohivyo;
Baba anatabia ya kupenda sana kula nyanya -Mwana naye ni hivyohivyo
Baba na Mtoto wakikaa ni kama wachina ni copyright kabisa
Kama ikibidi DNA Test baba yuko tayri hata kesho
 
Back
Top Bottom