Sheria inasemaje kuhusu NDOA hivi kuna kuachana jamani?

Sheria inasemaje kuhusu NDOA hivi kuna kuachana jamani?

Apataye mke apata kitu chema, naye ajipatia kibali kwa Bwana... (Mit 19:22). hii itamhusu zaidi huyu aliyeoa 6/7/2013 Arushaone
 
Last edited by a moderator:
sasa hapo nimekupata na nimeelewa vyema, thanks
Ndiyo maana nikaweka alama ya kuuliza nikiashiria kwamba kuachana kunawezekana kabisa kwa sababu hamjapigiliwa misumari licha ya mafundisho au matakwa ya baadhi ya imani za kidini kwamba hakuna kuachana mpaka kifo kiwatenganishe.

Nimeeleweka sasa?
 
Maudhi katika ndoa yanaweza kuwa mazito sana na
ndipo mlalamikaji mume au mke anapokwenda
mahakamani kudai amri ya kuvunja ndoa kabisa
ambayo inaitwa amri ya talaka.
Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inasema ya kuwa
mashauri ya kudai talaka ambavo lazima yatolewe
na mahakama yanapaswa kwanza kupitia kwenye
baraza Ia usuluhishi. Mabaraza ya usuluhishi yapo
mengi na yameundwa kwa shughuli hiyo kwenye
vijiji na mijini. Jukumu Ia mabaraza hayo ni
kuwasuluhisha mlalamikaji na mlalamikiwa ili
waweze kusameheana. Baraza hilo linaposhindwa
kusuluhisha, hawana budi kutoa shahada kwa
mume na mke wanaohusika. Shahada
hiyo itamwezesha mlalamikaji kufungua
madai ya talaka kwenye mahakama. Bila
shahada hiyo madai hayawezi kupokele-
wa mahakamani. Sababu zinazoweza kuf-
anya ndoa ivunjike.
(a) Maasi au utoro wa makusudi
usiopungua miaka mitatu.
(b) Mlalamikiwa kufungwa jela kwa
muda wa miaka mitano mfululizo au
maisha.
(c) Kutengana kwa hiari au kwa amri ya
mahakama kusikopungua miaka
mitatu.
(d) Ukatili wa mwili au akili kwa watoto
wa ndoa au kwa mlalamikaji.
(e) Kichaa kinachothibishwa na
madaktari wawili kwamba hakiponi.
(f) Mlalamikaji kubadili dini ikiwa wote
walikuwa na dini moja wakati wa
kuoana.
Kwa mujibu wa dini hiyo kubadili dini
kunavunja ndoa au kunakuwa na sababu
za kuvunja ndoa

Ahsante Mentor kwa maelezo mafupi ya ufashaa...swali la nyongeza, kwenye kugawana mali zilizochumwa mikiwa kwenye ndoa, mgawanyo ukoje/ hasa inapokuwa mume ndio 'main bread winner' bila mchango wowote toka kwa mke, japo naye ana kazi na/au biashara ndogo ndogo.
 
lakini kwanini vijana wa siku hizi mnang'ang'ania kuachana na kutoa talaka ovyo bila sababu yoyote kwani hujua kuwa nyote mmetoka kwenye familia tofauti na tabia ni tofauti kabisa, ni vyema ukajifunza kwa wenzao na kumvumilia kwa mapungufu yake kuliko kukimbilia kuachana ambako hakuna faida wala msingi wowote cc😡Mtambuzi
 
haya bhana kama una msamaha kwa mwenzi wako unamatatizo kabisa tutaona kwa marejesho kama utafanya hivyo
Hii wala haihitaji kusoma Waorintho wala Wafilipi!

We jua tu kwamba ukifumaniwa unaachwa!
 
Last edited by a moderator:
Mimi napenda sana sheria za talaka kwenye baadhi ya nchi za Ulaya na Marekani - no-fault divorce.

Mtu huhitaji kuwa hata na sababu (kama ugoni au kutendewa mabaya). Unachohitaji kusema kwenye petition yako ni kwamba ndoa yenu ipo irretrievably broken au mna irreconcilable differences na kama respondent hana pingamizi, ndoa inakuwa dissolved. Na kama mnakubaliana mnaweza hata ku-waive ile 90-day cooling off period na kuharakisha mambo ndani ya siku 30 tu na kila mtu anakuwa huru.
 
Kuachana kupo hila inategemea unatumia njia hipi kutafuta kuachnana, kama unatumia njia ya kwenda kwa padri/mchungaji sahau kuhusu kuachna maana hawa hawakubali kuachana na wakotayari kutumia miaka hata miwili kutafuta suluhu ili mradi ndoa isivunjwe.

Lakini kama utatumia njia ya serikali hasa kwenye mabaraza ya usuluhishi na ikaonekana hiyo ndoa imashindikana kurudishwa basi mnaachanishwa kabisa, lakini mpaka ithibitike imeshindikana kusuluhisha na kuna sababu za msingi za kuvunja ndoa.

Na kuhusu mali mlizo chuma pamoja lazima mtagawana, lakini kama hamkuchuma pamoja hamtogawana bali itabaki kuwa haki ya yule aliyechuma.
 
Ahsante Mentor kwa maelezo mafupi ya ufashaa...swali la nyongeza, kwenye kugawana mali zilizochumwa mikiwa kwenye ndoa, mgawanyo ukoje/ hasa inapokuwa mume ndio 'main bread winner' bila mchango wowote toka kwa mke, japo naye ana kazi na/au biashara ndogo ndogo.

Mali zina gawiwakulingana na mchnago wa mtu kwenye mali husika. kama huna mchango kwenye mali husika basi siyo haki yako. lakini kama ulimnunulia gari mkeo na ukampa kama zawadi hiyo itabaki ni mali yake.
 
Refer case ya malekh sultan v.sheraj jeraj uisome vizuri utaelewa procedures na uhalali wa talaq
 
Mali zina gawiwakulingana na mchnago wa mtu kwenye mali husika. kama huna mchango kwenye mali husika basi siyo haki yako. lakini kama ulimnunulia gari mkeo na ukampa kama zawadi hiyo itabaki ni mali yake.

Katika hali hiyo..mchango wa mke (hasiye bread winner kabisa) kwa utunzaji wa familia unafidiwaje kisheria? Na inakuwaje kisheria iwapo maisha yenu yote mliyoishi kwenye ndoa mlikuwa na msaidizi wa nyumbani (housegirl) ambaye ndo alifanya kazi za nyumbani badala mke, na huyo msaidizi analipwa na baba kama bread winner?
 
Back
Top Bottom