Sheria za Soka za FIFA: Ifahamu sheria namba tatu ya FIFA inayohusu idadi ya Wachezaji Uwanjani

Sheria za Soka za FIFA: Ifahamu sheria namba tatu ya FIFA inayohusu idadi ya Wachezaji Uwanjani

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Kwa mujibu wa Sheria za FIFA (Shirikisho la Soka Duniani) mwaka 2015/16, mechi inachezwa na timu mbili, kila moja ikiwa na Wachezaji wasiozidi 11, mmoja wao ni Kipa. Mechi haiwezi kuanza ikiwa timu yoyote ina Wachezaji chini ya 7

Kiwango cha juu cha kubadili Wachezaji wakati wa mechi kwenye mashindano rasmi yaliyoandaliwa na FIFA au Wanachama wake ni Wachezaji watatu. Kanuni za shindano husika zitaeleza wachezaji wangapi wakae benchi kuanzia 3 hadi 12

photo_2020-03-11_16-21-25.jpg

Kwenye mashindano mengine (Kitaifa) hadi Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa lakini kwenye mashindano mengine Wachezaji zaidi wanaweza kubadilishwa

Katika mashindano ambayo zaidi ya Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa, timu lazima zikubaliane na Mwamuzi wa mchezo aambiwe. Hayao yasipofanyika Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa

Kurudishwa Uwanjani kwa mchezaji aliyefanyiwa mabadiliko kunaruhusiwa tu kwenye mashindano ya viwango vya chini au mashindano kwa ajili tu ya burudani lakini lazima wanaohusika wakubaliane

Mchezaji yeyote anaweza kubadilishana nafasi na Golikipa ilimradi tu, Mwamuzi apewe taarifa kabla na ubadilishanaji huko kufanyika mpira ukiwa umesimama

Mchezaji aliyepewa kadi nyekundu kabla ya mpira kuanza, nafasi yake inaweza kuchukuliwa na mchezaji yeyote aliye benchi ila haiwezekani mchezaji mwingine kuingia ikiwa mchezaji atapeka kadi nyekundu mchezo ukiwa umeanza


Pia unaweza kusoma Sheria za Soka za FIFA: Ifahamu Sheria namba Mbili ya FIFA inayohusu Mpira wa Soka
 
Thank you
Kwa mujibu wa Sheria za FIFA (Shirikisho la Soka Duniani) mwaka 2015/16, mechi inachezwa na timu mbili, kila moja ikiwa na Wachezaji wasiozidi 11, mmoja wao ni Kipa. Mechi haiwezi kuanza ikiwa timu yoyote ina Wachezaji chini ya 7

Kiwango cha juu cha kubadili Wachezaji wakati wa mechi kwenye mashindano rasmi yaliyoandaliwa na FIFA au Wanachama wake ni Wachezaji watatu. Kanuni za shindano husika zitaeleza wachezaji wangapi wakae benchi kuanzia 3 hadi 12


Kwenye mashindano mengine (Kitaifa) hadi Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa lakini kwenye mashindano mengine Wachezaji zaidi wanaweza kubadilishwa

Katika mashindano ambayo zaidi ya Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa, timu lazima zikubaliane na Mwamuzi wa mchezo aambiwe. Hayao yasipofanyika Wachezaji 6 wanaweza kubadilishwa

Kurudishwa Uwanjani kwa mchezaji aliyefanyiwa mabadiliko kunaruhusiwa tu kwenye mashindano ya viwango vya chini au mashindano kwa ajili tu ya burudani lakini lazima wanaohusika wakubaliane

Mchezaji yeyote anaweza kubadilishana nafasi na Golikipa ilimradi tu, Mwamuzi apewe taarifa kabla na ubadilishanaji huko kufanyika mpira ukiwa umesimama

Mchezaji aliyepewa kadi nyekundu kabla ya mpira kuanza, nafasi yake inaweza kuchukuliwa na mchezaji yeyote aliye benchi ila haiwezekani mchezaji mwingine kuingia ikiwa mchezaji atapeka kadi nyekundu mchezo ukiwa umeanza


Pia unaweza kusoma Sheria za Soka za FIFA: Ifahamu Sheria namba Mbili ya FIFA inayohusu Mpira wa Soka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna sheria ngumu kama ile ya OFFSIDE....tuelezee kidogo kocha
 
Back
Top Bottom