Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sheria zote Nchini kuwa kwa Kiswahili
![]()
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome amesema kuanzia sasa sheria zote zitakazotungwa nchini zitakuwa katika lugha ya Kiswahili ili kuwawezesha wananchi wengi ambao ndio walengwa wa sheria hizo, kuzielewa.
Uamuzi huo unakwenda sambamba na kuzitafsiri sheria zote zinazotumika nchini ambazo ziko katika lugha ya Kiingereza ili kutimiza lengo hilo la kuwafanya wananchi wengi wazielewe.
“Kwa sasa serikali imeamua kuwa sheria zote nchini zitakuwa katika lugha ya Kiswahili na zile ambazo ziko katika lugha ya Kiingereza zitatafsiriwa ili kuwawezesha Watanzania wengi ambao ndio walengwa wa sheria hizo kuzielewa,” alisema.
Pia alisema serikali itazifanyia marekebisho sheria zote ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na wadau mbalimbali kuwa hazikidhi mahitaji au haja, haziendani na wakati uliopo sasa ili kutekeleza azma yake ya kuwahudumia wananchi wake kwa ukamilifu.
Profesa Mchome ameyasema hayo jijini Dar es Salaam jana baada ya kupokea mapendekezo yaliyowasilishwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WILDAF), ambayo yanataka kufutwa kwa sheria mbalimbali za kimila zinazosimamia masuala ya mirathi ambazo zinalalamikiwa kuwakandamiza wanawake nchini.
Profesa Mchome amewashukuru WILDAF kwa kazi waliyoifanya na kuwaahidi kuwa wataalamu wake wizarani watayafanyia kazi mapendekezo yao ili kuhakikisha gurudumu la sheria nchini linasonga mbele na kuwasaidia wananchi wengi.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkurugenzi wa WILDAF, Judith Odunga alisema mapendekezo hayo yanataka kufutwa kwa sheria za kimila ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiwakandamiza wanawake, kuwanyima haki ya kumiliki mali na kufanyiwa vitendo vya kidhalilishaji pale wanapofiwa na waume zao.
Alisema katika mapendekezo hayo WILDAF inaiomba serikali itunge sheria moja ambayo pamoja na zile za kidini itashughulikia masuala ya mirathi na kuweka usawa wa kisheria katika urithi wa mali kati ya mwanamke na mwanamume, ikiwa ni pamoja na watoto wa kiume na wa kike kuwa na usawa katika kurithi mali inapotokea mzazi wa kiume amefariki dunia.
My Take
Ni jambo la kupongezwa.
kuielewa sheria ni zaidi ya lughaSheria zote Nchini kuwa kwa Kiswahili
![]()
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome amesema kuanzia sasa sheria zote zitakazotungwa nchini zitakuwa katika lugha ya Kiswahili ili kuwawezesha wananchi wengi ambao ndio walengwa wa sheria hizo, kuzielewa.
Uamuzi huo unakwenda sambamba na kuzitafsiri sheria zote zinazotumika nchini ambazo ziko katika lugha ya Kiingereza ili kutimiza lengo hilo la kuwafanya wananchi wengi wazielewe.
“Kwa sasa serikali imeamua kuwa sheria zote nchini zitakuwa katika lugha ya Kiswahili na zile ambazo ziko katika lugha ya Kiingereza zitatafsiriwa ili kuwawezesha Watanzania wengi ambao ndio walengwa wa sheria hizo kuzielewa,” alisema.
Pia alisema serikali itazifanyia marekebisho sheria zote ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na wadau mbalimbali kuwa hazikidhi mahitaji au haja, haziendani na wakati uliopo sasa ili kutekeleza azma yake ya kuwahudumia wananchi wake kwa ukamilifu.
Profesa Mchome ameyasema hayo jijini Dar es Salaam jana baada ya kupokea mapendekezo yaliyowasilishwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WILDAF), ambayo yanataka kufutwa kwa sheria mbalimbali za kimila zinazosimamia masuala ya mirathi ambazo zinalalamikiwa kuwakandamiza wanawake nchini.
Profesa Mchome amewashukuru WILDAF kwa kazi waliyoifanya na kuwaahidi kuwa wataalamu wake wizarani watayafanyia kazi mapendekezo yao ili kuhakikisha gurudumu la sheria nchini linasonga mbele na kuwasaidia wananchi wengi.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkurugenzi wa WILDAF, Judith Odunga alisema mapendekezo hayo yanataka kufutwa kwa sheria za kimila ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiwakandamiza wanawake, kuwanyima haki ya kumiliki mali na kufanyiwa vitendo vya kidhalilishaji pale wanapofiwa na waume zao.
Alisema katika mapendekezo hayo WILDAF inaiomba serikali itunge sheria moja ambayo pamoja na zile za kidini itashughulikia masuala ya mirathi na kuweka usawa wa kisheria katika urithi wa mali kati ya mwanamke na mwanamume, ikiwa ni pamoja na watoto wa kiume na wa kike kuwa na usawa katika kurithi mali inapotokea mzazi wa kiume amefariki dunia.
My Take
Ni jambo la kupongezwa.
Nami nilitokea kutokumkubali kabisa huyu Prof kipindi kile yuko Elimu kwa kuweza kuidhalilisha taaluma yake bila aibu. Lakini Kwa hili naona yuko sahihi na anastahili pongeziNimewahi kukutana na Prof huyu katika forums tofauti, lakini niseme tu sijawahi kuona "competence" yake na hasa kwenye masuala ya kiuongozi. Huwa anatumia majibu rahisi kujibu maswali magumu. Alipokuwa Katibu Mkuu wa Elimu, aliposhindwa kuifanya elimu iwe shindani na kuzalisha vijana wenye uwezo, na wanaoweza kupasi mitihani, solution alioiona ni kubadilidha mfumo wa alama na kupunguza pass mark pamoja na GPA system. Badala ya kujibu swali gumu kwanini watanzania walio wengi wamashindwa kuielewa lugha ya kiingereza na hivyo kunufaika na fursa za lugha hiyo duniani ikiwa pamoja na kujua sheria zilizoandikwa kiingereza, amekuja na majibu rahisi tena ya kubadilisha lugha iliyotumika kuandika sheria. Sasa nasubiri, je watakapoziandika kwa lugha ya kiswahili na kisha kubaini watu wengi wanaelewa zaidi zikiwa kwenye lugha zao za kimakabila, sijui atakuja na mkakati wa kuziandika sheria katika lugha za kimakabila?
Nchi zote za kiafrika zinatumia Lugha tatu tu katika masuala yao makubwa (ama kuendesha Serikali au mfumo wa Elimu). Bahati nzuri Lugha zote hizo tatu ni za Kimataifa (English, French and Arabic). Si kwamba hawana lugha zao za ndani, bali wamebaini lugha zao si shindani hivyo zitawatoa katika ulingo wa kimataifa. Unfortunately, nchi yetu ndio inataka kuelekea huko. Tunakipenda sana kiswahili, na ni fahari, lakini hakina utayari wa kuipeleka nchi katika Uchumi wa kati. Tukomae kwenye kujua kiingereza kina nafasi sana katika dunia ya leo kuliko kiswahili. Tusidanganyane jamani.

Hivi wanao somea. Uinjinia wa maji kwan wanasoma kwa kiswahil? Au kazi haiend? Umeuliza Swali la kujinga sanaNa mahakamani, patakua je, hukumu zitaandikwa kwa kiswahili au?
Vipi kuhusu wanafunzi wanaosomea sheria, mitihani itakua kwa kiswahili pia?
Ukiwa na "akili za kijinga" lazima uone maswali niliyouliza ni ya "kijinga".Hivi wanao somea. Uinjinia wa maji kwan wanasoma kwa kiswahil? Au kazi haiend? Umeuliza Swali la kujinga sana
Acha uongoNimewahi kukutana na Prof huyu katika forums tofauti, lakini niseme tu sijawahi kuona "competence" yake na hasa kwenye masuala ya kiuongozi. Huwa anatumia majibu rahisi kujibu maswali magumu. Alipokuwa Katibu Mkuu wa Elimu, aliposhindwa kuifanya elimu iwe shindani na kuzalisha vijana wenye uwezo, na wanaoweza kupasi mitihani, solution alioiona ni kubadilidha mfumo wa alama na kupunguza pass mark pamoja na GPA system. Badala ya kujibu swali gumu kwanini watanzania walio wengi wamashindwa kuielewa lugha ya kiingereza na hivyo kunufaika na fursa za lugha hiyo duniani ikiwa pamoja na kujua sheria zilizoandikwa kiingereza, amekuja na majibu rahisi tena ya kubadilisha lugha iliyotumika kuandika sheria. Sasa nasubiri, je watakapoziandika kwa lugha ya kiswahili na kisha kubaini watu wengi wanaelewa zaidi zikiwa kwenye lugha zao za kimakabila, sijui atakuja na mkakati wa kuziandika sheria katika lugha za kimakabila?
Nchi zote za kiafrika zinatumia Lugha tatu tu katika masuala yao makubwa (ama kuendesha Serikali au mfumo wa Elimu). Bahati nzuri Lugha zote hizo tatu ni za Kimataifa (English, French and Arabic). Si kwamba hawana lugha zao za ndani, bali wamebaini lugha zao si shindani hivyo zitawatoa katika ulingo wa kimataifa. Unfortunately, nchi yetu ndio inataka kuelekea huko. Tunakipenda sana kiswahili, na ni fahari, lakini hakina utayari wa kuipeleka nchi katika Uchumi wa kati. Tukomae kwenye kujua kiingereza kina nafasi sana katika dunia ya leo kuliko kiswahili. Tusidanganyane jamani.
Alisema katika mapendekezo hayo WILDAF inaiomba serikali itunge sheria moja ambayo pamoja na zile za kidini itashughulikia masuala ya mirathi na kuweka usawa wa kisheria katika urithi wa mali kati ya mwanamke na mwanamume, ikiwa ni pamoja na watoto wa kiume na wa kike kuwa na usawa katika kurithi mali inapotokea mzazi wa kiume amefariki dunia.
Au mlitaka muendelee kunyanyasa watu kwa kizungu kwanza sio lugha yetu mnaobeza sijui wa wapiUkiwa na "akili za kijinga" lazima uone maswali niliyouliza ni ya "kijinga".
Jaribu kujibu maswali yangu ili tuelewane, sio kusoma kitu juu juu.
Dhumuni la Professor, amedai kutafsiri sheria za Tanzania kwa kiswahili ni ili watu wazielewe, kuna member moja humu kauliza Swali zuri sana, kwamba mbona Katiba ipo katika Lugha ya kiswahili lakini bado baadhi ya Raia hawajui katiba yenyewe, wengine pamoja na usomi wao wote wa PhD bado wanaisigina na kuivunja, huku wengine walioapa kuilinda ndio wamekuwa wakanza kuivunja, sasa hapa tujiulize mimi na wewe tatizo lipo wapi?
Na Mwisho nikukumbushe kutokana na muundo wa katiba yetu bado watakao baki na mamlaka ya mwisho ya kutafsiri sheria nchini ni Mahakama pekee.
Nimeuliza Swali kwa mfano, kama lengo na Dhumuni la profesa Mchome ni kufanya sheria husika watu wazijue, je itailazimu na mahakama iandike hukumu zake kwa kiswahili ili lengo la profesa litimie? Na je kuna umuhimu gani wa kutafsiri (translate) sheria husika ikiwa ili hali bado hukumu zitakazo tolewa na mahakama bado zitabaki kwenye lugha ya kiingereza?
Hapa naomba na wewe unijibu nione "akili" zako zilipopo ishia.