Shetta: Sina mpango wa kufanya kazi na Ali Kiba

Shetta: Sina mpango wa kufanya kazi na Ali Kiba

Mimi huyu shettah sielewi anaimba nini zaidi ya kusikia tu kwenye nyimbo zake akisema... Shedah da shedah da shedah..
 
Mashabiki wa Kiba siku hizi wamekuwa kama mashabiki wa UKAWA kule jukwaa la siasa...

Nimesoma majibu yake hata mimi sijaona kosa lake.. Kajibu alichoulizwa basi jibu lake watu wameshalipindua.
Jamani nawashauri wasanii wengine wakiulizwa kama wana mpango wakufanya collabo na Kiba wawe wanajibu ndiyo hata kama hawana maana wakijibu hapana wataanza semwa kuwa wana dharau.
Kwenye my play list ya clouds Rich Mavoko aliulizwa kati ya Kiba na Diamond angependa fanya collabo na nani, akajibu Diamond sijui watu hawakusikia maana nilidhani naye atashambuliwa.
 
mimi nimemmind muulizaji, alafu mbona kuna wimbo sheta kafanya na kiba na sijui nani yule tena mzuri tu misago ye anataka nini tena??

Unaitwa Basi uje Kariakoo...wimbo wa Abby Skills!!
 
Kwani huyo kiba siku hizi kawa mlemavu? Yaani eti kila mtu lazima awe upande wake!!! Ukiwa na mawazo tofauti naye basi wajiwa juu!! Mbona wanampa huruma asizohitaji huyu kiba? Anaonewa huruma kama mlemavu wa ngozi hahaaa! Kiba kataa kuwa na mashabiki wasiotaka upate challenges! Kimbia kabisaaa!

Wacha kiba apendwe ww coz hana mpinzani kwa ss
 
Kwanza hicho kisanii nakijua jina tu, hakuna hata nyimbo yake moja ambayo naijua.
Kitakuwa kimerogwa, si bure.
Ina maana hakijui kama Ali ni wa intaneshino na alifanya kazi na akina R Kelly!
 
@elmagnifico

Tatizo la mashabiki wa KIba wana inferiority complex... yaani hapo wanaona ni kama Shetta kam-dis Kiba wakati amejibu alichoulizwa... namuunga mkono Paula kilaki, Misago kauliza swali la kich'oko kwavile tu anafahamu Shetta na Diamond wapo karibu... swali la Misago ni kama ambavyo Sporah alivyokuwa anamlazimisha Ally K ajibu maswali kuhusu Diamond wakati Kiba alionesha wazi kwamba hakuwa interested!

But all in all, hawa mashabiki ndio wanaokuza zaidi haya mambo... trust me, kama kuna bifu basi bifu la Ally K lilikuwa linaelekea ukiongoni lakini kidonda kikajakutiwa chumvi kwenye Fiesta... wenyewe wanadhani wanadhani wanamsaidia Kiba kumbe wanamuhariabia... wote hawa wala si wadau wa muziki bali wapiga kelele za majukwaani na kwenye social networks... hawana msaada hawa!

Kama wapiga kelele wangekuwa na msaada wangeanza kuwa na msaada wapiga kelele wa Wanaume Halisi! Watu walidhani ku-shine kwa Wanaume Halisi kulitokana solely na Juma Nature... yes, Juma Nature alikuwa na nyota sana ya kupendwa lakini sie ambao tulikuwa hatukauki pale maskani ya TMK tulifahamu pale TMK ilipokuwa kulichangiwa zaidi na Said Fella simply because Saidi Fella anazijua A-Z fitina za muziki wa kibongo!

Mtu wa kwanza kujitoa TMK alikuwa Kakaman... cku Kakaman anapeleka album yake ya kwanza sokoni akiwa sole artist, nilikuwa nae pamoja na mchizi fulani hivi! Hadi leo cjapata jibu la moja kwa moja kwanini ile album ilishindwa ku-shine wakati ilikuwa na pini zilizoenda shule!

Anyway, enzi zile nilikuwa naingia jijini kwa ku-beep lakini nilipofuatilia nikaambiwa Saidi Fella alipita kote tulikokuwa tumepita... sina ushahidi katika hili! Wakati naondoka Dar, nikawaeleza washikaji kwamba Wanaume naipa miezi sita kabla haijasambaratika... na kweli hata miezi mitatu haikuisha Wanaume Halisi ikaanzishwa na kupata bonge la back-up la mashabiki!

Ambao tulihudhuria show ya Wanaume Halisi vs Family bado tunakumbuka nini kiliwakumba Wanaume Family lakini kama nilivyosema hapo awali, mashabiki wapiga kelele hawana msaada kwa msanii! Pamoja na back up yote hiyo ya mashabiki, Wanaume Halisi ambao kimsingi ndio kambi yangu (ingawaje nili-refrain kuchukua side) wamepotezea wazima wazima!

Si kwamba hakuna vipaji... Nature ndie yule yule wa miaka yote lakini walichobaki nacho ni mashabiki wapiga kelele wasio na msaada wa moja kwa moja huku wakikosa wadau wanaofahamu fitina za muziki wa kibongo!

Kama mtu ni mfuatiliaji wa muziki kwenye redio na matamasha wala hawezi kunielewa lakini kama ni inside guy, atanielewa...
 
Hahahaaaa hii dunia ina vituko yaani shetta nae anazuga yuko juu kiasi cha kujifananisha na alikiba? Sasa shetta anafanya nini kikubwa mpaka adhani alikiba anahitaji kufanya nae collabo! Shetta hajawahi kuimba wimbo wake mwenyewe anapenda kubebwa tu
 
mi nakereka sana watanzania wanapenda kuchonganisha wasamii kwenye social networks. mi huwa naangalia mambo watu wayoandika kuhusu alikiba na ' domo' nashangaa sana kuna watu wanataman hata wapigane, hata waanahabari jinsi tu wanavyo wahoji unajua ni unafiki na uchonganishi
 
Hahahaaaa hii dunia ina vituko yaani shetta nae anazuga yuko juu kiasi cha kujifananisha na alikiba? Sasa shetta anafanya nini kikubwa mpaka adhani alikiba anahitaji kufanya nae collabo! Shetta hajawahi kuimba wimbo wake mwenyewe anapenda kubebwa tu
Nyie watu kwa kupindisha maneno hamjambo... wapi katika hayo maelezo Shetta amejiona yupo juu na kujifananisha na Ali Kiba? Wapi amesema Ali Kiba anahitaji kufanya kolabo na Shetta?
 
sheta anatembelea nyota za watu
anategemea collabo ndo ahit
kuthibisha hilo ndo mana hajawàh toa wimbo km solo artist

wimbo wake wa kwanza "tunaplay" aliimba mwenyewe, mwisho wa siku aliishia kuusikiliza gheto mwenyewe mana ulibuma.
 
mi nakereka sana watanzania wanapenda kuchonganisha wasamii kwenye social networks. mi huwa naangalia mambo watu wayoandika kuhusu alikiba na ' domo' nashangaa sana kuna watu wanataman hata wapigane, hata waanahabari jinsi tu wanavyo wahoji unajua ni unafiki na uchonganishi
Tena wanavyopenda kukopa bifu basi... mbaya zaidi wengine wanadhani wapo karibu zaidi na hao wasanii kuliko walivyo karibu wasanii kwa wasanii wenyewe! Halafu hawa wasanii wengi wao ni dugu moja kutoka Kigoma... wengine wanaoshabikia bifu utashangaa kuona ni Wapogoro kutoka Mtimbila na Malinyi na wengine Wandendeule kutoka Namtumbo... sasa cjui hawataona aibu cku wenyewe wakishapatana!! Waswahili walipata kusema: "ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime!" Team Wema walijifanya kumtolea uvivu Diamond matokeo yake wakajikuta wanashuhuliwa wenyewe na huyo huyo waliekuwa wanampigania!
 
Back
Top Bottom