Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Napiga hodi watani, wa kijiji naingia,
Ngojea niketi chini, swali kuwaulizia,
Nilonalo mtimani, beti ninalitungia,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Ni ndege niliyemwinda, asubuhi na jioni,
Ndege mwenyewe si kinda, nilipomuona mtini,
Na ndipo nilimpenda, nikatamani moyoni,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Mtego nikauweka, na punje nikamwagia,
Ndege pweke akaruka, mtegoni kashukia,
Mara puh! Kanasika, Miguu kajifungia,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Ndipo nikafanya hima, kukimbilia nyumbani,
Kumtaarifu mama, ndege yuko mtegoni,
Kwamba ninaleta nyama, ya chakula cha jioni,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Mama kanipa pongezi, mwanangu sasa kakua,
Yakamtoka machozi, na kicheko cha kishua,
Mwenyewe nikala pozi, huku nikijishaua,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Baba kaniangalia, kaniona mimi chizi,
Ndipo kaniulizia, huyo ndege wa ulozi,
Mtego nimeachia, ni nani wangu mlinzi,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Kwa haraka nikatoka, kumuwahi ndege wangu,
Mara pale nikafika, nikapatwa na uchungu,
Mtego umevunjika, au umepigwa rungu!
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Mwili ukatetemeka, hasira zikanishika,
Nilidhani nimefika, kumbe nimekamatika,
Na ndipo nikaondoka, na kichwa nimekishika,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Nilipokuwa njiani, nikamwona Shaabani,
Ana ndege mkononi, ni yule nilotamani,
Kamkuta kichakani, ndege yuko taabani,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Sijui nifanye nini, nimpate ndege wangu,
Shaabani haniamini, huyo ndege ndiye wangu,
Ananicheka kihuni, wa kwake siye wa kwangu,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Ngojea niketi chini, swali kuwaulizia,
Nilonalo mtimani, beti ninalitungia,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Ni ndege niliyemwinda, asubuhi na jioni,
Ndege mwenyewe si kinda, nilipomuona mtini,
Na ndipo nilimpenda, nikatamani moyoni,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Mtego nikauweka, na punje nikamwagia,
Ndege pweke akaruka, mtegoni kashukia,
Mara puh! Kanasika, Miguu kajifungia,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Ndipo nikafanya hima, kukimbilia nyumbani,
Kumtaarifu mama, ndege yuko mtegoni,
Kwamba ninaleta nyama, ya chakula cha jioni,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka
Mama kanipa pongezi, mwanangu sasa kakua,
Yakamtoka machozi, na kicheko cha kishua,
Mwenyewe nikala pozi, huku nikijishaua,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Baba kaniangalia, kaniona mimi chizi,
Ndipo kaniulizia, huyo ndege wa ulozi,
Mtego nimeachia, ni nani wangu mlinzi,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Kwa haraka nikatoka, kumuwahi ndege wangu,
Mara pale nikafika, nikapatwa na uchungu,
Mtego umevunjika, au umepigwa rungu!
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Mwili ukatetemeka, hasira zikanishika,
Nilidhani nimefika, kumbe nimekamatika,
Na ndipo nikaondoka, na kichwa nimekishika,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Nilipokuwa njiani, nikamwona Shaabani,
Ana ndege mkononi, ni yule nilotamani,
Kamkuta kichakani, ndege yuko taabani,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka.
Sijui nifanye nini, nimpate ndege wangu,
Shaabani haniamini, huyo ndege ndiye wangu,
Ananicheka kihuni, wa kwake siye wa kwangu,
Ndege niliyemnasa, mtegoni katoweka!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)