Shida ni akili ndogo za madereva au ni maisha magumu yanachangia hizi ajari

Shida ni akili ndogo za madereva au ni maisha magumu yanachangia hizi ajari

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Leo asubuhi nikiwa njiani nimeona ajali Moja eneo la ilula na nikiwa nimetulia napitia mitandao nimekutana na picha za ajali Ile. Ukiangalia Ile ajali Ile fuso ilikuwa imeharibika , na jamaa wa fuso walikuwa waungwana wameweka alama zote muhimu barabarani kujua huko mbele unaenda kukutana na nini, Cha ajabu dereva wa IT pamoja na alama.zote zile kalivaa Lori na matokeo yake yamekuwa magumu, ule muda tuliokuwa kwenye Lori mimi, dereva na tingo tumejadili hadi tumechoka nini kimefanya yule mwenye IT akalivamie Lori, wakati tunajadiliana na sisi tumekoswa tena na gari ndogo ya abiria amekwangua bodi, na gAri imeharibika kidogo mwenye gari inabidi atupie Milion kama Moja kwenye lile coaster ,unamuliza dereva wa coaster imekuwaje asubuhi unahama anakwambia , biashara ngumu , unamuliza kwa kukimbia hovyo hovyo ndio kunapunguza ugumu wa biashara hana majibu. Kuna shida gani kwenye akili za driver maisha magumu yanachangia au hawana tu akili ,.nashukuru Nina miaka sasa sina gari iliyojitupa kwa ujinga wa dereva, nini kifanyike kwa udereva huu wa sasa ambao unafanya barabarani kutishe , siku hizi inatisha sana unakopa, unaweka pesa kwenye gari halafu unaanza kuishi kwa hofu na kuogopa kuw huenda usimalize mkopo na gari usiwe nayo
 

Attachments

  • 1721393576396.jpg
    1721393576396.jpg
    373.2 KB · Views: 8
Leo asubuhi nikiwa njiani nimeona ajali Moja eneo la ilula na nikiwa nimetulia napitia mitandao nimekutana na picha za ajali Ile. Ukiangalia Ile ajali Ile fuso ilikuwa imeharibika , na jamaa wa fuso walikuwa waungwana wameweka alama zote muhimu barabarani kujua huko mbele unaenda kukutana na nini, Cha ajabu dereva wa IT pamoja na alama.zote zile kalivaa Lori na matokeo yake yamekuwa magumu, ule muda tuliokuwa kwenye Lori mimi, dereva na tingo tumejadili hadi tumechoka nini kimefanya yule mwenye IT akalivamie Lori, wakati tunajadiliana na sisi tumekoswa tena na gari ndogo ya abiria amekwangua bodi, na gAri imeharibika kidogo mwenye gari inabidi atupie Milion kama Moja kwenye lile coaster ,unamuliza dereva wa coaster imekuwaje asubuhi unahama anakwambia , biashara ngumu , unamuliza kwa kukimbia hovyo hovyo ndio kunapunguza ugumu wa biashara hana majibu. Kuna shida gani kwenye akili za driver maisha magumu yanachangia au hawana tu akili ,.nashukuru Nina miaka sasa sina gari iliyojitupa kwa ujinga wa dereva, nini kifanyike kwa udereva huu wa sasa ambao unafanya barabarani kutishe , siku hizi inatisha sana unakopa, unaweka pesa kwenye gari halafu unaanza kuishi kwa hofu na kuogopa kuw huenda usimalize mkopo na gari usiwe nayo
Hakuna high way yoyote ina single lane Karne hii ya 21,ni ujinga tuu kwa gari eti upishane na mtu mita tano tano ni wehu mkubwa.Tutaendelea kutumika,jingine ni usingizi na fatigue kwa ITs hawataki kuweka pembeni wapumue kidogo
kidogo au health break hawataki,sasa nini hapo?
 
Dereva wa IT alikua kachoka na usingizi hakuna kingine kustuka gari hili akiwa kwenye ndoto bara barani na hawataki kupumzika wao wanaweka malengo lazima afike sehemu fulani hata kama akili imechoka..
 
Hivi ajali ni miongoni mwa vitu vinavyoangukia kwenye mipango ya mungu kwa maana unaweza kuchukua tahadhari zote na still ukapata ajali
 
Hakuna high way yoyote ina single lane Karne hii ya 21,ni ujinga tuu kwa gari eti upishane na mtu mita tano tano ni wehu mkubwa.Tutaendelea kutumika,jingine ni usingizi na fatigue kwa ITs hawataki kuweka pembeni wapumue kidogo
kidogo au health break hawataki,sasa nini hapo?
Dereva wa IT anatoka Dar saa 12 jioni anafika Kasumulu Kyela saa tatu asubuhi anaiacha gari boda anarudi Dar kwa kupanda Costa mpaka Uyole Mbeya anapanda gari yoyote kurudi Dar, anafika usiku asubuhi anakwenda bandarini kuchukua gari na jioni safari ya kwenda Kyela, pesa wanazolipwa si nyingi ila jitahidi upate safari nyingi.
 
Back
Top Bottom