Shinyanga, Buyubi: Watu 3 wadaiwa kufariki dunia kwa ajali ya basi, 34 wajeruhiwa

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Watu 3 wanadaiwa kufariki na wengine 34 wakijeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Classic lililokuwa likitokea Kampala kuelekea Dar kupata ajali eneo la Buyubi Shinyanga.

Baadhi ya majeruhi kwenye ajali hiyo wamesema kuwa dereva wa basi hilo alishindwa kuimudu kona ya Didia.


Watu watatu wanahofiwa kufa katika ajali ya basi la Classic eneo la Buyubi Kata ya Didia mkoani Shinyanga, huku wengine 34 wakijeruhiwa baada ya basi hilo kuacha njia na kupinduka majira ya saa 10:00 alfajiri ya Juni 2, 2021, wakati likitokea Kampala Uganda kuelekea Dar es Salaam.

Basi la kampuni ya Classic lililopata ajali
Baadhi ya majeruhi wa ajili hao wamesema kuwa ajali hiyo imetokea baada ya dereva wa basi hilo kushindwa kukata kona katika barabara ya Shinyanga Kahama na kwamba mara baada ya ajali hiyo dereva alikimbia.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa wilaya ya Shinyanga John Kafumu, amefika eneo la tukio na kueleza kuwa taarifa zaidi kuhusiana na ajali hiyo zitatolewa na Kamanda wa Polisi mkoa Debora Magiligimba.
 
Dereva kashindwa kuimudu kona....inawezekana kona ilitokea ghafla! RIP
Sababu ya speed! Au kama labda ni mgeni pia....lakini nawaza kwa speed 80 basi lisingeanguka
 
Napajua hapo Didia.
Kwa mbele kidogo tulikuaga na Petrol Station. Pale mkabala na Jumbo Oil Mills.
Mzee alipofariki niliamua kupauza, tukafungua biashara ya kuuza vifaa vya ujenzi na demu wangu.
Alikuja kunitapeli yeye na hawara yake, basi tukaachana. Nikabaki masikini hadi leo.
 

Stori imepitiliza kuhusu ajali
 
Mungu ajalie uponyaji majeruhi.
 
R.i.p mlotangulia, Mwenyezi Mungu nakuomba uwajarie majeruhi wapone mapema.
 
Pole, story yako fupi ila inasikitisha sana
 
hii ni dhambi ya kuuza urithi
 
Aseeee

Pole yako ,
 
Ni wanafunzi. Wengi from Zanzibar

Allah Awaraham Waliotangulia mbele ya haq. Na Awajalie uponaji wa haraka majeruhi. Ameen Ameen.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…