RWANDES
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 1,788
- 4,401
Naibu waziri Katambi amefanya ziara katika Machinjio ya kisasa ya ng’ombe yaliyopo katika kata ya Ndembezi na kuonesha kutoridhishwa na ujenzi wa machinjio hayo yenye gharama ya Shilingi Bilioni 5.57 ulioanza mwaka 2018 ukitarajiwa kukamilika mwaka 2019 lakini mpaka leo hauoneshi dalili yoyote ya kuanza kufanya kazi, haufunguliwi na hauoneshimatumaini ya kufunguliwa.
“Ujenzi wa mradi huu wa machinjio hauoneshi dalili zozote utaanza kufanya kazi lini. Sikubaliani na hatua ya ujenzi wa mradi huu ambao umetumia fedha nyingi kiasi cha shilingi Bilioni 5.1 mpaka sasa na haujaanza kufanya kazi na kuna mapungufu mengi katika mradi huu, hali inayofanya wananchi wakose kazi na ajira”, amesema Katambi.
Katmbi amesema kutokana na mradi huo wa machinjio kukwawama kuna mambo lazima yachunguzwe ili kuondoa mashaka na hatua za kisheria "Lazima hatua zichukuliwe ili tujiridhishe kama fedha zimetumika kiha tujue,sasa ni wakati wa kuchukua hatua".
“Haiwezekani viwanda vya Shinyanga kila vinapoanzishwa vinakwama, kile kiwanda cha Old Shinyanga kilishakwama. Najua viongozi wengi wakiwemo Mawaziri wamewahi kufika hapa na kuahidiwa kuwa kiwanda kitafunguliwa punde lakinihakifunguliwi.
Maelezo ni haya haya hatua hazikuchuliwa, Mimi sitakubali kiwanda kukwama,hatuwezi kuwa tunaimba kila siku, hatua hazichukuliwi, jambo hili nalichukua nitalipeleka katika mamlaka zinazohusika na ni lazima hatua zichukuliwe kwa yeyote aliyesababisha mradi huu ukwame.
Ni lazima tujue mbivu na mbichi kama mradi huu unafunguliwa au la. Na kama haufunguliwi tujue fedhazimeenda wapi”,ameongeza Katambi.
Hata hivyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga,Mhe. David Nkulila amesema manispaa ya Shinyangakupitia kamati ya fedha imeagiza kuitwa na kuhojiwakwa Wakuu wa Idara wa Manispaa ya Shinyangaakiwemo aliyekuwa Afisa Mifugo waManispaa, Afisa Mipango, Mhandisi, AfisaManunuzi, Mhandisi Mshauri, Contractor wa mradi HomeAfrica Investment ili waeleze kuhusu sababu za kukwama kwa mradi huo na Mkurugenzi wa Manispaa achukue hatua za kisheria.
“Ujenzi wa mradi huu wa machinjio hauoneshi dalili zozote utaanza kufanya kazi lini. Sikubaliani na hatua ya ujenzi wa mradi huu ambao umetumia fedha nyingi kiasi cha shilingi Bilioni 5.1 mpaka sasa na haujaanza kufanya kazi na kuna mapungufu mengi katika mradi huu, hali inayofanya wananchi wakose kazi na ajira”, amesema Katambi.
Katmbi amesema kutokana na mradi huo wa machinjio kukwawama kuna mambo lazima yachunguzwe ili kuondoa mashaka na hatua za kisheria "Lazima hatua zichukuliwe ili tujiridhishe kama fedha zimetumika kiha tujue,sasa ni wakati wa kuchukua hatua".
“Haiwezekani viwanda vya Shinyanga kila vinapoanzishwa vinakwama, kile kiwanda cha Old Shinyanga kilishakwama. Najua viongozi wengi wakiwemo Mawaziri wamewahi kufika hapa na kuahidiwa kuwa kiwanda kitafunguliwa punde lakinihakifunguliwi.
Maelezo ni haya haya hatua hazikuchuliwa, Mimi sitakubali kiwanda kukwama,hatuwezi kuwa tunaimba kila siku, hatua hazichukuliwi, jambo hili nalichukua nitalipeleka katika mamlaka zinazohusika na ni lazima hatua zichukuliwe kwa yeyote aliyesababisha mradi huu ukwame.
Ni lazima tujue mbivu na mbichi kama mradi huu unafunguliwa au la. Na kama haufunguliwi tujue fedhazimeenda wapi”,ameongeza Katambi.
Hata hivyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga,Mhe. David Nkulila amesema manispaa ya Shinyangakupitia kamati ya fedha imeagiza kuitwa na kuhojiwakwa Wakuu wa Idara wa Manispaa ya Shinyangaakiwemo aliyekuwa Afisa Mifugo waManispaa, Afisa Mipango, Mhandisi, AfisaManunuzi, Mhandisi Mshauri, Contractor wa mradi HomeAfrica Investment ili waeleze kuhusu sababu za kukwama kwa mradi huo na Mkurugenzi wa Manispaa achukue hatua za kisheria.