Shinyanga: Mzee wa miaka 70 ashambuliwa na fisi akiwa amelala usiku

Matukio ya fisi kuua watu mara zote yanatokea kwa wingi Kanda ya Ziwa! Hivi hao fisi huwa wanafugwa huko, au wanatokea hifadhini.

Watu wa Kanda ya Ziwa tafadhali, naombeni mnisaidie kwenye ufafanuzi.
Hawa ni fisi watu, ushirikina umezidi, npo meatu najionea
 
..lakini mkuu hizo nyumba za wenzetu zikoje yani fisi anakuja usiku anavunja mlango anaingia ndani na kuvunja mwingine wa kuingia chumbani na kuanza kushambulia watu!!
Nyumba zenyewe ni tembe, milango ni vibati vimeunganishwa na vimbao
 
Nilikuwa namsoma tu huyu jamaa hapo juu nkajisemea huyu bwana hamjui fisi.

Fisi ni habari nyingine, fisi ni muoga akiwa kashiba ila akiwa na njaa hata simba anasanda.

Fisi wakiwa kikundi hata simba wanakimbia na kuwaachia mzoga licha ya wao kuwa ndio waliowinda.

Narudia kusema "Fisi muoga ni yule aliyeshiba tu mwenye njaa ni jasiri mithili ya Simba"
 
Tena ukutane na fisi madoa, vichaa walee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…