Shinyanga: Watumishi 4 Wafikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi

Shinyanga: Watumishi 4 Wafikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Walioshtakiwa ni Abel J. Kitinya (Mlinzi wa Mahakama ya Mwanzo Shinyanga), Janeth W. Lugano (Mwinjilisti), Mariam W. Kiloba (Mfanyabiashara) na Magreth W. Kiloba (Mfanyabiashara).

Mshtakiwa Abel Joseph Kitinya amesomewa Mashtaka ya kujihusisha na vitendo vya Rushwa na Kughushi Nyaraka. Washtakiwa 2, 3 na 4 wanakabiliwa na Makosa ya kuwasilisha Nyaraka za Uongo na kujipatia Tsh. Milioni 22,166,666 kila mmoja.

Kesi hiyo yenye Usajili wa CC. No. 6/2023, chini ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeahirishwa hadi Machi 28, 2023 itakaporejea Mahakamani kwa ajili ya kusoma hoja za Awali.
 
Walioshtakiwa ni Abel J. Kitinya (Mlinzi wa Mahakama ya Mwanzo Shinyanga), Janeth W. Lugano (Mwinjilisti), Mariam W. Kiloba (Mfanyabiashara) na Magreth W. Kiloba (Mfanyabiashara)...
Mpaka hapa Hakuna kesi tuendelee na kawaida.
 
Kamateni wa matrillioni sio kudeal na hao wadogo wa vicents ambao hamwalipi hata stahiki zao na salaries....

TAKUKURU YENYEWE INANUKA RUSHWA.
 
Back
Top Bottom