Shirika la reli (trc) acheni uhuni

activist

Senior Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
180
Reaction score
281
Treni ya shirika la reli tanzania imekwama eneo la same toka jana asubuhi. Treni hiyo iliyoondoka dar juzi kwenda mikoa ya kilimanjaro na arusha ilitegemewa kuwasili kilimanjaro jana alfajiri ila imekwama maeneo ya same pasipo shirika la reli kutoa taarifa kwa uma au abiria huku wananchi wakiendelea kuteseka maporini. Baadhi ya abiria wakiwemo watoto na wagonjwa imewabidi kukodi pikipiki iwapeleke same mjini ambapo ni umbali mrefu ili waweze kuendelea na safari zao. Shirika limeshimdwa kuwa na uungwana angalau kwa dharura kuhakikisha wateja wao wanasaidika. Serikali ya Mama kizimkazi imekwama kwa kila kitu.
 
Treni ya shirika la reli tanzania imekwama eneo la same toka jana asubuhi. Treni hiyo iliyoondoka dar juzi kwenda mikoa ya kilimanjaro na arusha ilitegemewa kuwasili kilimanjaro jana alfajiri ila imekwama maeneo ya same pasipo shirika la reli kutoa taarifa kwa uma au abiria huku wananchi wakiendelea kuteseka maporini. Baadhi ya abiria wakiwemo watoto na wagonjwa imewabidi kukodi pikipiki iwapeleke same mjini ambapo ni umbali mrefu ili waweze kuendelea na safari zao. Shirika limeshimdwa kuwa na uungwana angalau kwa dharura kuhakikisha wateja wao wanasaidika. Serikali ya Mama kizimkazi imekwama kwa kila kitu.
 
Poleni mkuu
 
Hamia Naigeria ambako usafiri wa treni ni BURE na mabasi ni NUSU ya NAURI mpaka baada ya tarehe 6 Januari.
 
Imekwama kwa kuharibika ama kuna shida nyingine?

Poleni sana kwa yaliyowakuta mkuu.
 
Wenyewe si wapo humu muwatag

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…