Shobo na waarabu wakati wenyewe hawatupendi, suala la Michezo Yanga na Simba

Kaka yake shetani

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2023
Posts
5,771
Reaction score
14,732
Watanzania ni wanafiki sana tena ukisafiri ndio utawafahamu. Waarabu wenyewe hawatupendi na kitendo walichotufanyia kwao kabisa kinaonesha wenzetu wana ushirikiano, huwezi kuona mpinzani wa kwao kashangilia timu ngeni.

Huku kwetu yaani mijitu badala ya kuipongeza yanga wao wanashobokea waarabu utadhani wamezaliwa huko.

Utaifa kwanza, Yanga hongereni
 
Ukiambiwa athari za ukoloni ndio hizo sasa ni ngumu kutoka zinakaa kizazi hadi kizaziii...
 
Hapo siyo kushobokea Waarabu
Watu wanafurahia Yanga kushindwa siyo Waarabu kushinda
 
Wale madogo ball boys walifanya kazi tukufu sana iliyomvuruga mleta uzi.

Kuna wakati refa alienda kumfokea mmoja wao, dogo mjeuri wa kiarabu akawa anamcheki tu refa kama ganda la muwa, na baada ya muda mfupi akarusha mipira mingine uwanjani, ikawa mipira 3 kwa wakati mmoja.
 
Inaonekana mlihitaji sana mbinu kutoka kwa Simba ila tatizo mlileta dharau sana ndiyo mjifunze wakati mwingine kuwa na adabu kwa waliokutangulia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…