Shoneni suti za kuipokea Simba SC wakitua airport toka Lubumbashi,imeshaingia nusu fainali

Shoneni suti za kuipokea Simba SC wakitua airport toka Lubumbashi,imeshaingia nusu fainali

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Watanzania wote na wanaSimba mnatakiwa kujiandaa mapema. Kwa vipato vyetu kutungua suti dukani hiyo jumapili inaweza kuwa ngumu,anza kabisa kesho kuongea na fundi,mpe tahadhari ijumaa iwe imekuwa tayari,jumamosi ufue na iweke kwenye sanduku. Ili jumapili au jumatatu unakuwa ndani ya suti kali ukiwapokea wanyama Simba SC toka Congo wakiwa wametinga nusu fainali.

Wale wanaotudharau na kutukatisha tamaa hawajaanza leo. Wapo toka enzi za Nkana FC,lakini ajabu wakati wao wanacheza rede na kina Lipuli na Ndanda siye tunacheza football na Mabigwa wa Africa,African giants Al Ahl na TP Mazembe.

Bado muda kidogo watatuheshimu tu pale tutakapo washika mkono na kuwaingiza CAF Club Bigwa bila wao kuwa na uwezo huo. Mnapopitisha bakuli hakikisheni linatosha kupanda ndege mwakani mtakapo shiriki kupitia nguvu ya Simba

Kumbuka suti yako iwe na logo ya Simba SC kifuani mkono wa kuume
 
Na wale wanaovaa dela la TP Mazembe wajue mwaka kesho SIMBA Tumo tena Klabu bingwa AFRIKA.
Kweli kabisa. Ila kwa bahati mbaya na wao watakuwepo clab bingwa baada ya simba kuwabeba. Tuwaombee njaa gor mahia (ambaye kimsingi hawezi kutoboa nusu fainali CCC) ili tuwe nao pamoja msimu ujao wa CCL
 
Hii week kelele mjini zimepungua ila bado zipo-zipo..
lakini kuanzia jumapili kelele zitaisha kabisaa... story kuu itaanza kuwa kuiondoa yanga nafasi ya kwanza TPL...

Sie wazalendo suti tutashona, na kamwe hatuiombei mabaya club yetu pendwa... ila tu kelele zitaisha kabisa hapa mjini


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom