Shroud of Turin (Sanda Aliyovikwa Bwana Yesu Inayoonyesha SURA Yake). Je, ni kweli ilikuwa ya yesu kristo?

Kuna utata mkubwa kuhusu iwapo Shroud of Turin inayoaminika kuwa sanda ambayo ilivikwa mwili wa Yesu Kristo kabla ya kuzikwa, ni halisi au la....
Hadi sasa hakuna ushahidi wa kutosha na wa kuaminika kuonyesha kuwa Shroud of Turin ni halisi na inaonyesha sura ya Yesu Kristo...
Wataalamu wa masuala ya sayansi wamefanya uchunguzi wa kisayansi wa Shroud of Turin na wamegundua kuwa ni rahisi kwa Shroud hiyo kutengenezwa kwa teknolojia ya zamani, na kwamba haikuwa ya kale kama inavyodaiwa...

Shroud of Turin ni halisi au la linabaki kuwa suala la imani na maoni ya kibinafsi...
 
Naaam
Mkuu mambo mengi sana , yamebaki kuwa ni kitendawili kuhusu Shroud ,
 
Andiko fikirishi na zuri
 
Inawezekana Yesu kweli, kwani alikuwa mtu wa kawaida aliyeweza kutambua na kumtumia Kisto aliye ndani yake.
 
Swali nalojiuliza kwa hawa warumi,inawezekanaje wamshadadie huyo YESU kiasi hicho wakati alikuwa mtawaliwa wao?
Kuna jambo gani hapo!!??
 
Wazungu nibwaongo sana tena waongo kupitiliza. Kwa watu tunaofikiria kiundani mambo tunaweza kujua huu ni uongo mkubwa. Yesu alikufa akiwa kijana mdogo wa miaka 30 hii sura inaonesha ni ya mzee sana wa miaka 70 huko halafu mnatuambia ni ya yesu. Ijulikane yesu alikuwa mwarabu mweusi hakuwa mweupe kama tunavyofikiri na kuambiwa. Yesu hakuwa mrefu bali alikuwa mfupi chini ya 6ft, yesu hakuwa na uso mrefu alikuwa na uso mfupi na mpana sio kama picha tunazoziona.
 
Swali nalojiuliza kwa hawa warumi,inawezekanaje wamshadadie huyo YESU kiasi hicho wakati alikuwa mtawaliwa wao?
Kuna jambo gani hapo!!??
Naam
Kuna mambo mengi sana ambayo hatuyajui mkuu
 
Aiseee, mambo
Ni mengi sanaa yasiyojulikana
 
Aiseee
 
Ni utapeli wa Roman Catholic kuendelea kuhadaa watu hakuna sanda ya Yesu
 
Mimi ni artist.
Kuna kitu nitafanya na mtakuja kuamini kuwa ni kweli kabisaaa.


Pia, nikuambieni jambo ambalo Roho Mtakatifu anataka mlifahamu. Uthibitisho wa kuwa Yesu alikuja, akasulubiwa, akafa na kufufuka ni kwa kupitia Neno la Mungu. Majabali, mbao, misumari na masalia ya nguo hayana viwango vya kuuthibitishia ulimwengu kuhusu Injili na kusamehewa dhambi zetu.

Wanaofanya haya mambo ya hadaa kuhusu kanzu, sanda na material things wanaongozwa na roho ya mpinga kristo.

Stuka
 
Naam
Nadhani kama umeisoma vyema Nyuzii hii utaona nmejaribu kuiandika kwa Mtindo wa maswali juu ya Kile kinachosemwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…