DIDAS TUMAINI
JF-Expert Member
- Nov 11, 2014
- 242
- 676
Serikali ya Mkoa wa Singida imefanya uamuzi wa kubadili jina la uwanja wa mpira wa MAMFUA STADIUM na sasa umepewa jina la LITTI STADIUM ikiwa ni hatua muhimu za kumuenzi mwanamke shujaa wa Singida aliyepigana na wakoloni wa Kijerumani kwa kutumia nyuki kama silaha ya mapambano.
LITTI alikuwa ni mwanamke shujaa aliyepigana na Wajerumani kwa kulinda himaya ya Wanyaturu akipinga utaratibu wa kupora ng'ombe, kupora nafaka, kutumikisha watu na kutoza kodi uliofanywa na wakoloni wa Kijerumani miaka ya 1907 - 1910.
Mwanamke huyu alifanikiwa kuwashinda Wajerumani kwenye mapambano mawili kwa kuwafurumushia nyuki na kuwaua baadhi ya askari ya Kijerumani. Pambano la tatu LITTI alisalitiwa na mtu wake wa karibu aliyetoa siri kwa Wajerumani na kufanikiwa kumkamata na kumchinja.
Kichwa cha mwanamke huyu kilichukuliwa kupelekwa Ujerumani hadi leo hakijarejeshwa Tanzania.
Tunaendelea kuwaibua mashujaa wetu ili waweze kutambuliwa na kuenziwa kwenye historia ya mkoa wa Singida na nchi yetu.
LITTI alikuwa ni mwanamke shujaa aliyepigana na Wajerumani kwa kulinda himaya ya Wanyaturu akipinga utaratibu wa kupora ng'ombe, kupora nafaka, kutumikisha watu na kutoza kodi uliofanywa na wakoloni wa Kijerumani miaka ya 1907 - 1910.
Mwanamke huyu alifanikiwa kuwashinda Wajerumani kwenye mapambano mawili kwa kuwafurumushia nyuki na kuwaua baadhi ya askari ya Kijerumani. Pambano la tatu LITTI alisalitiwa na mtu wake wa karibu aliyetoa siri kwa Wajerumani na kufanikiwa kumkamata na kumchinja.
Kichwa cha mwanamke huyu kilichukuliwa kupelekwa Ujerumani hadi leo hakijarejeshwa Tanzania.
Tunaendelea kuwaibua mashujaa wetu ili waweze kutambuliwa na kuenziwa kwenye historia ya mkoa wa Singida na nchi yetu.