Shule ya kwanza Tanganyika ilijengwa na waingereza huko Muheza

Shule ya kwanza Tanganyika ilijengwa na waingereza huko Muheza

MWAKA 1848, Mmishenari wa Kijerumani Dk Johan Ludwig Krapf, alitembelea kijiji cha Magila kilichopo Muheza mkoani Tanga akiwa katika safari zake za Afrika Mashariki.

Dk Krapf alipofika na kuwaona wagonjwa hao waliokuwa wakiishi kwa madhila makubwa, alichonga msalaba katika mti wa mkuyu kwa imani kuwa Mwenyezi Mungu angewaponya wagonjwa hao.

Eneo hilo ndilo lililokuja kujengwa shule ya kwanza na Waingereza mwaka 1886. Alama ya msalaba huo ipo hadi na sasa na ndipo ilipo Shule ya Sekondari Hegongo.

Hadi leo mahali hapo panaitwa Magila Msalabani. Kwa sasa Magila ni kata yenye vijiji vya vya Magila, Mikwamba, Misongeni na Mafleta.

Anawataja baadhi ya Wamishenari hao kuwa ni pamoja na David Livingstone, Charles Mackenzie, William Tozer na Edward Steer.

Anasema harakati hizo zilianzia tangu visiwa vya Zanzibar mwaka 1863 ambako pia walikomesha biashara ya utumwa na kuanza ujenzi wa kanisa la Anglikana la Mkunazini Zanzibar kwa miaka 10 tangu mwaka 1873.

Anasema wakati huo kulikuwa na shule iliyoanzishwa Zanzibar maeneo ya Kiungani na Kiinua mguu na Askofu William Tozer mwaka 1869. Hata hivyo, anasema shule hiyo haikuwa rasmi na ilikuwa ikifundisha elimu ya dini kwa watumwa waliokombolewa.

Uamuzi wa kujenga shule Bara
“Mnamo Agosti 13, 1967 Askofu Tozer alimtuma Padri CA Alington aende Vuga (Lushoto) kwa Chifu Kimweri ili apate kibali cha kujenga kituo cha misheni kwenye maeneo ya Bara,’’anasimulia Luteni Kanali Mhina na kuongeza:

“
Baadaye Januari 20, 1868, Padri Alington alirudi Vuga na kuruhusiwa na Chifu Kimweri kujenga sehemu yoyote katika maeneo ya Pwani.

Anasema Padri Alington aliamua kuchagua eneo la Magila ambalo lilikwishajulikana kutokana na alama ya msalaba uliowekwa na Dk Krapf.

“ “Shule ya sokoni ilikuwa kwanza kujengwa maeneo hayo mwezi Aprili 1869 chini ya Padri Fraser na wanafunzi wake walikuwa ni pamoja na Jumbe Kifungiwe na ndugu yake Sagosago na vijana wengine. Palikuwa na soko dogo na mti mkubwa wa Mzindanguuwe, watu wazima walipenda kukaa hapo ili walione jambo hilo geni,” anaongeza kusema.

Sekondari ya Hegongo
Hivi sasa eneo hilo kuna shule iitwayo Hegongo. Mkuu wa shule hiyo, Wilfred Mdimu anasisitiza kuwa eneo hilo ndipo palipojengwa shule ya kwanza Tanzania ambapo mpaka sasa kuna mabaki ya darasa la kwanza lililojengwa na Wamisheni.

Hivi sasa anasema darasa hilo linatumiwa kama ofisi ya walimu wa shule ya sekondari ya kata Magila.

“Hili ndilo darasa la kwanza lililojengwa mwaka 1869 na Waingereza. Awali lilikuwa ghorofa lakini likabadilishwa. Inasemekana shule nyingine ilijengwa Bagamoyo na baadaye Minaki,” anasema Mdimu na kuongeza,

“ Mwaka 1974 hadi 75, majengo hayo yakafanywa kuwa mahali pa kujifungulia wanawake na ndipo ilipoanzia hospitali teule ya Muheza. Lakini ikahamishiwa eneo ilipo sasa na majengo haya yakabaki matupu,” anasema Mdimu.

Kuanzishwa kwa Hegongo sekondari
Mwalimu Mdimu anasema baada ya majengo kubaki matupu, mwaka 1976 wenyeji wa Magila walimwomba Askofu wa kanisa hilo dayosisi ya kaskazini John Ramadhani, ili waanzishe shule ya sekondari hasa kwenye majengo ulipo msalaba wa Dk Krapf, naye akawakubalia.

“Februari 24, 1977 shule ya Hegongo ilianzishwa ikiwa chini ya wenyeji wa Magila ili kuwapa elimu watoto wa wilaya hiyo,” anasema.

Hata hivyo anasema shule hiyo haikuwa na maendeleo mazuri kwa muda mrefu. Isitoshe, wasimamizi wa shule hiyo walishindwa kuiendesha kutokana na madeni makubwa ya umeme, mishahara ya watumishi na mafao yao.

Hegongo ya sasa
Anasema hadi mwaka 2000 wasimamizi wa shule hii walishindwa kabisa kuiendesha wakairudisha kwa kanisa.

“Tangu wakati huo uongozi wa kanisa umeamua kuiendesha kwa kwa kulipa madeni makubwa yaliyokuwepo na kuimarisha hali ya elimu,” anasema na kuongeza:

Kwa upande mwingine, majengo ya zilizokuwa shule za St. Mary’s na St. Martin sasa zimechukuliwa na Serikali, huku mojawapo ikitumika kama shule ya sekondari ya kata ya Magila na nyingine kama shule ya msingi.

Mwananchi
Asante kwa historia NZURI. Naomba kunyoosha historia, hasa sehemu nilizoweka rangi.
1. 1967, ilikuwa 1867.
2. Askofu John Ramadhani (wakati huo) alikuwa wa Dayosisi ya Zanzibar na Tanga, (siyo Dayosisi ya kaskazini. Hapa mwandishi, pengine, kachukua mfumo wa KKKT. Kwa sasa Dayosisi hiyo ya Anglikana, imegawanywa kuwa dayosisi mbili: Dayosisi ya Zanzibar na Dayosisi ya Tanga.
3.Hapo kwa Dkt. Livingstone, yeye alishughulika zaidi na Umisioni Afrika ya Kati. Ripoti yake ndio iliyoibua hamasa kwa wanafunzi na wana taaluma wa Vyuo Vikuu vya Oxford na Cambridge kujiunga na Mision ya UMCA (University Mission for Central Africa) kwenda kupeleka ijnili "Afrika ya kati". Wakilenga zaidi Malawi, Zambia na Zimbabwe.
Kutokana na kushindwa kuingia eneo hilo kupitia Afrika ya Kusini, Walitumia Zanzibar. Shirika lao ni la Kiangilikana (lenye mlengo wa Ki Katoliki. Wao wanauita High Church.Ndio maana wanawaita Makasisi wao "Padri"). Maaskofu wake 3 wa kwanza ni Charles Mackenzie, William Tozer na Dkt. Edward Steer. Walieneza Injili kwa Kaskazini hadi Magila (baadae Korogwe). Hapa ndipo yalipo Makao Makuu ya Dayosisi ya Tanga. Walienea pia Dar es Salaam, Masasi, Ruvuma, Njombe na Mbeya.
Eneo hili ndilo limetoa Dayosisi za Anglikana zenye mfumo wa "High Church" za zanzibar, Tanga, Dar es Salaam, Masasi, Newala, Ruvuma, South Western Tanganyika (Njombe) na Sourthern Highlands (Mbeya).
Kwa taarifa, Dayosisi nyingine za Kanisa hilo zinafuata mfumo wa "Low Church" na zinatokana na shirika la Kimissioni la Church Mission Society (yaani CMS). Hawa wana historia tofauti kidogo. Hii ilianza na Dayosisi ya Central Tanganyika (Mwaka 1927). Hapa ndipo yalipo Makao Makuu ya Kanisa hilo Nchini.
 
mkuu shule ilijengwa na Waingereza au Wajerumani?
Ilijengwa na WAINGEREZA (wa Kanisa Anglikana), pamoja na kuwa wakati huo "Watawala" walikuwa Wajerumani. Wajerumani walikuja na Ulutheri.
Miongoni mwa shule walizojenga eneo hilo (ambalo kwa sasa kwa KKKT ni Dayosisi ya Kaskazini Mashariki-chini ya Askofu Dkt. Munga, ni Lwandai. Shule hii, ilihamishiwa Ilboru mwaka 1946. infact ndio iliyo "zaa" Ilboru Sekondari tuijuayo sasa. Hapa wamesoma watu wengi tu miongoni mwao Fred Sumaye, Paskali Mayalla, Hayati Sengondo Mvungi, wabunge 4 wa sasa wa Mkoa wa Singida: Allan Kiula, Antipasi Mnghway (Tundu Lissu), Lazaro Nyalandu na Mwigulu Nchemba...Miongoni mwa wengi.
Lwandai pia ndiyo chimbuko la Magamba Sekondari, mahali ambapo kipo Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (yaani SeKoMU)....
 
Daah huyo mhina ni babu yangu kafsriki mwezi mmoja sasa tumemzikA magila masoroko.
 
shule.jpg

MWAKA 1848, Mmishenari wa Kijerumani Dk Johan Ludwig Krapf, alitembelea kijiji cha Magila kilichopo Muheza mkoani Tanga akiwa katika safari zake za Afrika Mashariki.

Magila kuna mlima ulio katika safu za milima ya Usambara ukipakana na mlima wa Magoroto ambao ndio chanzo cha maji ya mto Mkurumuzi unaoelekea Muheza.

Historia inaonyesha eneo la mlima Magila wenye miamba na mawe mengi, zamani kabla ya kuja wageni lilitumika kuwatenga wagonjwa wa ukoma na magonjwa mengine yasiyotibika, kwa lengo la kuwazuia wasiwaambukize wengine.

Dk Krapf alipofika na kuwaona wagonjwa hao waliokuwa wakiishi kwa madhila makubwa, alichonga msalaba katika mti wa mkuyu kwa imani kuwa Mwenyezi Mungu angewaponya wagonjwa hao.

Eneo hilo ndilo lililokuja kujengwa shule ya kwanza na Waingereza mwaka 1886. Alama ya msalaba huo ipo hadi na sasa na ndipo ilipo Shule ya Sekondari Hegongo.

Hadi leo mahali hapo panaitwa Magila Msalabani. Kwa sasa Magila ni kata yenye vijiji vya vya Magila, Mikwamba, Misongeni na Mafleta.

Nilifika katika eneo hilo nilipokuwa wilayani Muheza hivi karibuni ili kuchunguza historia ya eneo hilo.

Hapo nikutana na Luteni Kanali mstaafu John Mhina ambaye amekamilisha kuandika kitabu kuhusu historia ya Magila Msalabani, kinachoeleza historia ya kijiji hicho na ujio wa wazungu walioanzisha shule ya kwanza Tanganyika na kanisa.

Luteni Kanali Mhina aliyelitumikia Taifa kwa muda mrefu kama mwanajeshi ,na baadaye kuwa Mbunge wa Muheza kutoka mwaka 1990 hadi 1995, anasema harakati za kuanzisha shule katika kijiji hicho zilitokana na Wamishenari waliokuja Afrika Mashariki kutoka Ulaya kwaajili ya kueneza dini ya kikristo tangu miaka ya 1770.

Anawataja baadhi ya Wamishenari hao kuwa ni pamoja na David Livingstone, Charles Mackenzie, William Tozer na Edward Steer.

Anasema harakati hizo zilianzia tangu visiwa vya Zanzibar mwaka 1863 ambako pia walikomesha biashara ya utumwa na kuanza ujenzi wa kanisa la Anglikana la Mkunazini Zanzibar kwa miaka 10 tangu mwaka 1873.

Anasema wakati huo kulikuwa na shule iliyoanzishwa Zanzibar maeneo ya Kiungani na Kiinua mguu na Askofu William Tozer mwaka 1869. Hata hivyo, anasema shule hiyo haikuwa rasmi na ilikuwa ikifundisha elimu ya dini kwa watumwa waliokombolewa.

Uamuzi wa kujenga shule Bara
“Mnamo Agosti 13, 1967 Askofu Tozer alimtuma Padri CA Alington aende Vuga (Lushoto) kwa Chifu Kimweri ili apate kibali cha kujenga kituo cha misheni kwenye maeneo ya Bara,’’anasimulia Luteni Kanali Mhina na kuongeza:

“ Padri Alington alimchukua Vincent Mkono aliyekuwa mwanafunzi wake wa Kiungani na mwingine Mwinyi Khatib aliyekuwa mkalimali. Msafara huo ulipata baraka za Sultan Majid aliyekuwa akitawala Zanzibar.”

Anaeleza kuwa baada ya msafara wao kufika Vuga, Chifu Kimweri aliwasikiliza, lakini akaomba apewe muda wa kutafakari kwanza.

Baadaye Januari 20, 1868, Padri Alington alirudi Vuga na kuruhusiwa na Chifu Kimweri kujenga sehemu yoyote katika maeneo ya Pwani.

Anasema Padri Alington aliamua kuchagua eneo la Magila ambalo lilikwishajulikana kutokana na alama ya msalaba uliowekwa na Dk Krapf.

“ Jumbe Kifungiwe aliyekuwa akiongoza Magila wakati huo chini ya baraza la ‘wamaka’ (Baraza la Wazee wa Kibondei), walimpa mlima wote wa Magila wakidhani kuwa atashindwa kujenga kwa sababu ya kuwa na mawe mengi….kwa mshangao aliporudi aliyatumia mawe hayo kujengea.” anaeleza.

Anasema pamoja na kazi ya kueneza dini Wamishenari hao walijipa jukumu la kuwatunza wagonjwa wa ukoma na kuanzisha shule.

“Shule ya sokoni ilikuwa kwanza kujengwa maeneo hayo mwezi Aprili 1869 chini ya Padri Fraser na wanafunzi wake walikuwa ni pamoja na Jumbe Kifungiwe na ndugu yake Sagosago na vijana wengine. Palikuwa na soko dogo na mti mkubwa wa Mzindanguuwe, watu wazima walipenda kukaa hapo ili walione jambo hilo geni,” anaongeza kusema.

Sekondari ya Hegongo
Hivi sasa eneo hilo kuna shule iitwayo Hegongo. Mkuu wa shule hiyo, Wilfred Mdimu anasisitiza kuwa eneo hilo ndipo palipojengwa shule ya kwanza Tanzania ambapo mpaka sasa kuna mabaki ya darasa la kwanza lililojengwa na Wamisheni.

Hivi sasa anasema darasa hilo linatumiwa kama ofisi ya walimu wa shule ya sekondari ya kata Magila.

“Hili ndilo darasa la kwanza lililojengwa mwaka 1869 na Waingereza. Awali lilikuwa ghorofa lakini likabadilishwa. Inasemekana shule nyingine ilijengwa Bagamoyo na baadaye Minaki,” anasema Mdimu na kuongeza,

“Walijenga pia kanisa baada ya lile la Mkunazini Zanzibar. Lakini lilipochakaa ndipo wakajenga kanisa jingine mwaka 1886 kama lile la Mkunazini na ndiyo linatumika hadi sasa.”

Akizungumzia uchaguzi wa eneo hilo, Mdimu anasema awali wazungu walitaka kujenga shule maeneo ya Muhenza Mkumbi na Mkanyageni, lakini wakaathiriwa na malaria, ndipo wakahamia katika mlima wa Magila.

Kuhusu shule hiyo, Mdimu anasema kuwa awali ililenga kuwaandaa Waafrika ili wawasaidie wamisheni katika kazi zao. Waliwafundisha kusoma, kuandika na kuhesabu.

Baadaye elimu ikapanuka baada ya shule za St. Marys na St Martin kujengwa zikiongeza masomo na wanafunzi.

Anaongeza kuwa shule hizo hazikudumu muda mrefu, bali zilibadilishwa na kuwa Sekondari ya wasichana ambayo nayo ilikuja kuhamishiwa wilayani Korogwe ilipo shule ya wasichana maarufu kwa jina la Korogwe girls.

Baada ya kuhamisha shule hiyo, matumizi yakabadilishwa na kikaanzisha chuo cha ualimu kwa wanawake tu. Hata hivyo, anasema chuo hicho nacho kilihamishiwa tena Korogwe kilipo chuo cha ualimu hadi leo.

“ Mwaka 1974 hadi 75, majengo hayo yakafanywa kuwa mahali pa kujifungulia wanawake na ndipo ilipoanzia hospitali teule ya Muheza. Lakini ikahamishiwa eneo ilipo sasa na majengo haya yakabaki matupu,” anasema Mdimu.

Kuanzishwa kwa Hegongo sekondari
Mwalimu Mdimu anasema baada ya majengo kubaki matupu, mwaka 1976 wenyeji wa Magila walimwomba Askofu wa kanisa hilo dayosisi ya kaskazini John Ramadhani, ili waanzishe shule ya sekondari hasa kwenye majengo ulipo msalaba wa Dk Krapf, naye akawakubalia.

“Februari 24, 1977 shule ya Hegongo ilianzishwa ikiwa chini ya wenyeji wa Magila ili kuwapa elimu watoto wa wilaya hiyo,” anasema.

Hata hivyo anasema shule hiyo haikuwa na maendeleo mazuri kwa muda mrefu. Isitoshe, wasimamizi wa shule hiyo walishindwa kuiendesha kutokana na madeni makubwa ya umeme, mishahara ya watumishi na mafao yao.

Hegongo ya sasa
Anasema hadi mwaka 2000 wasimamizi wa shule hii walishindwa kabisa kuiendesha wakairudisha kwa kanisa.

“Tangu wakati huo uongozi wa kanisa umeamua kuiendesha kwa kwa kulipa madeni makubwa yaliyokuwepo na kuimarisha hali ya elimu,” anasema na kuongeza:

“Kwa sasa tunaboresha majengo, tumejenga maabara, maktaba ya kisasa na tutaongeza nyingine. Askofu wa sasa ameamua kuwachukua mapadri 10 waliomaliza kidato cha sita na kuwapeleka vyuo vikuu ili wasomee ualimu kwa ajili ya shule hii.’’

Kwa upande mwingine, majengo ya zilizokuwa shule za St. Mary’s na St. Martin sasa zimechukuliwa na Serikali, huku mojawapo ikitumika kama shule ya sekondari ya kata ya Magila na nyingine kama shule ya msingi.

Mwananchi
Makala nzuri,ila ingependeza zaidi kama kungekuwa na picha za kutosha.
Asante kwa historia NZURI. Naomba kunyoosha historia, hasa sehemu nilizoweka rangi.
1. 1967, ilikuwa 1867.
2. Askofu John Ramadhani (wakati huo) alikuwa wa Dayosisi ya Zanzibar na Tanga, (siyo Dayosisi ya kaskazini. Hapa mwandishi, pengine, kachukua mfumo wa KKKT. Kwa sasa Dayosisi hiyo ya Anglikana, imegawanywa kuwa dayosisi mbili: Dayosisi ya Zanzibar na Dayosisi ya Tanga.
3.Hapo kwa Dkt. Livingstone, yeye alishughulika zaidi na Umisioni Afrika ya Kati. Ripoti yake ndio iliyoibua hamasa kwa wanafunzi na wana taaluma wa Vyuo Vikuu vya Oxford na Cambridge kujiunga na Mision ya UMCA (University Mission for Central Africa) kwenda kupeleka ijnili "Afrika ya kati". Wakilenga zaidi Malawi, Zambia na Zimbabwe.
Kutokana na kushindwa kuingia eneo hilo kupitia Afrika ya Kusini, Walitumia Zanzibar. Shirika lao ni la Kiangilikana (lenye mlengo wa Ki Katoliki. Wao wanauita High Church.Ndio maana wanawaita Makasisi wao "Padri"). Maaskofu wake 3 wa kwanza ni Charles Mackenzie, William Tozer na Dkt. Edward Steer. Walieneza Injili kwa Kaskazini hadi Magila (baadae Korogwe). Hapa ndipo yalipo Makao Makuu ya Dayosisi ya Tanga. Walienea pia Dar es Salaam, Masasi, Ruvuma, Njombe na Mbeya.
Eneo hili ndilo limetoa Dayosisi za Anglikana zenye mfumo wa "High Church" za zanzibar, Tanga, Dar es Salaam, Masasi, Newala, Ruvuma, South Western Tanganyika (Njombe) na Sourthern Highlands (Mbeya).
Kwa taarifa, Dayosisi nyingine za Kanisa hilo zinafuata mfumo wa "Low Church" na zinatokana na shirika la Kimissioni la Church Mission Society (yaani CMS). Hawa wana historia tofauti kidogo. Hii ilianza na Dayosisi ya Central Tanganyika (Mwaka 1927). Hapa ndipo yalipo Makao Makuu ya Kanisa hilo Nchini.
 
Ilijengwa na WAINGEREZA (wa Kanisa Anglikana), pamoja na kuwa wakati huo "Watawala" walikuwa Wajerumani. Wajerumani walikuja na Ulutheri.
Miongoni mwa shule walizojenga eneo hilo (ambalo kwa sasa kwa KKKT ni Dayosisi ya Kaskazini Mashariki-chini ya Askofu Dkt. Munga, ni Lwandai. Shule hii, ilihamishiwa Ilboru mwaka 1946. infact ndio iliyo "zaa" Ilboru Sekondari tuijuayo sasa. Hapa wamesoma watu wengi tu miongoni mwao Fred Sumaye, Paskali Mayalla, Hayati Sengondo Mvungi, wabunge 4 wa sasa wa Mkoa wa Singida: Allan Kiula, Antipasi Mnghway (Tundu Lissu), Lazaro Nyalandu na Mwigulu Nchemba...Miongoni mwa wengi.
Lwandai pia ndiyo chimbuko la Magamba Sekondari, mahali ambapo kipo Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (yaani SeKoMU)....
kaka miongoni mwa shule walizojenga wakati huo ni w3ajerumani au waingereza?kwa kumbukumbu sikumbuki mwaka wajerumani walijenga shule za msingi za kuishia darasa la nne na lengo kupata makarani kwa wakati wao sikumbuki mwaka ila nikipita hicho kitabu nitakiweka na picha ya hiyo shule na kinasema shule ya kwanza tanganyika ya wajerumani ilikua vuga huku usambara.
kuhusu lwandai ni ya kkkt dayosisis ya kaskazini mashariki ila ninavyojua mashirika yalitoleta injili tanga na kilimanjaro na arusha ni tofauti.
nakubali kukosolewa mkuu nipe ufafanuzi
 
shule.jpg

MWAKA 1848, Mmishenari wa Kijerumani Dk Johan Ludwig Krapf, alitembelea kijiji cha Magila kilichopo Muheza mkoani Tanga akiwa katika safari zake za Afrika Mashariki.

Magila kuna mlima ulio katika safu za milima ya Usambara ukipakana na mlima wa Magoroto ambao ndio chanzo cha maji ya mto Mkurumuzi unaoelekea Muheza.

Historia inaonyesha eneo la mlima Magila wenye miamba na mawe mengi, zamani kabla ya kuja wageni lilitumika kuwatenga wagonjwa wa ukoma na magonjwa mengine yasiyotibika, kwa lengo la kuwazuia wasiwaambukize wengine.

Dk Krapf alipofika na kuwaona wagonjwa hao waliokuwa wakiishi kwa madhila makubwa, alichonga msalaba katika mti wa mkuyu kwa imani kuwa Mwenyezi Mungu angewaponya wagonjwa hao.

Eneo hilo ndilo lililokuja kujengwa shule ya kwanza na Waingereza mwaka 1886. Alama ya msalaba huo ipo hadi na sasa na ndipo ilipo Shule ya Sekondari Hegongo.

Hadi leo mahali hapo panaitwa Magila Msalabani. Kwa sasa Magila ni kata yenye vijiji vya vya Magila, Mikwamba, Misongeni na Mafleta.

Nilifika katika eneo hilo nilipokuwa wilayani Muheza hivi karibuni ili kuchunguza historia ya eneo hilo.

Hapo nikutana na Luteni Kanali mstaafu John Mhina ambaye amekamilisha kuandika kitabu kuhusu historia ya Magila Msalabani, kinachoeleza historia ya kijiji hicho na ujio wa wazungu walioanzisha shule ya kwanza Tanganyika na kanisa.

Luteni Kanali Mhina aliyelitumikia Taifa kwa muda mrefu kama mwanajeshi ,na baadaye kuwa Mbunge wa Muheza kutoka mwaka 1990 hadi 1995, anasema harakati za kuanzisha shule katika kijiji hicho zilitokana na Wamishenari waliokuja Afrika Mashariki kutoka Ulaya kwaajili ya kueneza dini ya kikristo tangu miaka ya 1770.

Anawataja baadhi ya Wamishenari hao kuwa ni pamoja na David Livingstone, Charles Mackenzie, William Tozer na Edward Steer.

Anasema harakati hizo zilianzia tangu visiwa vya Zanzibar mwaka 1863 ambako pia walikomesha biashara ya utumwa na kuanza ujenzi wa kanisa la Anglikana la Mkunazini Zanzibar kwa miaka 10 tangu mwaka 1873.

Anasema wakati huo kulikuwa na shule iliyoanzishwa Zanzibar maeneo ya Kiungani na Kiinua mguu na Askofu William Tozer mwaka 1869. Hata hivyo, anasema shule hiyo haikuwa rasmi na ilikuwa ikifundisha elimu ya dini kwa watumwa waliokombolewa.

Uamuzi wa kujenga shule Bara
“Mnamo Agosti 13, 1967 Askofu Tozer alimtuma Padri CA Alington aende Vuga (Lushoto) kwa Chifu Kimweri ili apate kibali cha kujenga kituo cha misheni kwenye maeneo ya Bara,’’anasimulia Luteni Kanali Mhina na kuongeza:

“ Padri Alington alimchukua Vincent Mkono aliyekuwa mwanafunzi wake wa Kiungani na mwingine Mwinyi Khatib aliyekuwa mkalimali. Msafara huo ulipata baraka za Sultan Majid aliyekuwa akitawala Zanzibar.”

Anaeleza kuwa baada ya msafara wao kufika Vuga, Chifu Kimweri aliwasikiliza, lakini akaomba apewe muda wa kutafakari kwanza.

Baadaye Januari 20, 1868, Padri Alington alirudi Vuga na kuruhusiwa na Chifu Kimweri kujenga sehemu yoyote katika maeneo ya Pwani.

Anasema Padri Alington aliamua kuchagua eneo la Magila ambalo lilikwishajulikana kutokana na alama ya msalaba uliowekwa na Dk Krapf.

“ Jumbe Kifungiwe aliyekuwa akiongoza Magila wakati huo chini ya baraza la ‘wamaka’ (Baraza la Wazee wa Kibondei), walimpa mlima wote wa Magila wakidhani kuwa atashindwa kujenga kwa sababu ya kuwa na mawe mengi….kwa mshangao aliporudi aliyatumia mawe hayo kujengea.” anaeleza.

Anasema pamoja na kazi ya kueneza dini Wamishenari hao walijipa jukumu la kuwatunza wagonjwa wa ukoma na kuanzisha shule.

“Shule ya sokoni ilikuwa kwanza kujengwa maeneo hayo mwezi Aprili 1869 chini ya Padri Fraser na wanafunzi wake walikuwa ni pamoja na Jumbe Kifungiwe na ndugu yake Sagosago na vijana wengine. Palikuwa na soko dogo na mti mkubwa wa Mzindanguuwe, watu wazima walipenda kukaa hapo ili walione jambo hilo geni,” anaongeza kusema.

Sekondari ya Hegongo
Hivi sasa eneo hilo kuna shule iitwayo Hegongo. Mkuu wa shule hiyo, Wilfred Mdimu anasisitiza kuwa eneo hilo ndipo palipojengwa shule ya kwanza Tanzania ambapo mpaka sasa kuna mabaki ya darasa la kwanza lililojengwa na Wamisheni.

Hivi sasa anasema darasa hilo linatumiwa kama ofisi ya walimu wa shule ya sekondari ya kata Magila.

“Hili ndilo darasa la kwanza lililojengwa mwaka 1869 na Waingereza. Awali lilikuwa ghorofa lakini likabadilishwa. Inasemekana shule nyingine ilijengwa Bagamoyo na baadaye Minaki,” anasema Mdimu na kuongeza,

“Walijenga pia kanisa baada ya lile la Mkunazini Zanzibar. Lakini lilipochakaa ndipo wakajenga kanisa jingine mwaka 1886 kama lile la Mkunazini na ndiyo linatumika hadi sasa.”

Akizungumzia uchaguzi wa eneo hilo, Mdimu anasema awali wazungu walitaka kujenga shule maeneo ya Muhenza Mkumbi na Mkanyageni, lakini wakaathiriwa na malaria, ndipo wakahamia katika mlima wa Magila.

Kuhusu shule hiyo, Mdimu anasema kuwa awali ililenga kuwaandaa Waafrika ili wawasaidie wamisheni katika kazi zao. Waliwafundisha kusoma, kuandika na kuhesabu.

Baadaye elimu ikapanuka baada ya shule za St. Marys na St Martin kujengwa zikiongeza masomo na wanafunzi.

Anaongeza kuwa shule hizo hazikudumu muda mrefu, bali zilibadilishwa na kuwa Sekondari ya wasichana ambayo nayo ilikuja kuhamishiwa wilayani Korogwe ilipo shule ya wasichana maarufu kwa jina la Korogwe girls.

Baada ya kuhamisha shule hiyo, matumizi yakabadilishwa na kikaanzisha chuo cha ualimu kwa wanawake tu. Hata hivyo, anasema chuo hicho nacho kilihamishiwa tena Korogwe kilipo chuo cha ualimu hadi leo.

“ Mwaka 1974 hadi 75, majengo hayo yakafanywa kuwa mahali pa kujifungulia wanawake na ndipo ilipoanzia hospitali teule ya Muheza. Lakini ikahamishiwa eneo ilipo sasa na majengo haya yakabaki matupu,” anasema Mdimu.

Kuanzishwa kwa Hegongo sekondari
Mwalimu Mdimu anasema baada ya majengo kubaki matupu, mwaka 1976 wenyeji wa Magila walimwomba Askofu wa kanisa hilo dayosisi ya kaskazini John Ramadhani, ili waanzishe shule ya sekondari hasa kwenye majengo ulipo msalaba wa Dk Krapf, naye akawakubalia.

“Februari 24, 1977 shule ya Hegongo ilianzishwa ikiwa chini ya wenyeji wa Magila ili kuwapa elimu watoto wa wilaya hiyo,” anasema.

Hata hivyo anasema shule hiyo haikuwa na maendeleo mazuri kwa muda mrefu. Isitoshe, wasimamizi wa shule hiyo walishindwa kuiendesha kutokana na madeni makubwa ya umeme, mishahara ya watumishi na mafao yao.

Hegongo ya sasa
Anasema hadi mwaka 2000 wasimamizi wa shule hii walishindwa kabisa kuiendesha wakairudisha kwa kanisa.

“Tangu wakati huo uongozi wa kanisa umeamua kuiendesha kwa kwa kulipa madeni makubwa yaliyokuwepo na kuimarisha hali ya elimu,” anasema na kuongeza:

“Kwa sasa tunaboresha majengo, tumejenga maabara, maktaba ya kisasa na tutaongeza nyingine. Askofu wa sasa ameamua kuwachukua mapadri 10 waliomaliza kidato cha sita na kuwapeleka vyuo vikuu ili wasomee ualimu kwa ajili ya shule hii.’’

Kwa upande mwingine, majengo ya zilizokuwa shule za St. Mary’s na St. Martin sasa zimechukuliwa na Serikali, huku mojawapo ikitumika kama shule ya sekondari ya kata ya Magila na nyingine kama shule ya msingi.

Mwananchi
mkuu miaka naona kwenye miaka kuna walakini mfano mwaka 1967 siamini ndo mwaka walioamua kuamia bara
 
Back
Top Bottom