Mapambano Yetu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 1,130
- 2,102
Inasikitisha sana kuona serikali hii ya JK imeshindwa kabisa kuhakikisha walau kila wilaya hapa nchini inakuwa na shule ya A'level (Kidato cha tano & sita). Utashangaa Wilaya kongwe Mfano Halmashauri ya Morogoro pamoja na Ukerewe hazina Shule yenye A'level ya serikali. Halmashauri ya Morogoro ina A'level ya private moja tu (KIZUKA) wakati Ukerewe Hakuna hata moja. Hizo ni baadhi tu lakini wadau nadhani mtakuwa mnaelewa ninachomaanisha.
Katika dunia ya leo tunahitaji kuwa na shule za A'level mpaka ngazi ya kata ili angalau vijana wengi ambao kimsingi tumeadhimia elimu yao ya msingi ikomee kidato cha nne basi wapate nafasi ya kujiendeleza na kidato cha tano & Sita kupitia shule hizo.
Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo hili linatakiwa kuwa miongoni mwa ilani za uchaguzi za vyama vya siasa ambavyo kimsingi viko mstari wa mbele katika kusimamia maendeleo ya watanzania kwa ujumla.
Naomba kuwakilisha.
Katika dunia ya leo tunahitaji kuwa na shule za A'level mpaka ngazi ya kata ili angalau vijana wengi ambao kimsingi tumeadhimia elimu yao ya msingi ikomee kidato cha nne basi wapate nafasi ya kujiendeleza na kidato cha tano & Sita kupitia shule hizo.
Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo hili linatakiwa kuwa miongoni mwa ilani za uchaguzi za vyama vya siasa ambavyo kimsingi viko mstari wa mbele katika kusimamia maendeleo ya watanzania kwa ujumla.
Naomba kuwakilisha.