Wakusoma 12
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 4,035
- 11,462
Wakuu habari za mchana, moja kwa moja kwenye maada. Ni kwa muda mrefu Sasa kumekuwepo na utaratibu wa kuziita shule za watanzania (wananchi) kuwa ni shule za serikali jambo ambalo naliona siyo sawa.
Ki kawaida shule hizi zinatakiwa ziitwe "shule za Umma (Public schools) na siyo shule za serikali (Government schools).
Shule hizi zote za Umma zinazopokea ruzuku ya serikali ziwe mali ya Umma huku shule ambazo hazipokei ruzuku ya serikali zibaki zikiitwa shule za binafsi.
Kwanini nasema hivi ni kwa sababu huko mbele mambo yanaweza kubadirika na shule za serikali kuchukua mkondo mpya na watu kujimilikisha kama walivyofanya kwenye viwanja vya michezo.
Siyo Kila mtu anaunga mkondo au mtiifu kwa serikali ila Umma ni jambo ambalo haliepukiki kwenye mtindo wa maisha, hivyo napendekeza shule zetu tuziite za Umma ili kuhimiza uzalendo na ushiriki wa wananchi katika maswala ya kielimu.
Ki kawaida shule hizi zinatakiwa ziitwe "shule za Umma (Public schools) na siyo shule za serikali (Government schools).
Shule hizi zote za Umma zinazopokea ruzuku ya serikali ziwe mali ya Umma huku shule ambazo hazipokei ruzuku ya serikali zibaki zikiitwa shule za binafsi.
Kwanini nasema hivi ni kwa sababu huko mbele mambo yanaweza kubadirika na shule za serikali kuchukua mkondo mpya na watu kujimilikisha kama walivyofanya kwenye viwanja vya michezo.
Siyo Kila mtu anaunga mkondo au mtiifu kwa serikali ila Umma ni jambo ambalo haliepukiki kwenye mtindo wa maisha, hivyo napendekeza shule zetu tuziite za Umma ili kuhimiza uzalendo na ushiriki wa wananchi katika maswala ya kielimu.