Shule za VIPAJI maalum: Nini dhumuni lake hasa?

Shule za VIPAJI maalum: Nini dhumuni lake hasa?

Kiraka Kikuu

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
5,903
Reaction score
1,979
Habarini wakuu!
Kuna hizi shule zinazoitwa "Shule za wanafunzi wenye Vipaji vya kipekee vya kiakili."
Kigezo pekee kinacho tumika kudahili wanafunzi huko ni "national exams".
Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa:
1: Hivi ni kweli wanafunzi wanao soma,au walio wahi soma huko wana "vipaji vya kipekee vya kiakili"?
2: Kama jibu 1 ni ndiyo,mazingira gani yamewekwa katika shule hizo,ya kuweza kukuza "vipaji vya kipekee vya kiakili vya wanafunzi hawa?
3: Pia kama jibu na 1 ni ndiyo,kwanini baadhi ya wanafunzi wanatoka na div two au div three,ambazo ni common kwenye shule za kawaida?
4: Kuna empirical evidence yoyote ya product toka shule hizo i.e. Tabora Boys,Mzumbe,Kibaha,Ilboru na Kilakala kuwa na utendaji/ubunifu ulio tukuka after school?
[nimeiacha Kisimiri kwani ni special ya hv karibuni.]
Karibuni kwa mjadala.
 
Habarini wakuu!
Kuna hizi shule zinazoitwa "Shule za wanafunzi wenye Vipaji vya kipekee vya kiakili."
Kigezo pekee kinacho tumika kudahili wanafunzi huko ni "national exams".
Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa:
1: Hivi ni kweli wanafunzi wanao soma,au walio wahi soma huko wana "vipaji vya kipekee vya kiakili"?
2: Kama jibu 1 ni ndiyo,mazingira gani yamewekwa katika shule hizo,ya kuweza kukuza "vipaji vya kipekee vya kiakili vya wanafunzi hawa?
3: Pia kama jibu na 1 ni ndiyo,kwanini baadhi ya wanafunzi wanatoka na div two au div three,ambazo ni common kwenye shule za kawaida?
4: Kuna empirical evidence yoyote ya product toka shule hizo i.e. Mzumbe,Kibaha,Ilboru na Kilakala kuwa na utendaji/ubunifu ulio tukuka after school?
[nimeziacha Tabora boys na Kisimiri kwani ni special za hv karibuni.]
Karibuni kwa mjadala.

TABORABOYS ndio special ya kwanza tanzania
 
Lengo la kuwa na shule hizo ni zuri kwa maana ya kuwaweka watoto wenye vipaji maalum kama vile vya ubunifu ili waweze kuwa pamoja na kushirikiana katika kubuni vitu. Tatizo lililokuwepo kwenye ni jinsi ya kuwapata kwa kutumia matokeo ya mtihani wa kuandika tu, ingekuwa vizuri kama watoto wangechunguzwa vipaji vyao halsi tangu shule na aina ya maisha wanayoishi nje ya shule, kwa kutumia ufaulu wa mtihani kama kigezo, kuna uwezekano wa kuchukua mtoto aliyeba mtihani kwa hiyo yeye kipaji atachokuwa nacho ni cha wizi wa mitihani na atakapokuwa mkubwa na kuajiriwa sehemu ataendeleza kipaji chake kwa kuiba mali ya uuma na kuwa fisadi.
 
Hivi kufaulu mitihani sio kipaji?

Well,ni kipaji,
ila jaribu kuangalia shule kama Marian Girls,Feza boys na St.Francis,
wanafaulu vizuri mitihani,na mazingira bora yamewekwa kukuza vipaji vingine kama michezo n.k.
Ukiangalia vema maisha ya wanafunzi wa special schools,wanatumia karibu masaa 18 had 20 in a day just studying hard [KUTOBOA].
I wonder kama ndio lengo kuu la kuanzishwa kwake.
 
Mkuu kabla ya kujibu maswali yako labda naomba tuwekane sawa kwenye msamiati huu wa "Vipaji Maalumu" au "Vipaji Maalumu Kiakili".

Elimu ya sekondari ya Tanzania kwa nyakati nilizokuwa nasoma ilikuwa na shule za aina nne zenye kutoa mafunzo ya elimu hiyo.

1. Shule za Vipaji Maalumu
2. Shule za Mafunzo ya Ufundi
3. Shule za Bweni zisizo na Umaalumu au Mafunzo ya Ufundi
4. Shule za Kutwa

Namna ya kudahiliwa au kujiunga na shule hizi ilitegemea na viwango vya ufaulu wa wanafunzi, iwe kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari au kutoka "ordinary level" kwenda "advanced level".

Binafsi nimefanikiwa kusoma kwa miaka sita katika shule hizi za vipaji maalumu, na wakati ule namaliza darasa la saba tulikuwa tunatahiniwa masomo matatu tu nayo ni Hisabati, Maarifa na Lugha ambapo kila somo lilikuwa linapewa alama hamsini.
Ili uweze kujiunga na shule za vipaji ilikuwa unatakiwa upate jumla ya alama kati ya 145 hadi 150.

Kwa baadhi ya mikoa ambayo viwango vya elimu ya msingi vilikuwa duni, wanafunzi kutoka mikoa hiyo walipunguziwa alama kiasi wenye ufaulu wa alama 138 waliweza kupata nafasi pia.

Kwa wale waliotakiwa kujiunga na shule za ufundi ufaulu wa somo la Hisabati ulizingatiwa zaidi, wanafunzi wa shule hizo wengi wao walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kukokotoa hisabati.
 
Walikuwa wanataka kuandaa akina Newton, Albert na Galileo. Basi tu project haiku-mature ila lengo lilikuwa sahihi.
 
1: Hivi ni kweli wanafunzi wanao soma,au walio wahi soma huko wana "vipaji vya kipekee vya kiakili"?

Ni ngumu kujibu moja kwa moja NDIO au HAPANA isipokuwa asilimia kubwa ya wanafunzi hao wana vipaji vya pekee vya kiakili, huenda ikawa ni kwenye somo moja pekee au baadhi ya masomo au yote.

Kitu pekee ambacho shule hizi zimekuwa nacho au zilikuwa nacho ni ile ushindani, hamasa na molari wa wanafunzi kutaka kufikia malengo au ndoto zao za maisha ya kielimu.

Mitaala inayotumika huko ni ile ile itumiwayo na shule nyinginezo, waalimu ni wale wale (by the way hakuna waalimu wenye vipaji maalumu vya kiakili hahah).

2: Kama jibu 1 ni ndiyo,mazingira gani yamewekwa katika shule hizo,ya kuweza kukuza "vipaji vya kipekee vya kiakili vya wanafunzi hawa?

Ni ushindani, kujituma na molari tu wa wanafunzi ndio chanzo kikuu cha ufaulu kuwa mkubwa.

Wengi wa wanafunzi wanaopelekwa shule hizi wanajua kuwa wapo uwanja wa vita na itakuwa ni dhuluma kwa nafsi zao wasipotumia fursa waliyopata.

3: Pia kama jibu na 1 ni ndiyo,kwanini baadhi ya wanafunzi wanatoka na div two au div three,ambazo ni common kwenye shule za kawaida?

Kuna sababu nyingi mkuu, baadhi ya mambo ambayo nilipata kuyaona wakati huo ni;
1. Kubweteka kwa baadhi ya wanafunzi.
2. Ugumu wa matumizi ya lugha haswa kwa wanafunzi wanaotoka sehemu za vijijini kiasi kwamba njia pekee watumiayo ni kukariri.
3. Kuendekeza starehe maana shule zote za vipaji ni za bweni.
4. Ufukara (wanafunzi wenye uwezo walikuwa wakisoma masomo ya ziada aka tuition wawapo likizo).

4: Kuna empirical evidence yoyote ya product toka shule hizo i.e. Mzumbe,Kibaha,Ilboru na Kilakala kuwa na utendaji/ubunifu ulio tukuka after school?

Wapo wengi tu mkuu isipokuwa wengi ni underdogs na wengine wapo ughaibuni wakifanya mambo yao huko.

nimeziacha Tabora boys na Kisimiri kwani ni special za hv karibuni.

Mkuu umeikosea sana heshima Tabora Boys kuiita ni shule ya vipaji ya karibuni, kumbukumbu zangu zinaonesha hiyo ndio ya kwanza kuliko nyinginezo.
 
Walikuwa wanataka kuandaa akina Newton, Albert na Galileo. Basi tu project haiku-mature ila lengo lilikuwa sahihi.

Ni kweli kabisa konnie, wazo lilikuwa zuri isipokuwa utekelezaji kwa namna fulani ulikwama...
 
Ni ngumu kujibu moja kwa moja NDIO au HAPANA isipokuwa asilimia kubwa ya wanafunzi hao wana vipaji vya pekee vya kiakili, huenda ikawa ni kwenye somo moja pekee au baadhi ya masomo au yote.
Kwa hiyo ni "vipaji maalum" kwenye masomo tu?

Kitu pekee ambacho shule hizi zimekuwa nacho au zilikuwa nacho ni ile ushindani, hamasa na molari wa wanafunzi kutaka kufikia malengo au ndoto zao za maisha ya kielimu.
Is this fair?
Nimebahatika kusoma miaka 6 huko, MZUMBE o level,then Kibaha A Level,nilipo htm miaka kadhaa ilopita.
Wanafunzi wanaachwa kama kuku wa kienyeji,sylabi haziwi covered,then wanasoma kupita kiasi [hata wengine huchizika]

Mitaala inayotumika huko ni ile ile itumiwayo na shule nyinginezo, waalimu ni wale wale (by the way hakuna waalimu wenye vipaji maalumu vya kiakili hahah).[
Walimu wenye vipaji wapo aisee!
Namkumbuka Wibonele Mz [RIP] na Sir Mgina KBH,LOL!



Ni ushindani, kujituma na molari tu wa wanafunzi ndio chanzo kikuu cha ufaulu kuwa mkubwa.

Wengi wa wanafunzi wanaopelekwa shule hizi wanajua kuwa wapo uwanja wa vita na itakuwa ni dhuluma kwa nafsi zao wasipotumia fursa waliyopata.



Kuna sababu nyingi mkuu, baadhi ya mambo ambayo nilipata kuyaona wakati huo ni;
1. Kubweteka kwa baadhi ya wanafunzi.
2. Ugumu wa matumizi ya lugha haswa kwa wanafunzi wanaotoka sehemu za vijijini kiasi kwamba njia pekee watumiayo ni kukariri.
3. Kuendekeza starehe maana shule zote za vipaji ni za bweni.
4. Ufukara (wanafunzi wenye uwezo walikuwa wakisoma masomo ya ziada aka tuition wawapo likizo).



Wapo wengi tu mkuu isipokuwa wengi ni underdogs na wengine wapo ughaibuni wakifanya mambo yao huko.



Mkuu umeikosea sana heshima Tabora Boys kuiita ni shule ya vipaji ya karibuni, kumbukumbu zangu zinaonesha hiyo ndio ya kwanza kuliko nyinginezo.
Mkuu,T.Boys imepewa hadhi ya u special miaka ya 2000's!
 
Sasa ulitaka wapimweje jamani?

Utaratibu wa watoto kwenda sekondari ulipimwa kwa mitihani ya masomo, na hicho kilitumika kama kigezo.

Wangewaonaje hao vipaji maalumu nje ya darasani? Wale waliokuwa na ubunifu nje ya darasa walianzishiwa vyuo vya ufundi, kama mtu anakipaji basi walau akavumbue jembe/sindano/shoka huko ufundi.

Kwa hiyo ni "vipaji maalum" kwenye masomo tu?
 
Wale waliokuwa na ubunifu nje ya darasa walianzishiwa vyuo vya ufundi, kama mtu anakipaji basi walau akavumbue jembe/sindano/shoka huko ufundi.

Ha ha ha!
Kongosho, you are always funny!
 
Last edited by a moderator:
Katika hizo shule wengi wao wana vipaji vya kubeba maandishi/kukariri kwa kiwango kikubwa sana.
Ni wachache sana wameweza kuja na maarifa au vitu vipya kuonyesha wao wana vipaji bada ya kumaliza hizo shule.
Huo ni ushuhuda wang kwa miaka niliyosoma huko.
 
Kwa hiyo ni "vipaji maalum" kwenye masomo tu?

Ndio maana yake mkuu, ni vipaji maalumu kwa mujibu wa mitaala iliyopo ambayo 100% ni elimu ya darasani.

Is this fair?
Nimebahatika kusoma miaka 6 huko, MZUMBE o level,then Kibaha A Level,nilipo htm miaka kadhaa ilopita.
Wanafunzi wanaachwa kama kuku wa kienyeji,sylabi haziwi covered,then wanasoma kupita kiasi [hata wengine huchizika]

Sijui kwa nini umeuliza kama ni fair au unfair.

Binafsi naamini mwanafunzi yoyote inampasa awe na ndoto fulani maishani kama kuwa rubani, daktari, mkulima, mwalimu n.k

Ili ndotoze zitimie inampasa awe mshindani, awe na hamasa fulani pia awe na molari wa kutaka kufikia malengo au ndoto zake za maisha ya kielimu.

Walimu wenye vipaji wapo aisee!
Namkumbuka Wibonele Mz [RIP] na Sir Mgina KBH,LOL!

Hahah ile niliiweka kufurahisha genge tu, ndio sio siri marehemu Mwl Wibonele wa Mzumbe wakati huo alikuwa mzuri sana wa Fizikia kwa namna nilivyokuwa nikimsikia, Mr Mgina wa Kibaha naye kwa Fizikia alikuwa mzuri, kuna Mwl mmoja wa practicals za Chemistry A Level nakumbuka tu aka yake ya Abacha, kuna kina Mr&Mrs Mkwizu, Mr Tara, Mr Kiringo, Mr Mushi (Ilboru) na wengine wengi tu kuwataja hapatoshi hapa.

Mkuu,T.Boys imepewa hadhi ya u special miaka ya 2000's!

Sidhani mkuu, tangu mimi naanza form I na niliijua Tabora kama shule maalumu isipokuwa watu wengi hawakupenda kupelekwa huko kwa kuwa kulikuwa mbali.

Hiyo miaka ya 2000's ulikuwa ni mpango wa Wizara ya Elimu kutaka kuifufua shule hiyo maana iliachwa mbali sana na shule kama Mzumbe, Ilboru na Kibaha.

Kuna wakati fulani miaka hiyo ya 2000 walipelekwa wanafunzi wengi sana wa form waliofaulu vizuri sana, na serikali kupitia waziri wa wakati huo kama sikosei ni Mungai yule akapiga marufuku uhamisho. (lakini nchi yetu hii nadhani waijua kutoa tamko sio kusimamia tamko, miezi sita ya mwanzo wanafunzi wengi wakaikimbia shule wakaenda Mzumbe, Ilboru na Kibaha).
 
Kwa kuwa umeamua kuamini hivyo basi sawa...

Ndio nikwenda huko nikitokea shule zisizo na vipaji. Kwa mfano mtoto wa form 1 anatumia zaidi ya masaa 6 kujisomea mwenyewe tu, huyo mtu akifaulu zaidi ya wengne utasema ana kipaji.
 
Fanya uchunguzi wa hao waliokuwa wanasemekana kuwa wana vipaji uone hata uko makazini walipo wameweza kuja hata na chochote kipya. Mi nakwambia wengi wao ni mabingwa wa kukariri maandishi tu.
 
Back
Top Bottom