Shule za VIPAJI maalum: Nini dhumuni lake hasa?

Shule za VIPAJI maalum: Nini dhumuni lake hasa?

habarini wakuu!
Kuna hizi shule zinazoitwa "shule za wanafunzi wenye vipaji vya kipekee vya kiakili."
kigezo pekee kinacho tumika kudahili wanafunzi huko ni "national exams".
Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa:
1: Hivi ni kweli wanafunzi wanao soma,au walio wahi soma huko wana "vipaji vya kipekee vya kiakili"?
2: Kama jibu 1 ni ndiyo,mazingira gani yamewekwa katika shule hizo,ya kuweza kukuza "vipaji vya kipekee vya kiakili vya wanafunzi hawa?
3: Pia kama jibu na 1 ni ndiyo,kwanini baadhi ya wanafunzi wanatoka na div two au div three,ambazo ni common kwenye shule za kawaida?
4: Kuna empirical evidence yoyote ya product toka shule hizo i.e. Mzumbe,kibaha,ilboru na kilakala kuwa na utendaji/ubunifu ulio tukuka after school?
[nimeziacha tabora boys na kisimiri kwani ni special za hv karibuni.]
karibuni kwa mjadala.
hata mimi nilichaguliwa kwenda shule ya wasichana ya vipaji maalumu sio wote ni vipaji bali pia juhudi binaffsi
nairi kwamba asilimia 80%mtoe mwigulu mchemba wengi hawajaishia hapa hapa wengi wameenda mbali na wanamafanikio makubwa sana sana kielimu na kiutafiti,kwa ninaowafahamu mimi wengi wameishia kuchukuliwa na nchi za watu huko huko wanakokwenda kusoma seems their potential.na ukija ona watu kama wakina mwigulu -ilboru ndio wanaoharibu hizi shule maana hawakwenda pale kama vipaji maalumu kweli ni michongo nakushikwa mkono lakini.ila hata kama sio kipaji maalumu ukikopy hawa wenye navyo ukaweka juhudi binafsi basi na wewe unaitwa kipaji maalumu.
 
Kwa kuwa umeamua kuamini hivyo basi sawa...

Embu naomba nieleweshe!! Nini maana ya kipaji maalumu?? Je hizi shule mnazoita "za vipaji maalumu" ziko wapi??
Kama mdau alivosema mtu kufaulu ni kipaji maalumu je kama kasoma shule yakata na akapata one je na yeye ana kipaji maalumu au alisoma shule ya vipaji maalum?? Je hizi shule za seminary na hiz za st st kama marian, feza nazo ni za vipaji maalum?? mayakubanga nahitaji majibu yako pia..
 
Last edited by a moderator:
hata mimi nilichaguliwa kwenda shule ya wasichana ya vipaji maalumu sio wote ni vipaji bali pia juhudi binaffsi
nairi kwamba asilimia 80%mtoe mwigulu mchemba wengi hawajaishia hapa hapa wengi wameenda mbali na wanamafanikio makubwa sana sana kielimu na kiutafiti,kwa ninaowafahamu mimi wengi wameishia kuchukuliwa na nchi za watu huko huko wanakokwenda kusoma seems their potential.na ukija ona watu kama wakina mwigulu -ilboru ndio wanaoharibu hizi shule maana hawakwenda pale kama vipaji maalumu kweli ni michongo nakushikwa mkono lakini.ila hata kama sio kipaji maalumu ukikopy hawa wenye navyo ukaweka juhudi binafsi basi na wewe unaitwa kipaji maalumu.

Nini maana ya kipaji maalumu?
 
Naendelea kusisitiza wenye vipaji ni wachache wengi wao ni mabingwa wa kukariri masomo. Nimesoma nao na wengi hao hawana ukipaji wowote.
 
Mwanafunzi anatumia robo tatu ya siku katika kusoma alafu akifaulu unataka tumuone kuwa ana kipaji, hapana hili halipo sahihi hata kidogo. Kuomba ubaki ulipokwenda kusoma si kigezo cha kuona kuwa huyo mtu ana kipaji, ila inaweza kuwa ni cheap labour kwa kuwa hawakukugharamia masomo yako toka shule ya msingi hadi A-level.
 
Mwanafunzi anatumia robo tatu ya siku katika kusoma alafu akifaulu unataka tumuone kuwa ana kipaji, hapana hili halipo sahihi hata kidogo. Kuomba ubaki ulipokwenda kusoma si kigezo cha kuona kuwa huyo mtu ana kipaji, ila inaweza kuwa ni cheap labour kwa kuwa hawakukugharamia masomo yako toka shule ya msingi hadi A-level.

Kaka punguza hasira...
Cc watu8
 
Last edited by a moderator:
Habarini wakuu!
Kuna hizi shule zinazoitwa "Shule za wanafunzi wenye Vipaji vya kipekee vya kiakili."
Kigezo pekee kinacho tumika kudahili wanafunzi huko ni "national exams".
Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa:
1: Hivi ni kweli wanafunzi wanao soma,au walio wahi soma huko wana "vipaji vya kipekee vya kiakili"?
2: Kama jibu 1 ni ndiyo,mazingira gani yamewekwa katika shule hizo,ya kuweza kukuza "vipaji vya kipekee vya kiakili vya wanafunzi hawa?
3: Pia kama jibu na 1 ni ndiyo,kwanini baadhi ya wanafunzi wanatoka na div two au div three,ambazo ni common kwenye shule za kawaida?
4: Kuna empirical evidence yoyote ya product toka shule hizo i.e. Mzumbe,Kibaha,Ilboru na Kilakala kuwa na utendaji/ubunifu ulio tukuka after school?
[nimeziacha Tabora boys na Kisimiri kwani ni special za hv karibuni.]
Karibuni kwa mjadala.

kisimiri, naomba uniambie tafadhali ipo mkoa gani?
 
Ndio nikwenda huko nikitokea shule zisizo na vipaji. Kwa mfano mtoto wa form 1 anatumia zaidi ya masaa 6 kujisomea mwenyewe tu, huyo mtu akifaulu zaidi ya wengne utasema ana kipaji.

Hahahah!!!

Ni mwanafunzi gani wa kidato cha kwanza asiye struggle??

Umesahau kuwa mfumo wa elimu ya msingi hutumia lugha ya Kiswahili halafu ghafla mwanafunzi anabadilika kuelekea mfumo wa Kiingereza!

Halafu pia hivi hujui kuwa kukariri maandishi ni hatua ya kuelekea kuelewa? Naomba urudie tena kusoma somo moja la Baiolojia linaloitwa coordination
 
Hahahah!!!

Ni mwanafunzi gani wa kidato cha kwanza asiye struggle??

Umesahau kuwa mfumo wa elimu ya msingi hutumia lugha ya Kiswahili halafu ghafla mwanafunzi anabadilika kuelekea mfumo wa Kiingereza!

Halafu pia hivi hujui kuwa kukariri maandishi ni hatua ya kuelekea kuelewa? Naomba urudie tena kusoma somo moja la Baiolojia linaloitwa coordination

Huo ni mfano mmoja tu, ukwel ni kwamba muda mwingi wa wanafunzi wa hizi shule unatumika ktk kusoma.

Nikupe mfano mwngine kuhusu mwanafunzi wa A-level anayelamba glucose kuhakikisha kuwa anakuwa na nguvu ya kutosha ili asome kwa muda mrefu, huyo mwanafunza anaamka saa 10 alfajiri anaanza kujisomea hadi muda wa mstarini bada ya hapo anaingia kwenye ratiba ya masomo ya kawaida, sa tisa mchana anakwenda kula bada ya hapo anarud kujisomea hadi saa 11 na nusu jioni.
Baada ya hapo anapumzka hadi saa 1 usiku, anakwenda kula hadi kufika mida ya saa 2 anarudi tena darasani na kuanza kusoma hadi saa 7 usiku, anakwenda kulala inapofika saa 10 alfajiri anaanza ratiba yake upya.

Najua ni njia ya kuelekea kuelewa ila kama una muda katafute filamu moja inaitwa THREE ------, ni filamu inayoweza kukufanya ukatofautsha kukariri na kipaji.
 
Embu naomba nieleweshe!! Nini maana ya kipaji maalumu??

Mkuu hilo ni jina tu ambalo kama hiyo vision ingeweza kutimia sidhani kama ungelikuwa na doubts.

Lengo kuu la dhana hii lilikuwa ni kufanya incubation ya wale wanafunzi wanaojiweza kiakili kupitia alama zao za ufaulu.

Je hizi shule mnazoita "za vipaji maalumu" ziko wapi??

Shule ambazo zilikuwa allocated kwa mission hiyo zilitengwa katika makundi mawili, wasichana na wavulana na shule hizo ni Ilboru, Mzumbe, Tabora Wavulana, Kibaha, Kilakala, Msalato, Tabora Wasichana (Hizi ndio ninazozifahamu)...

Kama mdau alivosema mtu kufaulu ni kipaji maalumu je kama kasoma shule yakata na akapata one je na yeye ana kipaji maalumu au alisoma shule ya vipaji maalum??

Kufaulu tu haitoshi isipokuwa umefaulu kwa kiwango gani.

Division One ni daraja lenye points nyingi tu sasa sijui intention yako ilikuwa ni alama gani ya division one?

Je hizi shule za seminary na hiz za st st kama marian, feza nazo ni za vipaji maalum?? mayakubanga nahitaji majibu yako pia..

Hizo shule ulizozitaja sio za vipaji maalumu, kumbuka kuwa shule za vipaji zinamilikiwa na serikali chini ya Wizara ya Elimu kwa 100%.
 
Fanya uchunguzi wa hao waliokuwa wanasemekana kuwa wana vipaji uone hata uko makazini walipo wameweza kuja hata na chochote kipya. Mi nakwambia wengi wao ni mabingwa wa kukariri maandishi tu.

Wengi wao hawana vipaji vyovyote vile vilivyo maalumu.

Ni nani kati ya waliosoma huko ambaye walau kavumbua hata kifomyula cha uongo na kweli?

Ni nani kati yao ambaye hata kaja na kinadharia cha uongo na kweli?

Kufaulu mtihani wa taifa si kipaji maalumu. Ni juhudi na bidii tu. Sasa mtu mwenye juhudi na bidii katika jambo fulani ndo ana kipaji maalumu?

Ndo maana sishangai nchi kuwa na hali iliyonayo!!
 
Huo ni mfano mmoja tu, ukwel ni kwamba muda mwingi wa wanafunzi wa hizi shule unatumika ktk kusoma.

Mkuu ni wanafunzi wangapi wanatumia muda mwingi kusoma hadi kuloweka miguu kwenye mabeseni na bado wanashindwa kufaulu?

Binafsi jambo pekee ninalohisi lina mushkeli ni matumizi ya msamiati "kipaji", serikali hailitendei haki neno hilo kwa kushindwa kuweka facilities za kutosha katika shule hizi.

Kwa mantiki hiyo dhana nzima ya neno kipaji inapotea na kuonekana wasomao huko ni wasongo au vipanga fulani tu wanafagiliwa kuwa wana akili.
 
Nakubaliana nawe 100 kwa 100.

Hahaha!!!
Nyani Ngabu labda litumike neno gani mbadala kuziita shule hizi?

Btw huwa nakuona kwenye mijadala mingi pindi shule hizi zikiwekewa mijadala hapa...
 
Last edited by a moderator:
Hahaha!!!
Nyani Ngabu labda litumike neno gani mbadala kuziita shule hizi?

Btw huwa nakuona kwenye mijadala mingi pindi shule hizi zikiwekewa mijadala hapa...

We ndugu si umesoma kwenye hizo shule? Kama umesoma huko, wewe una kipaji gani kilicho maalumu?

Huwa unaniona kwenye hii mijadala kwa sababu huwa sipendi mambo kupotoshwa. Mtu hana kipaji chochote kilicho maalumu lakini kwa vile ana juhudi na bidii ya kujisomea na inatokea anafaulu mtihani wa mwisho basi eti ndo anapachikwa ukipaji maalumu.

Come on now.
 
pamoja na yaliyosemwa na wadau! Mimi nionavyo ni kwamba shule za vipaji maalum ama special schools zilirithiwa na kuendelezwa (kwa maana historia inasema hivi toka kwa wakoloni) kwa madhumuni ya kuwafanya wanafunzi wanaosemekana kuwa na akili na maarifa ama vipaji maalum kuzidi wengine kulinda na kuendeleza zaidi vile vipaji vyao. Kwa namna nyingine sioni umuhimu wa shule hizi kwakua kwanza, zinatengeneza matabaka baina ya wanafunzi, pili Tanzania inaendelea kudumisha mabaki ya ukoloni katika elimu ambapo inatengeneza mifumo miwili ya elimu ambayo ni elimu kwa wote kama shule za kata nakadhalika pia shule maalum ambazo wengi wa wanafunzi huwa ni watoto wa wakubwa ama undugu hutumika katika machaguzi ya wanafunzi (kwa siku hizi)
 
Mkuu ni wanafunzi wangapi wanatumia muda mwingi kusoma hadi kuloweka miguu kwenye mabeseni na bado wanashindwa kufaulu?.

Je unachokariri hadi unakikeshea kinatoka kwenye mtihani? Kama wana vipaji basi wengi wao wana vipaji vya uwezo mkubwa wa kukariri masomo.
 
shule za wenye vipaji maalumu zipo hata nchi zingne kama usa.
HADI university zipo kwa mfano qualification za kuingia stanford univ.havard,m.i.t ni za juu zaidi ya vyuo vingine.lakini nao bado wana consider academic qualification
 
Back
Top Bottom