Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Promota mkubwa wa ngumi hapa nchini Tanzania ,JAY MSANGI anashutumiwa kuwawekea madawa mabondia Ibrahimu Classic pamoja na mwenzake Adam Mbega.
Shutuma hizo zilitolewa na bondia Ibrahimu Classic kwa kudai kuwa Jay alihusika moja kwa moja kumuwekea yeye madawa ili asiweze kuona vizuri dhidi ya mpinzani wake ambaye walikuwa wanawania mkanda wa WBO, pia Ibrahimu alidai kuwa JAY alihusika pia katika kumuwekea madawa Adam Mbega ili ashindwe kufanya vizuri katika pambano lake ambapo alimsababishia matatizo ya tumbo Adam.
Mbali na hao Jay Msangi pia anahusishwa katika kumuhujumu bondia mwingine aitwae Muhsin Kizota kwa kufanya figisu figisu ili tu Muhsin apoteze pambano .
Mpaka mwisho wa pambano Ibrahimh Class alipoteza pambano round ya saba kwa Technical Knockout, Muhsin Kizota alipoteza pambano kwa Technical Knockout round ya sita na Adam Mbega alipoteza pambano kwa points round nane.
Mbaya zaidi JAY MSANGI aliamua kukimbia na pesa za mabondia hao.
Mbali na mabondia hao, mabondia wengi wamekuwa wakimshutumu Jay Msangi mara kwa mara kwamba yeye ndiye kisababishi kikuu cha wao kupoteza mapambano .
Inavyosemekana Jay Msangi huwalazimisha mabondia wakubali kupigwa na wazungu ili waongezewe dau na kama itatokea bondia akikataa kupigwa Jay atafanya kila ajualo yeye ili tu wabongo wapoteze pambano na hivyo kuwatengenezea wazungu rekodi nzuri za mapambano yao.
*********************************************
Ila kiukweli hata mimi huyu Jay Msangi nilikuwa nina mashaka naye sana kwa kipindi kirefu ,kwa sababu haiwezekani kila akiondoka na bondia hapa nchini huyo bondia lazima apoteze iwe isiwe,sijawahi kusikia au kuona hata mara moja Jay akisafiri na bondia halafu huyo bondia akashinda hilo pambano.
Mamlaka husika embu ingilieni kati hili suala .
Shutuma hizo zilitolewa na bondia Ibrahimu Classic kwa kudai kuwa Jay alihusika moja kwa moja kumuwekea yeye madawa ili asiweze kuona vizuri dhidi ya mpinzani wake ambaye walikuwa wanawania mkanda wa WBO, pia Ibrahimu alidai kuwa JAY alihusika pia katika kumuwekea madawa Adam Mbega ili ashindwe kufanya vizuri katika pambano lake ambapo alimsababishia matatizo ya tumbo Adam.
Mbali na hao Jay Msangi pia anahusishwa katika kumuhujumu bondia mwingine aitwae Muhsin Kizota kwa kufanya figisu figisu ili tu Muhsin apoteze pambano .
Mpaka mwisho wa pambano Ibrahimh Class alipoteza pambano round ya saba kwa Technical Knockout, Muhsin Kizota alipoteza pambano kwa Technical Knockout round ya sita na Adam Mbega alipoteza pambano kwa points round nane.
Mbaya zaidi JAY MSANGI aliamua kukimbia na pesa za mabondia hao.
Mbali na mabondia hao, mabondia wengi wamekuwa wakimshutumu Jay Msangi mara kwa mara kwamba yeye ndiye kisababishi kikuu cha wao kupoteza mapambano .
Inavyosemekana Jay Msangi huwalazimisha mabondia wakubali kupigwa na wazungu ili waongezewe dau na kama itatokea bondia akikataa kupigwa Jay atafanya kila ajualo yeye ili tu wabongo wapoteze pambano na hivyo kuwatengenezea wazungu rekodi nzuri za mapambano yao.
*********************************************
Ila kiukweli hata mimi huyu Jay Msangi nilikuwa nina mashaka naye sana kwa kipindi kirefu ,kwa sababu haiwezekani kila akiondoka na bondia hapa nchini huyo bondia lazima apoteze iwe isiwe,sijawahi kusikia au kuona hata mara moja Jay akisafiri na bondia halafu huyo bondia akashinda hilo pambano.
Mamlaka husika embu ingilieni kati hili suala .