Mnyakyusa5000
Member
- Sep 21, 2021
- 83
- 136
Tumefundishwa vibaya. Tangu tukiwa watoto tumeambiwa kufanya kazi kwa bidii huleta mafanikio. Tumehakikishiwa kuwa hakuna njia nyingine isipokuwa hii.
Sasa tumekua. Tumeingia katika shughuli za uzalishaji na mahusiano. Mambo haya mawili yaani uzalishaji mali na mahusiano yamekuwa mzigo mzito usiohimilika. Wengi wetu hatujafanikiwa kuhimili changamoto nyingi zitokanazo na mahitaji yanayotegemea vitu hivi.
Juhudi zetu hazizai matunda. Tunaamka asubuhi na mapema. Tunalala usiku wa manane. Hakuna kitu. Hatutoboi. Mahusiano hayawi bora wala hali zetu za kiuchumi.
Sasa ni muda wa kujiuliza. Je, tulielekezwa jambo sahihi? Ni kweli kuwa bidii na juhudi ndio njia pekee ya mafanikio? Mbona hatufanikiwi? Sisi sio wavivu. Sisi hatuchagui kazi. Inakuwaje?
Ukweli ni kuwa si sahihi kwamba bidii na juhudi huleta mafanikio. Sio kweli. Mafanikio hayaji kwa kufanya kazi kwa bidii bali kufanya kazi kwa furaha.
Mwanazuoni mashughuli aitwae Napoleon Hill ameandika katika moja ya vitabu vyake juu ya aina kumi na mbili za mafanikio. Anasema kuwa mafanikio ni: kuwa na akili tulivu, afya njema, mahusiano mema, kuwa huru dhidi ya hofu, kuwa na matumaini, kuwa na imani, ushirikiano, upendo, utayari wa kujifunza, nidhamu, kuwaelewa watu na kuwa na pesa.
Aina zote hizo za mafanikio hazipatikani kwa kuwa na bidii au juhudi isipokuwa hupatikana pale mtu anapoamua kuwa na furaha wakati wote.
Furaha tunayoizungumzia ni ile furaha ya asili. Furaha isiyotegemea mtu au kitu chochote. Furaha ambayo mtu huwa nayo bila sababu.
Tujifunze kufurahi wakati wote. Inalipa. Jaribu uone muujiza. Tabasamu kwa furaha wakati wote. Ongea na watu kwa furaha. Ishi nao kwa furaha. Fanya kazi kwa furaha. Furahi bila sababu yoyote. Wewe furahi tu. Furahi jua likiwaka. Furahi mvua ikinyesha. Fanya kila kitu unachopaswa kukifanya ukiwa na furaha uone jinsi aina mojamoja ya mafanikio itakavyokuja upande wako.
Sasa tumekua. Tumeingia katika shughuli za uzalishaji na mahusiano. Mambo haya mawili yaani uzalishaji mali na mahusiano yamekuwa mzigo mzito usiohimilika. Wengi wetu hatujafanikiwa kuhimili changamoto nyingi zitokanazo na mahitaji yanayotegemea vitu hivi.
Juhudi zetu hazizai matunda. Tunaamka asubuhi na mapema. Tunalala usiku wa manane. Hakuna kitu. Hatutoboi. Mahusiano hayawi bora wala hali zetu za kiuchumi.
Sasa ni muda wa kujiuliza. Je, tulielekezwa jambo sahihi? Ni kweli kuwa bidii na juhudi ndio njia pekee ya mafanikio? Mbona hatufanikiwi? Sisi sio wavivu. Sisi hatuchagui kazi. Inakuwaje?
Ukweli ni kuwa si sahihi kwamba bidii na juhudi huleta mafanikio. Sio kweli. Mafanikio hayaji kwa kufanya kazi kwa bidii bali kufanya kazi kwa furaha.
Mwanazuoni mashughuli aitwae Napoleon Hill ameandika katika moja ya vitabu vyake juu ya aina kumi na mbili za mafanikio. Anasema kuwa mafanikio ni: kuwa na akili tulivu, afya njema, mahusiano mema, kuwa huru dhidi ya hofu, kuwa na matumaini, kuwa na imani, ushirikiano, upendo, utayari wa kujifunza, nidhamu, kuwaelewa watu na kuwa na pesa.
Aina zote hizo za mafanikio hazipatikani kwa kuwa na bidii au juhudi isipokuwa hupatikana pale mtu anapoamua kuwa na furaha wakati wote.
Furaha tunayoizungumzia ni ile furaha ya asili. Furaha isiyotegemea mtu au kitu chochote. Furaha ambayo mtu huwa nayo bila sababu.
Tujifunze kufurahi wakati wote. Inalipa. Jaribu uone muujiza. Tabasamu kwa furaha wakati wote. Ongea na watu kwa furaha. Ishi nao kwa furaha. Fanya kazi kwa furaha. Furahi bila sababu yoyote. Wewe furahi tu. Furahi jua likiwaka. Furahi mvua ikinyesha. Fanya kila kitu unachopaswa kukifanya ukiwa na furaha uone jinsi aina mojamoja ya mafanikio itakavyokuja upande wako.