Utawala wa Jamal Malinzi umekuwa ukipokea shutuma nyingi kutoka pande mbalimbali za wadau wa soka. Mimi pia ni mmoja wa wakosoaji wake. Watu wengi tumekuwa tukihoji uwezo wake kiuongozi, uadilifu na umakini wake na wasaidizi wake katika shughuli ya usimamizi wa mchezo huu pendwa kuliko yote hapa nchini.
Mambo kama kashfa za rushwa na upangaji matokeo, tuhuma za ukabila, matumizi mabaya ya fedha, ubabe kwa kufungia wapinzani wake, na mengine yanayofanana na haya ndio yamekuwa mambo ambayo utawala huu umekuwa ukihusishwa nayo. Ilifikia watu kuona Malinzi na wenzake wameturudisha kipindi cha FAT ya akina Ndolanga na Rage.
Lakini katikati ya haya yote kuna kitu kiko dhahiri, nacho ni mafanikio ya kisoka katika miaka hii ya TFF chini ya Malinzi kuliko vipindi vingi tu huko nyuma! Na ili wadau tutende haki ni lazima tuzungumzie mambo haya kwa nia ya ku -acknowledge badala ya kukosoa tu sikuzote. Wakati tunaendelea kumkosoa ili kumtia spidi gavana, Malinzi ametujibu kupitia mafanikio yafuatayo, tena kwa mpigo;
1. Azam kuwa bingwa wa vilabu vya Afrika Mashariki na Kati (KAGAME)
2. Yanga kuwa timu pekee ktk eneo la ukanda wa CECAFA kucheza makundi ya kombe la
shirikisho la CAF.
3. Kilimanjaro Queens kutwaa kibabe ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA)
4. Serengeti Boys kukaribia kufuzu kushiriki fainali za vijana za CAF.
5. Kuendelea kuimarika kwa ushindani wa Ligi ya VPL na kupungua kwa malalamiko dhidi ya waamuzi.
Ni ukweli si mafanikio ya maana sana, lakini kwa nchi ambayo tumekuwa tukiambulia patupu karibu kila michuano ya soka tunayoshiriki, angalau kuna kitu kinaonekana hasa tunapoanza kuwa wababe kwa wanyonge wenzetu wa CECAFA. Hongera Malinzi.
Mambo kama kashfa za rushwa na upangaji matokeo, tuhuma za ukabila, matumizi mabaya ya fedha, ubabe kwa kufungia wapinzani wake, na mengine yanayofanana na haya ndio yamekuwa mambo ambayo utawala huu umekuwa ukihusishwa nayo. Ilifikia watu kuona Malinzi na wenzake wameturudisha kipindi cha FAT ya akina Ndolanga na Rage.
Lakini katikati ya haya yote kuna kitu kiko dhahiri, nacho ni mafanikio ya kisoka katika miaka hii ya TFF chini ya Malinzi kuliko vipindi vingi tu huko nyuma! Na ili wadau tutende haki ni lazima tuzungumzie mambo haya kwa nia ya ku -acknowledge badala ya kukosoa tu sikuzote. Wakati tunaendelea kumkosoa ili kumtia spidi gavana, Malinzi ametujibu kupitia mafanikio yafuatayo, tena kwa mpigo;
1. Azam kuwa bingwa wa vilabu vya Afrika Mashariki na Kati (KAGAME)
2. Yanga kuwa timu pekee ktk eneo la ukanda wa CECAFA kucheza makundi ya kombe la
shirikisho la CAF.
3. Kilimanjaro Queens kutwaa kibabe ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA)
4. Serengeti Boys kukaribia kufuzu kushiriki fainali za vijana za CAF.
5. Kuendelea kuimarika kwa ushindani wa Ligi ya VPL na kupungua kwa malalamiko dhidi ya waamuzi.
Ni ukweli si mafanikio ya maana sana, lakini kwa nchi ambayo tumekuwa tukiambulia patupu karibu kila michuano ya soka tunayoshiriki, angalau kuna kitu kinaonekana hasa tunapoanza kuwa wababe kwa wanyonge wenzetu wa CECAFA. Hongera Malinzi.