mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,778
- 7,145
KAGERA NI MUHAYA Turejee Historia. Wahaya ni nani? Jina Wahaya lilianza kutumika lini? Jina Wahaya linatokana na nomino IHAYA. Huu ni mwambao wa Ziwa Lweru.
Hadi ujio wa Wazungu lilimaanisha mwambao wa ziwa hilo sehemu za sasa Kyamutwara na Maruku. Ihaya lilikuwa ni eneo la vijiji vya wavuvi. Kwahiyo neno Wahaya lilimaanisha wavuvi. Katika kitabu cha Historia ya Bukoba, Hans Cory anasema jina Muhaya lilikuwa ni tusi dogo maana wavuvi hawakuwa na mahali pa kudumu pa kuishi na hawakuwa na mali ya kudumu.
Neno Ihaya halikuishia Kyamutwara na Maruku. Ihangiro ya zamani, uligawanyika sehemu mbili: Migongo na Omwihaya.
Kwa hiyo matumizi ya jina Wahaya yalienea hadi Ihangiro. Rekodi za wapelelezi wa Kizungu zinataja jina Buhaya. Omukama Rumanyika Orugundu alimwambia Speke: Mashariki mwa Karagwe kando ya ziwa kunaitwa BUHAYA ni maarufu kwa kilimo cha mibuni na pembe za ndovu. Mwisho wa kunukuu.
Katika vitabu vingine kama vile Victoria Nyanza, Karagwe ina sura yake na eneo lote Mashariki ya Karagwe wanaliita Kiziba.
Athari hiyo bado ipo Baganda huita Wahaya wote Baziba Jina Wahaya linaendana na jina jingine BUKOBA. Bukoba ni sehemu ya ukoo wa ABAKOBA. Ni pale kastamu.
Kwa kweli Bukoba kama eneo walikaa Wavuvi, Abahaya. Kuenea kwa matumizi ya majina Bukoba na Wahaya kuliambana na uvamizi wa wakoloni.
Wajermani walilipanua kujumuisha mji wa Bukoba, baadaye tawala zote za kando ya ziwa. Kwa wakati huo Karagwe haikujumuishwa. Na hata Omukama Ntare wa Karagwe walipomnyonga. Karagwe iliwekwa kwenye usimamizi wa Omukama Kahigi wa Kihanja ila ikabaki inajitegemea."
Hadi ujio wa Wazungu lilimaanisha mwambao wa ziwa hilo sehemu za sasa Kyamutwara na Maruku. Ihaya lilikuwa ni eneo la vijiji vya wavuvi. Kwahiyo neno Wahaya lilimaanisha wavuvi. Katika kitabu cha Historia ya Bukoba, Hans Cory anasema jina Muhaya lilikuwa ni tusi dogo maana wavuvi hawakuwa na mahali pa kudumu pa kuishi na hawakuwa na mali ya kudumu.
Neno Ihaya halikuishia Kyamutwara na Maruku. Ihangiro ya zamani, uligawanyika sehemu mbili: Migongo na Omwihaya.
Kwa hiyo matumizi ya jina Wahaya yalienea hadi Ihangiro. Rekodi za wapelelezi wa Kizungu zinataja jina Buhaya. Omukama Rumanyika Orugundu alimwambia Speke: Mashariki mwa Karagwe kando ya ziwa kunaitwa BUHAYA ni maarufu kwa kilimo cha mibuni na pembe za ndovu. Mwisho wa kunukuu.
Katika vitabu vingine kama vile Victoria Nyanza, Karagwe ina sura yake na eneo lote Mashariki ya Karagwe wanaliita Kiziba.
Athari hiyo bado ipo Baganda huita Wahaya wote Baziba Jina Wahaya linaendana na jina jingine BUKOBA. Bukoba ni sehemu ya ukoo wa ABAKOBA. Ni pale kastamu.
Kwa kweli Bukoba kama eneo walikaa Wavuvi, Abahaya. Kuenea kwa matumizi ya majina Bukoba na Wahaya kuliambana na uvamizi wa wakoloni.
Wajermani walilipanua kujumuisha mji wa Bukoba, baadaye tawala zote za kando ya ziwa. Kwa wakati huo Karagwe haikujumuishwa. Na hata Omukama Ntare wa Karagwe walipomnyonga. Karagwe iliwekwa kwenye usimamizi wa Omukama Kahigi wa Kihanja ila ikabaki inajitegemea."