Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Ni hivi:
Siyo Membe aliyesababisha biashara ya Korosho kudorora huko kusini. Ni maamuzi ya kukurupuka ndiyo yametufikisha hapa.
Ni sawasawa na walivyozuia wanunuaji wa Kahawa kutoka kwa madalali na matokeo yake kujikuta hawawezi kumtosheleza mkulima kwa soko bora na bei nzuri.
Jamani Mkapa alisema siyo kila lililofanywa na serikali za zamani ni la kipuuzi, mengine inafaa kuyachukua kuyaboresha na kusonga mbele, siyo kuweka question mark katika mambo ya maana!.
Asije akatokea mtu katika nchi hii akaingia madarakani akadhani kwamba amegundua matatizo ya watanzania ambayo watangulizi wake hawakuyajua!. Kwa mfano kama hoja ni vyeti feki BWM alikuwa anajua, JK alikuwa anajua. Ila may be hawakuamua kudeal navyo in the first place, au walikosa means za kudeal navyo ktk wakati huo. Huo ni mfano mmoja
Kama hoja ni mikataba mibovu ya serikali za nyuma kila atakayekalia hicho kiti atajua tu kwa sababu naye atakuwa na vyombo vilevile na instruments zilezile ambazo mwingine anazo!
Kwa hiyo cha msingi siyo kujua matatizo yapo au hayapo, HOJA YA MSINGI ni mbili
1. Kutokufanya makosa ambayo yalipelekea matatizo kuwepo in the first place
2. Kuja na mbinu BORA zaidi ya kuyaondoa hayo matatizo!
Wakati mwingine ni bora kusikiliza kauli, hoja na mitizamo mingine ili kuweza kufanya maamuzi yanayotokana na utafiti wa kina.
Ishu ya Korosho wabunge walipiga kelele sana, hawa ni wawakilishi wa wananchi, wanakuwa kule site, wanajua kero za wananchi, ukiwadismiss hawa as if ni wasaliti unadhani wananchi watafurahi?.
Kwa hiyo wananchi wanaona maslahi yao hayasimamiwi ipasavyo na wanaopaswa kuyasimamia. Kumtumbua huyu na yule hakuwezi kusolve ishu au kero ya mkulima.
Mkulima anataka soko la korosho, Pembejeo, Usafiri, Packaging nzuri etc etc. Hivi havipatikani kwa kumtumbua mtu!
Kulaumu watu, na kutafuta bangusilo wa kumtupia lawama haisaidii!
Membe siyo hata mtendaji wa kata, kudhani kwamba eti anakwamisha kwenye ishu ya korosho ni sawa na kupiga penati huku umefumba macho!
Siyo Membe aliyesababisha biashara ya Korosho kudorora huko kusini. Ni maamuzi ya kukurupuka ndiyo yametufikisha hapa.
Ni sawasawa na walivyozuia wanunuaji wa Kahawa kutoka kwa madalali na matokeo yake kujikuta hawawezi kumtosheleza mkulima kwa soko bora na bei nzuri.
Jamani Mkapa alisema siyo kila lililofanywa na serikali za zamani ni la kipuuzi, mengine inafaa kuyachukua kuyaboresha na kusonga mbele, siyo kuweka question mark katika mambo ya maana!.
Asije akatokea mtu katika nchi hii akaingia madarakani akadhani kwamba amegundua matatizo ya watanzania ambayo watangulizi wake hawakuyajua!. Kwa mfano kama hoja ni vyeti feki BWM alikuwa anajua, JK alikuwa anajua. Ila may be hawakuamua kudeal navyo in the first place, au walikosa means za kudeal navyo ktk wakati huo. Huo ni mfano mmoja
Kama hoja ni mikataba mibovu ya serikali za nyuma kila atakayekalia hicho kiti atajua tu kwa sababu naye atakuwa na vyombo vilevile na instruments zilezile ambazo mwingine anazo!
Kwa hiyo cha msingi siyo kujua matatizo yapo au hayapo, HOJA YA MSINGI ni mbili
1. Kutokufanya makosa ambayo yalipelekea matatizo kuwepo in the first place
2. Kuja na mbinu BORA zaidi ya kuyaondoa hayo matatizo!
Wakati mwingine ni bora kusikiliza kauli, hoja na mitizamo mingine ili kuweza kufanya maamuzi yanayotokana na utafiti wa kina.
Ishu ya Korosho wabunge walipiga kelele sana, hawa ni wawakilishi wa wananchi, wanakuwa kule site, wanajua kero za wananchi, ukiwadismiss hawa as if ni wasaliti unadhani wananchi watafurahi?.
Kwa hiyo wananchi wanaona maslahi yao hayasimamiwi ipasavyo na wanaopaswa kuyasimamia. Kumtumbua huyu na yule hakuwezi kusolve ishu au kero ya mkulima.
Mkulima anataka soko la korosho, Pembejeo, Usafiri, Packaging nzuri etc etc. Hivi havipatikani kwa kumtumbua mtu!
Kulaumu watu, na kutafuta bangusilo wa kumtupia lawama haisaidii!
Membe siyo hata mtendaji wa kata, kudhani kwamba eti anakwamisha kwenye ishu ya korosho ni sawa na kupiga penati huku umefumba macho!