Si sawa kumpongeza Mtu kwa uzuri alionao, hana mchango wowote kwa yeye kuwa hivyo

Si sawa kumpongeza Mtu kwa uzuri alionao, hana mchango wowote kwa yeye kuwa hivyo

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Sio tatizo kumpongeza Mtu alivyovaa na kupendeza, lakini ni vipi unampongeza Mtu kwa kuwa ni Mzuri au umbile lake zuri?...sio tatizo kumpongeza Mtu aliyefanya mazoezi na kutengeneza muonekano wa mwili (body building).

Hivi kwa akili zetu hizi huyo tunayempongeza ana mchango gani kumfanya yeye kuwa na muonekano huo wa sura au umbile?...yeye si amezaliwa tu na kujikuta yupo hivyo?...sasa sifa zinamuhusu nini?.

Sifa hutolewa kwa Mtu aliyejituma na kufanya bidii kufanikisha jambo fulani, iwe kwa kutumia nguvu zake au kwa kufikiri kwa bidii kufanikisha hilo alilolifanikisha.

Na kinyume chake basi pia ni kukosa busara kwa hali ya juu kumbeza, kumdhalilisha au kumkosoa anayeonekana kukosa mvuto wa sura na umbile.

Pia kwa maneno mengine basi ni ukosefu wa busara kwa aliye na mvuto kwa sura nzuri na umbile kujiona bora kuliko aliowazidi.
 
Ni kweli watu wanakosea kuwafanyia wengine body shaming knowing ts not their fault kuwa ivo ila ni wazaz hawakujitathmini kwmb kuna swala la kuharibu watoto.

Muhimu wanaume tujue pakuoa wakuu hakuna miujiza ktk uzao wetu,tabia ya mke ni muhimu ila tukumbuke kuna uzao pia inabid uish kwa amani duniani
 
Ni kweli watu wanakosea kuwafanyia wengne body shaming knowing ts not their fault kuwa ivo ila ni wazaz hawakujitathmini kwmb kuna swala la kuharibu watoto,,
Muhimu wanaume tujue pakuoa wakuu hakuna miujiza ktk uzao wetu,tabia ya mke ni muhimu ila tukumbuke kuna uzao pia inabid uish kwa amani duniani
Umeisha jiunga Jukwaa la Dini mkuu?
 
Mkuu lazima mtu apewe hongera. Kwa nini?
Kwa sababu kashinda. Kashinda nini?
Mbio.
Mbio zipi?
Mbio za kuogelea pale mimba inapotungwa. Kivip?
Mbegu moja iliyoogelea zaidi na kwa kasi kubwa ndio hufikia yai. Mbio zinazohusisha mambegu mabilioni halafu kamoja tu ndio hushinda. Kumbuka kila sperm na sura ake.
Mtu akiwa na sura nzuri Nasema hivi ASIFIWE TU
 
Back
Top Bottom