Siachi kutoa tip tangu nipitie kipindi kigumu

Siachi kutoa tip tangu nipitie kipindi kigumu

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,311
Reaction score
15,640
Si kwamba sikuwa na utaratibu wa kutowa tip, ila nilikuwa sijali na nilikuwa sioni kama inasaidia. Baada ya mimi kuyumba miaka fulani na kulazimika kujiajiri kwenye biashara fulani ambayo ndio ilinisitiri japo kuna siku unatoka kapa.

Ila kitu nilichojifunza kwa mtu kukupa buku au jero tu kama tip ilikua kubwa sana kwasababu kuna siku hata nauli mtu inatokea unakosa na jero uliyopewa inakusitiri, au buku inakuvusha mchana.

Tangu nimerudi kwenye mstari siachi kutoa tip sababu nimeelewa umuhimu na msaada inayompa mtu mradi tu usinihudimie vibaya.
 
Yeah ni muhimu japo kuna wahuni sana badala ya kula wanaishi na sigara kwa pesa unayompa. Inaleta kero sana.
 
Yeah ni muhimu japo kuna wahuni sana badala ya kula wanaishi na sigara kwa pesa unayompa. Inaleta kero sana.
Bora mvuta fegi kuna unawapa tip kwa jinsi MUNGU amekugusa Ila yeye anaidharau mpaka unaona nimempa ya Nini huyu boya asiyejua thamani ya "UTU'' au thamani " PESA"
 
Back
Top Bottom