Siasa Michezoni (Simba vs Al Ahly): Azam TV wanapaswa kuonywa, kuadhibiwa au kufungiwa!

Free Palestine ndio udini.????? Kwani Palestine WA anakaa waislamu peke Yao.???

Ila free Ukraine ilikuwa sio udini.???

Kuna watanzania hawa hawana akili za kufikiria hata kidogo ,wao kilichopo mbele Yao ndio wanakiamini.
Hivi umemuelewa mtoa hoja lakini?
Ebu rudia tena kusoma alichoandika.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Umejitahidi sana kuandika lakini kwa hali ilivyo huko Gaza yalipaswa kuwepo mabango mengi zaidi.
Israel ni magaidi kama magaidi wengine.
Kumbe wajinga mpo wengi kiasi hiki?

Andaa hata mabango milioni lakini usiyapeleke kwenye viwanja vya michezo. Siyo mahali pake, na taratibu za mpira zimepiga marufuku soka kutumika kwa mlengo tofauti.
 
Acha kukaza fuzu
 
Kumbe wajinga mpo wengi kiasi hiki?

Andaa hata mabango milioni lakini usiyapeleke kwenye viwanja vya michezo. Siyo mahali pake, na taratibu za mpira zimepiga marufuku soka kutumika kwa mlengo tofauti.
Sasa mbona Chawa huwa wanaingia na mabango yenye agenda za kisiasa na hampigi kelele?

Mbona HELA za " Magoli ya Wanasiasa" mnazipokea?

Azam Wako sahihi kabisa 😀😀
 
Bango tu inakuwa nongwa waacheni waweke mabango yao israili anazidi kuondoa roho za wapalestina huko
Wapalestina wawalaumu Hamas kwa yote wanayoyapitia.

Hivi Hamas waliamini baada ya kuua Wausrael zaidi ya 1,000, Waisrael wangrkaa kimya na kusema, asante Hamas kwa kuwaua watu wetu?

Ni dhahiri walijiandaa kwa haya yanayoendelea maana wamefanya hivyo mara nyingi, matokeo yake wanayajua, LAKINi waliamua kutenda waliyoyatenda.

Laana ya damu ba mateso ya Waisrael na wapalestina wasio na hatia, zitembee na Hamas na vizazi vyao. Ugaidi haujawahi kushinda, japo umefanikiwa kuzua taharuki.
 
Huwa najiuliza hivi mtu kuwa mpumbavu kiasi hiki inatokana na nini?

Unawashibokea wazungu kiasi hiki shida nini? Wazungu wako wanaamini katika Uhuru wa Maoni, walioshika Bango wametoa maoni Yao; wewe kijuso-kwinko mla chipsi yai unabinua kipuuzi-mbwa.

Nakushauri usidhihirishe sana upumbavu wako dada!
 
AZAM ni wadini sana, nshasema AZAM hawana ETHICS za habari. Matangazo yao yapo kidini zaidi na sijajua kwanini Wasirivoke leseni yao ya matangazo kutoka kuwa chombo cha habari cha kijamii SECULAR na kuwa cha kidini non SECULAR.
TCRA wanapambana na VPN jamani nji ii!!!!
 
Comments reserved
 
Fikiria Mashabiki wa Simba waende Misri na Bango la Kuisifu Izrael wakalioneshe uwanjani..

we fikiria tuu...

endelea kufikiria vizuri...

ndio maaana sheria zikawekwa kupiga marufuku hisia za kisiasa michezoni.
Hakuna sheria inayokataza kubeba bango la kupinga kitu fulani na mimi nikuulize swali fikiria mashabiki wa simba waende misri na bango la kuunga mkono wapalastine. Humanity has no Boundary
 
Swala hilo lina ukakasi mkubwa sana. Sijui sheria inasemaje kuhusu Vyombo vya habari. Ila kwa Wachezaji na timu zao, ipo very clear.

'Equipment must not have any political, religious or personal slogans, statements or images...For any offence the player and/or the team will be sanctioned by the competition organiser, national football association or by FIFA'.

Sasa, najaribu kupitia kuona kama kuna sheria inawabana mashabiki na vyombo vya habari juu ya swala la kuegemea upande mmoja kisiasa.
 
Biashala
Kuhalibikiwa
Matajili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…